Muhimu kwa Tume ya Katiba

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
Swala la Serikali tatu limeanza kupigiwa kelele na baadhi ya watu has wakidai ni mzigo kwa taifa. Wengi wa hawa wanaonekana ni wanaccm. Amelisemea Sumaye, Leo Sita naye kalisemea. Swali je, hawa viongozi na baadhi ya watu wanaopinga serikali tatu wnandhani hayo ni maoni ya tume imeamua kujiwekea yenyewe au ni maoni ya wanannchi? Je ni kweli hawa watu wana uchungu na walala hoi kubebeshwa mzigo wa kuendesha serikali tatu au wana ajenda zao binafsi? Ushauri kwa tume. Kablay ya rasimu kwenda kwenye mabaraza kuna umuhimu wa tume kufafanua hasa yale mabo yaliyokaa kitaalamu zaidi hasa hili la serikali tatu na mengine. La sivyo kutakuwa na upotoshaji mkubwa sana kwenye mabarzaya katiba na mwisho itakuwa vurugu mechi. Tafadhali Tume itoelee ufafanuzi vipengele ambavyo ni rahisi kupotoshwa.Binafsi naamini serikali tatu zitasaidia walau kuzuia kuvunjika kwa muungano haraka. lakini tukirudi kwenye serikali mbili muungano utavunjika immediately. Na serikali moja haiwezekani kwa sasa. Itakuwa balaa zaidi. Serikali moja ni tiketi ya wazi kuvunja muungano.
 
In short Samwel Sitta hajielewi, kwanza alisema wana mtandao wao unaoundwa na Dr. Mwakyembe, Dr. Magufuli, Membe, na Sitta mwenyewe; Dr. Magufuli akamkana live kuwa siyo mwana mtandao wa Samwel Sitta na kumtaka amuogope Mungu. Leo tena ametoka na single ya serikali mbili ambayo inapigiwa upatu na maCCM kwani wanajua, uwepo wa serikali tatu litakuwa pigo kwa mafisadi na wapambe zao.

Kauli ya huyu mzee Sitta inazua sintofahamu, ati uwepo wa serikali tatu ni mzigo; Yaani sisi wananchi tunapendekeza uwepo wa serikali tatu, Sita anadai ati ni gharama kubwa kuendesha hizo serikali. Kwani nani anaye beba huo mzigo wa hizo gharama ? Je ni Sitta na familia yake au ni sisi wananchi ? Endapo ni Sitta na familia yake ana haki kuongea hayo aliyo yanena otherwise ni mnafiki anaye tetea maslahi binafsi.
 
mmmmm Sidhani kama ni busara sana kuanza kumjadili Sitta au CCM kwani kila mtanzania anayo haki ya kusema yale anayofikiri ni sawa kwa mawazo na mtazamo wake.
Ni jambo lililo wazi(at least kwangu na si kwa sababu kasema Sitta au anybody else) kwamba Serikali Tatu ni Mzigo mkubwa na usio wa lazima kwetu!
Mmi kwa mawazo yangu Muungano huu kwa jinsi ulivyo hauna maslahi yoyote ya 'maana' kwa watanganyika wala wazanzibari na kwa hivo kuunda serikali Tatu kwa lengo la kuzuia usivunjike kwanza it will not work na kujiongezea tu mzigo bure japo ni kwa muda maana utavunjika tu!!
Ushauri wangu:1)Tuwe na Serikali MOJA au Tuachane na Muungano
2)Warioba na wenzake wamfanya walofanya Hatuhitaji waje tena kutu'kukubaliana na waloandika maana
hawajaandika matashi yao bali maoni ya watu(??????????)............
NIULIZE TU Hivi ni 'upuuzi'(samahani kwa kutumia neno hilo) gani huu walotuletea eti kila jimbo liwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa:MWANAMUME NA MWANAMKE eti ili kuweka usawa lol!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Serikali moja maana yake kuvunja muungano. Basi tuachane tu na huu muungano kwa sababu kero zimezidi. Mbona muungano umekuwa kama dini jamani?!
 
Back
Top Bottom