Uwezo Tunao
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 6,942
- 1,190
NIMUONAVYO HUYU MALECELA MDOGO WA HUKO UGHAIBUNI NEW YORK
Nilikua namfuatilia vizuri sana tena kwa karibu mno huyu kijana mwenzetu Malecela Mdogo na nimegundua mambo yafuatayoa kwamba;
1. Ni Mtu wa kujishusha ajabu
(kila siku navutiwa na michango yake humu na hata kukiri kwake sawa tu MM Mwanakijiji hata kama kuna kutofautiana lakini kamwe hakuwahi kuonyesha upepo wa kuwa mmojawapo wamiliki wa JF.
2. Ni Mtu Mwenye Fikra Huru
Kila sentensi aitoayo wala haonyeshekusimamia saana mambo yapindishwe vipi ili huyu na au yule apate kufurahika. Anachoonyesha yeye ni kule kuruhusu FACTS zikajisimamie na kujieleza zenyewe tu hata kama Mwana-CCM na au Mwana-CHADEMA atanuna - brutally a liberal mind.
3. Uwezo wa Kujieleza ni ule wa Baba Yake
Ingawaje mimi ni miongoni mwa watu wengi sana tu JF niliyempinga sana Dada yake huyu bwana kupewa uteuzi ule na hata sasa bado napinga hilo, ila katika huyu bwana kwa muda mrefu ambayo nimepata kumfahamu nayo hapa JF nadhani ni rahisi mno kusamehewa nikisema kwamba kuna uwezekano mkubwa kajizaa mwenyewe Mzee Katapila mwenyewe kwa picha na ujana wa huyu kijana mwenzetu.
Wakati fulani mzee mmoja aliwahi kunichekesha saaaana kwamba katika taifa letu hili la Tanzania kuna watu wawili tu ambao hata kama ulikua umekasirika kuliko mnyama simba na hata kujichagulia kubeba mawe ukamponde nayo pindi atakapokuja kuwahutubieni wa watu mtajikuta mawe yakidondoka yenyewe tu PINDI TU MTAKAPOMPA JAPO KIJINAFASI KUJIELEZA - aliwataja watu hawa kuwa ni Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na John Samuel Malecela.
4. Uwezo wa Kujikosoa na hata Kukosoa Kile Anachokipenda
Jaama eeehhh, ni lazima tukubali kwamba moyo wa binadamu siku zote haiko neutral katika swala lolote lile; ni kule ama kupenda au kuchukia tu. Na watu tunapendelea kuponda tunachokichukia na kulilamba lamba lile tunalolipenda. Lakini ahuyu ndugu pamoja na Mwanakijiji ni wale watu nadra wenye kuweza kuponda anachokipenda na kulamba anachokichukia alimradi mantiki na ukweli wa mambo unaelekeza hivyo.
Lakini yooote juu ya yooote Bwana Malecela Junior, wewe kwa kila rangi uipendayo ni mpenda haki na kwa bahati mbaya saaaana ni miaka mingi sana tangu haki kugeuka bidhaa hadimu inayouzwa na CCM tu kwa majonzi makubwa sana ya walalahoi.
Hivyo, hebu tafakari taratibu kama kweli hautoonekana A SQUARE PEG IN A ROUND HOLE kuendeleza harakati zako kwa kugonga Mlango CCM Ukuta usiosikiliza cha mtu???
Hebu usirudie kosa la kuwa Katapilla kutengenezea watu barabara ya ulaji wao binafsi ndani ya CCM huku vijana wenzako tukifa njaa bila ya wa kutukaribisha karamuni kwa kuwa si watoto wa wakubwa.
Njoo CHADEMA leo; chama ambacho hata wamachinga tu au wakulima wakisimama kusema husikilizwa kwa heshima zote mpaka kituo na bila kuingiziwa maneno ya kinafiki ambayo yamekua kama utamaduni wa CCM kama vile - 'yanazungumzika' kumbe wanamaanisha tu kwamba wewe chokambaya hujui waliko watu wa aina yako.
Hata hivyo pamoja na mimi kukupa shime hapa wala isichukuliwe kwamba sitoweza kutofautiana na wewe ki-mjadala pale panapobidi. Kheri!!
Nilikua namfuatilia vizuri sana tena kwa karibu mno huyu kijana mwenzetu Malecela Mdogo na nimegundua mambo yafuatayoa kwamba;
1. Ni Mtu wa kujishusha ajabu
(kila siku navutiwa na michango yake humu na hata kukiri kwake sawa tu MM Mwanakijiji hata kama kuna kutofautiana lakini kamwe hakuwahi kuonyesha upepo wa kuwa mmojawapo wamiliki wa JF.
2. Ni Mtu Mwenye Fikra Huru
Kila sentensi aitoayo wala haonyeshekusimamia saana mambo yapindishwe vipi ili huyu na au yule apate kufurahika. Anachoonyesha yeye ni kule kuruhusu FACTS zikajisimamie na kujieleza zenyewe tu hata kama Mwana-CCM na au Mwana-CHADEMA atanuna - brutally a liberal mind.
3. Uwezo wa Kujieleza ni ule wa Baba Yake
Ingawaje mimi ni miongoni mwa watu wengi sana tu JF niliyempinga sana Dada yake huyu bwana kupewa uteuzi ule na hata sasa bado napinga hilo, ila katika huyu bwana kwa muda mrefu ambayo nimepata kumfahamu nayo hapa JF nadhani ni rahisi mno kusamehewa nikisema kwamba kuna uwezekano mkubwa kajizaa mwenyewe Mzee Katapila mwenyewe kwa picha na ujana wa huyu kijana mwenzetu.
Wakati fulani mzee mmoja aliwahi kunichekesha saaaana kwamba katika taifa letu hili la Tanzania kuna watu wawili tu ambao hata kama ulikua umekasirika kuliko mnyama simba na hata kujichagulia kubeba mawe ukamponde nayo pindi atakapokuja kuwahutubieni wa watu mtajikuta mawe yakidondoka yenyewe tu PINDI TU MTAKAPOMPA JAPO KIJINAFASI KUJIELEZA - aliwataja watu hawa kuwa ni Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na John Samuel Malecela.
4. Uwezo wa Kujikosoa na hata Kukosoa Kile Anachokipenda
Jaama eeehhh, ni lazima tukubali kwamba moyo wa binadamu siku zote haiko neutral katika swala lolote lile; ni kule ama kupenda au kuchukia tu. Na watu tunapendelea kuponda tunachokichukia na kulilamba lamba lile tunalolipenda. Lakini ahuyu ndugu pamoja na Mwanakijiji ni wale watu nadra wenye kuweza kuponda anachokipenda na kulamba anachokichukia alimradi mantiki na ukweli wa mambo unaelekeza hivyo.
Lakini yooote juu ya yooote Bwana Malecela Junior, wewe kwa kila rangi uipendayo ni mpenda haki na kwa bahati mbaya saaaana ni miaka mingi sana tangu haki kugeuka bidhaa hadimu inayouzwa na CCM tu kwa majonzi makubwa sana ya walalahoi.
Hivyo, hebu tafakari taratibu kama kweli hautoonekana A SQUARE PEG IN A ROUND HOLE kuendeleza harakati zako kwa kugonga Mlango CCM Ukuta usiosikiliza cha mtu???
Hebu usirudie kosa la kuwa Katapilla kutengenezea watu barabara ya ulaji wao binafsi ndani ya CCM huku vijana wenzako tukifa njaa bila ya wa kutukaribisha karamuni kwa kuwa si watoto wa wakubwa.
Njoo CHADEMA leo; chama ambacho hata wamachinga tu au wakulima wakisimama kusema husikilizwa kwa heshima zote mpaka kituo na bila kuingiziwa maneno ya kinafiki ambayo yamekua kama utamaduni wa CCM kama vile - 'yanazungumzika' kumbe wanamaanisha tu kwamba wewe chokambaya hujui waliko watu wa aina yako.
Hata hivyo pamoja na mimi kukupa shime hapa wala isichukuliwe kwamba sitoweza kutofautiana na wewe ki-mjadala pale panapobidi. Kheri!!
William kutokana na haya maelezo yako uliyoyatoa hapa baada ya kumjibu sikonge , haihitaji mtu kuwa na PHD kujua upeo wako, wewe jamaa nakupa big up sana , haya maelezo yamejitosheleza na ushauri mzuri sana umewapa hawa CCM sasa hivi naona wamepoteana njia huku wakiwa wamesahau kuwa ulishawapa taarifa kama hii, lakini ndugu yangu wewe hujui kuwa wafuasi wengi wa ccm ni wale wenzangu na mimi wa ndio mzee? % kubwa ya wafuasi wao wapo vijijini, na huo ndio mtaji wao, na hizi shule za kata zinazoibukia ndio kifo chao believe me, nakuhakikishia itafika wakati chama chenu kitapotea kabisaaa kwa sababu kila anayeelimika anakimbia ,na anayebaki ndani ya ccm ujue ana maslahi fulani(hapa sikuongelei wewe) nawaongelea vijana wengi ambao ndio wameajiriwa tu na sasa hivi wanatumia masaa manne au matano kwenda kazini kutokana na foleni,sasa huyu kijana utamwambia aje hapa JF kuitetea ccm akuelewe? kama mimi nikija hapa kuipigia debe then jioni nikiondoka kwenda nyumbani nakaa barabarani kwa mda wa masaa 4 na joto zaidi ya nyuzi 30 , mimi si nitakuwa taahira? kwa hiyo ndugu yangu ccm huu moto wameuwasha wenyewe na jinsi tunavyozidi kwenda mbele na jinsi vijana wengi wanavyozidi kupata elimu ndio ccm nayo itazidi kupotea na kudidimia , kinachotakiwa ni kuwasikiliza wananchi from the botom thats all, na kuwawajibisha watu thats all, mtu akifanya masikhara kazini anapigwa chini ,thats all