Muhimu: Zijue athari za kuondoa thermostat kwenye gari yako

JituMirabaMinne

JF-Expert Member
May 4, 2020
3,327
9,298
Kuna msururu wa mafundi wengi ambao wamekuwa wakiwashauri wamiliki wa magari au wao wenyewe kuondoa thermostat katika gari bila kujua umuhimu wa hicho kifaa hasa pale gari inapoanza kuoverhit. Kwanza kabisa Thermostat ina kazi mbili kubwa katika engine. Ambazo ni:-

1. Kuifanya engine iwarm up haraka hadi kufikia operating temperature ya engine kwa kublock flow ya maji kutoka kwenye radiator kwenda kwenye engine.

2. Kuhakikisha engine inarun katika optimum temperature kwa kuruhusu tu maji ya baridi kuingia kwenye engine pale temperature inapokuwa imezidi ndani ya engine.

Nitaeleza athari kadhaa za kuendesha gari bila kuwa na thermostat.

1. Bila thermostat engine itarun katika cold condion. Kwa kawaida kama gari ina thermostat nzima basi coolant temperature itakuwa between 80 to 100 centigrade. Kama thermostat ikiondolewa basi temperature hiyo hupungua mpaka 50 centigrade. Hii hupelekea formation ya humidity ambayo ikicondese huja kuform sludge kwenye oil na hivyo kublock lubrication of the engine na hivyo kupelekea parts mbalimbali za engine kuwear. In a long run unaua engine yako.

2. Engine ikiwa katika cold condition ECT sensor itapeleka signal kwenye ECM kwamba engine ni ya baridi na hivyo ECM itakuwa inafikiri kwamba the engine need to start. Engine itawork kwenye closed loop (Wale wenye uelewa wa cold start za engine wanaelewa maana ya closed loop) na hivyo itakuwa inaburn more fuel na kuchafua mazingira.

3. Engine yako haitarun efficiently as engine huwa inarun efficiently in slightly rich mixture au slightly lean mixture depending kama unataka more power au more fuel economy. Sasa bila thermostat muda mwingi engine yako itarun in a richer mixture.

Pia kuna baadhi ya magari hasa magari ya wazungu ukiondoa thermostat utapata majibu ndani ya muda mfupi tu. Itakuwashia taa ya check engine n.k. Hivyo ni vema thermostat ikabaki pale ilipo. Kama imezingua weka nyingine.

Sasa nitarudi kwa baadhi ya watu hasa mafundi nyundo wengi ambao wanasema thermostat huku kwetu hazina umuhimu. Kwanza kabisa ukae ukijua thermostat zipo za aina mbalimbali na kichachozitofautisha ni Operating temperature. Zipo thermostat ambazo unaweza kutumia sehemu zenye baridi na zipo ambazo unaweza kutumia kwenye joto. Ni watu tu kutokuwa wafuatiliaji.

Mwisho kwa wamiliki wa magari. Hivi mtu anakuambia eti tuondoe hiki hakina umuhimu huku kwenye joto wakati before hapo ulikuwa unaendesha tu gari lako bila shida. Na wewe unamkubalia. Waliokiweka siyo wajinga.

Car Diagnosis, Engine service, Repair, Check engine, na mengine mengi.

Karibu Ofisini kwetu Dar es salaam, Sinza Kijiweni.

0688 758 625 au 0621 221 606
 
Na kingine huwa wanaunganisha radiator fan ku operate direct, ukiwasha tu gari inaanza nayo kufanya kazi kwa kisingizio isi-over heat

Sent using Jamii Forums mobile app

Yaani mkuu ni yaleyale. Hawa mafundi nyundo ambacho hawajui ni kwamba engine ina operating temperature yake. Ambayo ni (centigrade 82 plus or minus 3) za coolant.

Hivyo fan inatakiwa kuzunguka pale tu joto la coolant linapokuwa limezidi. Na kuiacha izunguke muda wote ni kuifanya engine ifanye kazi below working temperature yake na hivyo kuaffect the overall performance.
 
Kuna msururu wa mafundi wengi ambao wamekuwa wakiwashauri wamiliki wa magari au wao wenyewe kuondoa thermostat katika gari bila kujua umuhimu wa hicho kifaa hasa pale gari inapoanza kuoverhit. Kwanza kabisa Thermostat ina kazi mbili kubwa katika engine. Ambazo ni:-

1. Kuifanya engine iwarm up haraka hadi kufikia operating temperature ya engine kwa kublock flow ya maji kutoka kwenye radiator kwenda kwenye engine...
Yaani hapo ni tosha kabisa, hata bila maelezo. Mafundi wetu sijui huwa wanatoa wapi hizo hoja zao za kupingana na R&D ya manufacturers.
 
Yaani hapo ni tosha kabisa, hata bila maelezo. Mafundi wetu sijui huwa wanatoa wapi hizo hoja zao za kupingana na R&D ya manufacturers.

Hata hivyo shida kubwa watu wengi wengi ufundi wamejifunzia mtaani na most of them wamekaririshwa. Mafundi wengi hawana service manual za magari wanayotengeneza kwa hiyo ni mwendo wa kubahatisha tu.
Screenshot_20200524-092811.jpg
 
Hata hivyo shida kubwa watu wengi wengi ufundi wamejifunzia mtaani na most of them wamekaririshwa. Mafundi wengi hawana service manual za magari wanayotengeneza kwa hiyo ni mwendo wa kubahatisha tu. View attachment 1458160
Ni tatizo saana. Ukiwa na service manual na proper tools, karibu sehemu kubwa ya maintenance ni DIY. Mafundi wetu bado wanatumia knowledge ya ufundi wa 109.
 
Kwa kuongezea tu athari za kuondoa thermostat , kutaifanya Air condition kutofanya kazi vizuri as radiator inakuwa na joto Muda wote , kwa magari makubwa inaweza kuchangia kuchemsha pia hasa kwenye milima mirefu , maana maji yanakuwa yanachemshwa yote kwa pamoja .


Sent
 
Kwa kuongezea tu athari za kuondoa thermostat , kutaifanya Air condition kutofanya kazi vizuri as radiator inakuwa na joto Muda wote , kwa magari makubwa inaweza kuchangia kuchemsha pia hasa kwenye milima mirefu , maana maji yanakuwa yanachemshwa yote kwa pamoja .


Sent

Yeah upo sahihi sana mkuu. Mfano kwa wale ambao akiamka asubuhi windshield inakuwa na ukungu basi hataweza kudefrost ukungu ukatoka kwa sababu itachukua muda mrefu sana heater kupata moto.
 
Thermostat Ni muhimu sana , inashauriwa hata Kama imefail , ibadilishwe sio kutolewa , kuna sababu pia kwa nini maji yapo pale Kama coolant na sio liquid nyingine

Tuchukulie mfano huu, chemsha maji kiasi Lita 2 yafike boiling point kabisa 100c mathalan maji ya kupika ugali kabla hujaweka unga, then chukua maji baridi , kikombe cha chai uweke kwenye hayo maji yaliyochemka , kitakachotokea yataacha kuchemka na kuanza upya kuitafuta boiling point .

Mifumo wa thermostat ni kama nilivyoelezea hapo,inafungia maji kwenye engine na kuacha mengine ya baridi nje , joto likiongezeka kwenye engine inaruhusu kiasi kidogo Cha maji ya baridi yaingie kwenye engine na kuruhusu mengine yaende kwenye radiator ambapo Kuna maji mengi ya baridi, yakifika kule yanapozwa haraka , na haya maji ya baridi yaliyoingia kwenye engine yanafanya kama nilivoelezea hapo juu , cycle ni hiyo hiyo , japo inaweza kuongezeka frequency kutokana na kazi engine inafanya,

Faida zake ni kuwa
1 fan haitakuwa on muda mwingi Mana radiator inakuwa na kiasi kikubwa cha maji ya temp ndogo,

2.water pump itadumu sana Mana muda mwingi inakuwa imepumzika,

3.fuel consumption itakuwa nzuri maana , kuendesha fan na water pump Ni mzigo mwingine mkubwa tu hasa kwa magari makubwa,

4.Radiators zitadumu pia sababu kwa kupokea maji ya moto kwa muda mfupi tu, hasa radiator hzi za plastic,

5. Engine isiyo na thermostat huwa haina maisha marefu hii husababishwa liquid hammering ,maana muda mwingi cylinder zinakuwa na rich mixture ya mafuta , na hii huondoa ufanisi wa oil Kama kilainishi.

Sent
 
Thermostat Ni muhimu sana , inashauriwa hata Kama imefail , ibadilishwe sio kutolewa , kuna sababu pia kwa nini maji yapo pale Kama coolant na sio liquid nyingine

Tuchukulie mfano huu, chemsha maji kiasi Lita 2 yafike boiling point kabisa 100c mathalan maji ya kupika ugali kabla hujaweka unga, then chukua maji baridi , kikombe cha chai uweke kwenye hayo maji yaliyochemka , kitakachotokea yataacha kuchemka na kuanza upya kuitafuta boiling point...

Shukrani sana Mkuu yaani umeeleza vizuri sana.
 
Mkuu naomba uendelee kutupatia madini kuhusu magari...
Yaani mkuu ni yaleyale. Hawa mafundi nyundo ambacho hawajui ni kwamba engine ina operating temperature yake. Ambayo ni (centigrade 82 plus or minus 3) za coolant. Hivyo fan inatakiwa kuzunguka pale tu joto la coolant linapokuwa limezidi. Na kuiacha izunguke muda wote ni kuifanya engine ifanye kazi below working temperature yake na hivyo kuaffect the overall performance.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
duh afadhali kuna bwege mmoja nusu aniingize mkenge kisenge yan kuhusu iyo ishu ya kutoa thermostat..nikamwambia hii imekaa hapa kwa sababu walioweka sio wajinga
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom