Muhingo Rweyemamu kulipwa fadhila?

Ex Spy

JF-Expert Member
Jan 15, 2007
213
1,726
Kuna nyeti imenifikia nikaona si vema kukaa kimya. Nia si kuwaharibia move (najua hawatabadili mawazo) lakini kutaka kujua kutoka kwenu wakuu.

Nyeti yenyewe iko hivi; Muhingo anaweza kuanza kazi rasmi TSN wakati wowote kuanzia sasa. Mipango inakamilishwa. Hivi ndio kulipwa fadhila au????
 
Kwa nini isiwezekane mkuu. Kama iliwezekana kwa Salva Rweyemamu why not Mhingo? Ndio anakuwa ME AU?
 
Alikokuwa ni gazetini na anakokwenda ni gazetini, hakuna fadhila zozote ni kazi tuu.

Muhingo kama Muhingo, ameshajijengea sifa ya msimamo na heshima yake katika tasnia ya habari, iwe ni katika kumtumikia papa, nyangumi au kafiri, ili mradi upate mradi wako.

Ni kweli TSN inatafuta ME kwa muda mrefu, calibre ya Muhingo kwa ME wa TSN ni bado. Kama Mkumbwa amemfundisha kazi Muhingo, shule zenyewe za enzi zile za TSJ, Mkumbwa kashindwa kupewa itakuwa Mhingo!.

Kwa vile jahazi za Habari corp linayumba yumba, kuna hatari ya kuzama, nahodha makini ni yule anaye toa alert kwa abiria kuhusu hatari iliyo mbele yao, na kutia nanga pwani yoyote ya karibu kuepuka tufani, ndicho alichofanya Muhingo, its a right move.

Habari Corp ni jahazi dogo, TSN ni chombo kikubwa, imara na hakiwezi zama, hivyo capt wa jahazi dogo hawezi panda chombo kikubwa na kuanzia u-captain, lazima ataanzia 2nd Off, then 1st Off ndipo afikiriwe u-capt.

Kama ni kweli, all the best kwa Muhingo.
 
Back
Top Bottom