Muhimbili yakanusha kufa kwa watoto

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Lazima tulifuatilie swala hili hadi tujue ukweli umelalia wapi. Kama Muhimbili ndio wanasema ukweli kwamba hakuna vichanga vilivyopoteza uhai kwa kukosekana umeme, basi gazeti lililoandika habari ambazo hazikuwa na ukweli ni lazima lishutumiwe. Waandishi wa magazeti wanaoandika habari za uwongo siku zote lazima wapigwe vita hapa JF


habarileo; Friday,February 29, 2008 @06:11
Halima Mlacha

HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH), imekanusha taarifa kuwa watoto watano waliolazwa hospitalini hapo wamekufa kutokana na kukosa hewa baada ya kukatika umeme.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam leo na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano hospitalini hapo, Aminiel Aligaesha, hakuna mtoto yeyote aliyekufa kutokana na kukosekana kwa umeme hospitalini hapo.

"MNH inatoa ufafanuzi kuwa hakuna mtoto yeyote aliyekufa kutokana na kukatika kwa umeme, pia hakuna mashine zinazotumia umeme katika wodi ya watoto waliozaliwa njiti, ila kuna mashine za kuwapa joto," alisema Aligaesha.

Alisema hospitali hiyo ina jenereta sita ambazo umeme wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ukikatika tu, huunganishwa katika maeneo yote muhimu, ikiwamo wodi hiyo ya watoto waliozaliwa njiti.

Akizungumzia tukio hilo linalosadikiwa kusababisha vifo vya watoto watano, alisema umeme huo wa Tanesco ulikatika saa 9 usiku jana na jenereta hizo ziliwashwa usiku huo huo na kufanya kazi hadi saa 3 asubuhi.

"Ni dhahiri kuwa maeneo yote ya Muhimbili yaliathirika kutokana na kutokuwapo kwa umeme na ndiyo maana jenereta zetu ziliwashwa ili kuendelea kutoa huduma katika maeneo yote muhimu, ikiwamo maabara kuu (CPL), jengo jipya la wagonjwa wa nje (NOPD), vyumba vya kufanyia upasuaji, vyumba vya wagonjwa mahututi (ICU) na maabara maalumu ya watoto," alisema.

Alisema umeme wa Tanesco ulirejea kuanzia saa 7.30 mchana na hakuna madhara au tatizo lolote kubwa lililojitokeza.
 
... Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam leo na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano hospitalini hapo, Aminiel Aligaesha, hakuna mtoto yeyote aliyekufa kutokana na kukosekana kwa umeme hospitalini hapo...

No..No. No..It can be!!

Hatuwezi kuchezeana namna hii!! Habari zilitolewa kuwa hilo jambo lilitokea. Tena a solid report. Sasa hapa kuna habari kamili kabisa kuwa halikutokea... tunataka kujua ni nini kinaendelea...! Hizi ni habari mbili zinapisha completely. Lazima kiini kipatikane na hatua zichukuliwe pale itakapobainika pailikuwa na walakin!
 
... Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam leo na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano hospitalini hapo, Aminiel Aligaesha, hakuna mtoto yeyote aliyekufa kutokana na kukosekana kwa umeme hospitalini hapo...

No..No. No..It can be!!

Hatuwezi kuchezeana namna hii!! Habari zilitolewa kuwa hilo jambo lilitokea. Tena a solid report. Sasa hapa kuna habari kamili kabisa kuwa halikutokea... tunataka kujua ni nini kinaendelea...! Hizi ni habari mbili zinapisha completely. Lazima kiini kipatikane na hatua zichukuliwe pale itakapobainika pailikuwa na walakin!

Mara zote wanakanusha tu hata Wassira alipozomewa Mbeya alikanusha. Nafiiri hii ni style ya serikali ya JK.
 
Wale walio fiwa hawa watoto si wapo ? Kwani hawawezi kupatikana na hata ndugu zao ama wote wamesha hongwa na kuzibwa midomo ? Hebu leteni habari za maana hakuna mwandishi kichaa anaweza kusema kwamba watoto 5 wamekufa wakati ni uongo .Muhimbili waende Mahakamani tujue ukweli wa madai yao badala ya kubisha na kukaa kimya .
 
No..No. No..It can be!!

Hatuwezi kuchezeana namna hii!! Habari zilitolewa kuwa hilo jambo lilitokea. Tena a solid report. Sasa hapa kuna habari kamili kabisa kuwa halikutokea... tunataka kujua ni nini kinaendelea...! Hizi ni habari mbili zinapisha completely. Lazima kiini kipatikane na hatua zichukuliwe pale itakapobainika pailikuwa na walakin!

Nakuunga mkono mia kwa mia, lazima kiini kipatikane na hatua zichukuliwe pale itakapobainika palikuwa na walakin, iwe ni Uongozi wa Muhimbili au Mtoa habari za kusema watoto wamekufa.

Nini kifanyike ili kupata ukweli? haya wajuzi wa mambo tujuzeni.
 
Alisema hospitali hiyo ina jenereta sita ambazo umeme wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ukikatika tu, huunganishwa katika maeneo yote muhimu, ikiwamo wodi hiyo ya watoto waliozaliwa njiti.

Akizungumzia tukio hilo linalosadikiwa kusababisha vifo vya watoto watano, alisema umeme huo wa Tanesco ulikatika saa 9 usiku jana na jenereta hizo ziliwashwa usiku huo huo na kufanya kazi hadi saa 3 asubuhi.

Jenereta ziliwaka au ziliwashwa? Automatic haziwashwi.Kwa nini mtu asiende kuhakikisha kama kweli kuna mashine za kupumulia zinazotumia umeme kwenye wodi hizo? Ni vizuri kuhakikisha hakuna mashine za namna hiyo zinazohamishika! Kama ni kweli hivyo, itabidi Muhimbili waombwe radhi kwa kudhalilishwa bila sababu.
 
Wale walio fiwa hawa watoto si wapo ? Kwani hawawezi kupatikana na hata ndugu zao ama wote wamesha hongwa na kuzibwa midomo ? Hebu leteni habari za maana hakuna mwandishi kichaa anaweza kusema kwamba watoto 5 wamekufa wakati ni uongo .Muhimbili waende Mahakamani tujue ukweli wa madai yao badala ya kubisha na kukaa kimya .

Kwa nyumbani kukanusha ni staili yetu!
Naweza kusema kuwa saa nyingine kuna vitisho zaidi kuliko hongo ambayo watuhumiwa huwa wanakumbana navyo wanapotaka kutoa ushahidi.

Nakumbuka kulikuwa na Dr. mmoja(muhimbili-watoto) alikuwa nafanya part time ktk kijiwe nilichokuwa nabangaiza mimi, alitusimulia mkasa ulivyovikuta vitoto njiti usiku uliopita pale MNH, kwamba vilizidishiwa joto (kwa bahati mbaye) na vikafa, ikabidi wavilainishe kwa 'moisture' ili vionekane vilikufa natural death.

Wakati ule kama tulivyo waTZ niliishia kushangaa tu!

Yes naamini kuwa watoto hao walikufa kwa kukosa hewa kwa ajili ya kukatika kwa umeme.
 

“MNH inatoa ufafanuzi kuwa hakuna mtoto yeyote aliyekufa kutokana na kukatika kwa umeme, pia hakuna mashine zinazotumia umeme katika wodi ya watoto waliozaliwa njiti, ila kuna mashine za kuwapa joto,” alisema Aligaesha.
Hizo mashine za joto zinatmia nini kama si umeme?
 
Hizo mashine za joto zinatmia nini kama si umeme?

Haswa, Mkuu! Isije ikawa uongozi wanataka kutumia semantics kukwepa kuwajibika. Labda kilichosababisha vifo ni kuzima kwa hizi incubators na si kama walivyodhani waliofiwa! hii haibadilishi kitu. Kama uzembe ulifanyika ni lazima uanikwe. Kama ni makosa ya kiutendaji, ni bora kukiri na kuweka mikakati ya kuzuia kutokea tena. asante Mkuu!
 
Walotoa 'habari' za kufa kwa watoto hao kwa kukosa hewa walikua na conclusion kwamba watoto walikufa kwa kukosa hewa (kwa umeme kukatika kwa kama dakika 10 walitoa mfano wa kwenye lifti) ....... Muhimbili wanasema kwamba zile mashine ni kwa ajili ya kuwapatia joto njiti wanaozaliwa Muhi2. Labda kama mtaalam wa mambo hayo anaweza kufafanua zaidi, lakini ufafanuzi wa Muhi2 ni logical.

Naona huyo mwandishi hakufanya homework yake vizuri, ikumbukwe pia sio kila kinachotoka kwa waandishi wa habari (especially Tz) kinakua cha kweli. Kwa sehemu ya joto kama Dar mashine haziwezi kupoteza joto kiasi cha kusababisha kifo, within 10 minutes.

So, unless someone proves otherwise Muhimbili is in the right side on the matter.
 
Hizo mashine za joto zinatmia nini kama si umeme?

Nadhani hapa kuna mambo mawili ya kufahamu:

1) mashine za joto hata kama zinatumia umeme, haziwezi kupata baridi immediately ukikatika umeme, yaani specifications za mashine hizi kuzuwia joto zinapokuwa hazina umeme hutegemea na hali ya ubaridi ya sehemu zilizowekwa, kuna zinazozuwia joto baada ya kukatika umeme, kwenye sehemu ya baridi la kawaida la chumbani, kwa dakika 15 mpaka masaa mawili. Kwa hilo, umeme wa kukatika dakika 10 hauwezi kusababisha madhara ya kifo kwa kukosekana kwa joto kwa mashine hizo.

2)Kangaroo Care ni method inayotumika sana kwa sasa na kwa kiasi kikubwa inakuwa encouraged duniani, na hapa kwetu Tanzania inatumika na inafahamika sana hata kwenye mahospitali mengi ya wilaya na zahanati zisizokuwa na mashine za kutumia joto la umeme. Method hii ingetumika kama kuna hatari yoyote iliyooonekana kuwa itajitokeza kwa kukosa umeme na ni very effective.

Kwa hiyo kama ni umeme wa kukatika kwa dakika 10 na mashine joto kuzimika ndio kusababishe vifo vya watoto, sababu hiyo haiingii akilini, labda kuwe na sababu nyingine kabisa na labda iwe ni ya mashine aina zingine kabisa na si hizi za joto, kwani hata kama hazipo hizi mashine za joto still kuna Kangaroo Care ambayo ndio inatumika sana kwetu kuliko hizo mashine.

Kangaroo care is a way of holding a preterm or full term infant so that there is skin-to-skin contact between the infant and the person holding it. The baby, wearing only a diaper, is held against the parent's bare chest. Kangaroo care for preterm infants is typically practiced for two to three hours per day over an extended time period in early infancy. With babies who are medically stable, there is no maximum duration for kangaroo care, some parents may keep their babies in-arms for many hours per day...

source: http://en.wikipedia.org/wiki/Kangaroo_care
 
Nadhani hapa kuna mambo mawili ya kufahamu:

1) mashine za joto hata kama zinatumia umeme, haziwezi kupata baridi immediately ukikatika umeme, yaani specifications za mashine hizi kuzuwia joto zinapokuwa hazina umeme hutegemea na hali ya ubaridi ya sehemu zilizowekwa, kuna zinazozuwia joto baada ya kukatika umeme, kwenye sehemu ya baridi la kawaida la chumbani, kwa dakika 15 mpaka masaa mawili. Kwa hilo, umeme wa kukatika dakika 10 hauwezi kusababisha madhara ya kifo kwa kukosekana kwa joto kwa mashine hizo.

2)Kangaroo Care ni method inayotumika sana kwa sasa na kwa kiasi kikubwa inakuwa encouraged duniani, na hapa kwetu Tanzania inatumika na inafahamika sana hata kwenye mahospitali mengi ya wilaya na zahanati zisizokuwa na mashine za kutumia joto la umeme. Method hii ingetumika kama kuna hatari yoyote iliyooonekana kuwa itajitokeza kwa kukosa umeme na ni very effective.

Kwa hiyo kama ni umeme wa kukatika kwa dakika 10 na mashine joto kuzimika ndio kusababishe vifo vya watoto, sababu hiyo haiingii akilini, labda kuwe na sababu nyingine kabisa na labda iwe ni ya mashine aina zingine kabisa na si hizi za joto, kwani hata kama hazipo hizi mashine za joto still kuna Kangaroo Care ambayo ndio inatumika sana kwetu kuliko hizo mashine.

Kangaroo care is a way of holding a preterm or full term infant so that there is skin-to-skin contact between the infant and the person holding it. The baby, wearing only a diaper, is held against the parent's bare chest. Kangaroo care for preterm infants is typically practiced for two to three hours per day over an extended time period in early infancy. With babies who are medically stable, there is no maximum duration for kangaroo care, some parents may keep their babies in-arms for many hours per day...

source: http://en.wikipedia.org/wiki/Kangaroo_care

Asante kwa ufafanuzi wako makini. Kwa bahati mbaya kutokana na sababu za kihistoria ni wachache watakaoamini kuwa Muhimbili walikuwa blameless kwenye hili. Inavyoelekea hao wanaoitwa wafiwa si wataalamu kwa hiyo wamesema walivyoelewa wao. Ili Muhimbili wajikoshe, itakuwa vyema wakitufahamisha kama kuna vifo vilitokea katika idara hiyo siku hiyo na vilisababishwa na nini! Walioandika habari hii wawafuate waliohusika na kupata vithibitisho (death certificate) kutoka kwao kuhusu suala zima. Mkuu hiyo kangaroo care isingewezekana kutokana na maelezo yao maana wanadai walizuiwa kuingia kwenye chumba hicho! Au kangaroo care hiyo wanaweza kutoa wauguzi? Wauguzi wetu wa Bongo?
Samahanini kwa size ya font!
 
waliofiwa vipi walihojiwa na mwandishi aliyeandika hizo habari au wanasemaje kuhusu hili?lakini nina wasiwasi sana na muhimbili tangu wapasue mtu kichwa badala ya mguu,hawana credibility hawa lazima wachunguzwe vizuri na wawajibishwe maana kukanusha pale ni order of the day....inaudhi sana hii style ya ufanyaji kazi mana hata kina Lowassa na Karamagi hawakubali mpaka leo na kututia hasara kubwa kiasi kile,watu lazima waanze kuwa na culture ya kuwajibika sasa kama wamefanya makosa itatusaidia kwenda mbele kuliko kubishana tuu!
 
Asante kwa ufafanuzi wako makini. Kwa bahati mbaya kutokana na sababu za kihistoria ni wachache watakaoamini kuwa Muhimbili walikuwa blameless kwenye hili. Inavyoelekea hao wanaoitwa wafiwa si wataalamu kwa hiyo wamesema walivyoelewa wao. Ili Muhimbili wajikoshe, itakuwa vyema wakitufahamisha kama kuna vifo vilitokea katika idara hiyo siku hiyo na vilisababishwa na nini! Walioandika habari hii wawafuate waliohusika na kupata vithibitisho (death certificate) kutoka kwao kuhusu suala zima. Mkuu hiyo kangaroo care isingewezekana kutokana na maelezo yao maana wanadai walizuiwa kuingia kwenye chumba hicho! Au kangaroo care hiyo wanaweza kutoa wauguzi? Wauguzi wetu wa Bongo?
Samahanini kwa size ya font!

Hata kama usemavyo kuwa kangaroo care isingeweza kutumika, still tunarudi poit A, wasingeweza kufa kwa sababu za kukosekana joto kwa mashine joto kukosa umeme kwa dakika kumi. Kama nilivyosema labda kuwe na sababu nyingine. Muhimbili wameshasema, hakuna hivyo vifo, soma juu mwanzo wa thread. Sasa hao waandishi ndio wawa-prove wrong hao Muhibili. Waandishi wa hizo habari walete data za kueleweka, ni mashine gani zilizosababisha vifo, wakati gani umeme ulikatika, majina ya familia walizofiwa na kadhallika. Muhimbili washarudisha mpira kwa waandishi wa hizo habari na kama muhimbili ni waongo na wakweli ni hao waliotowa hizo habari basi ni wakati muafaka waku-prove waliandikalo. Unajauwa kuandika kuhusu vifo hasa hivi vinavyoonekana vimesababishwa kwa uzembe hautakiwi ukurupuke na inachotakiwa uwe na data kamili na kama hauna data kamili unaweza kushitakiwa ukajuta kwanini umekuwa muandishi.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam leo na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano hospitalini hapo, Aminiel Aligaesha, hakuna mtoto yeyote aliyekufa kutokana na kukosekana kwa umeme hospitalini hapo.

“MNH inatoa ufafanuzi kuwa hakuna mtoto yeyote aliyekufa kutokana na kukatika kwa umeme, pia hakuna mashine zinazotumia umeme katika wodi ya watoto waliozaliwa njiti, ila kuna mashine za kuwapa joto,” alisema Aligaesha.


Dar es Salaam, walichosema Muhimbili ni kuwa hakuna mtoto aliyekufa KUTOKANA NA KUKOSEKANA UMEME hospitalini hapo na si hakuna kifo kilichotokea. Hili suala lina unatata na kwa vile Muhimbili ndiyo historically hawaaminikiwi na jamii inabidi watoe ufafanuzi. Waseme tu kama kuna vifo vilivyotokea siku hiyo vilisababishwa na nini! Haya majibu ya mume wa Hillary Clinton hayawasaidii. Au mwenzetu na wewe uko Muhimbili?
 
Dar es Salaam, walichosema Muhimbili ni kuwa hakuna mtoto aliyekufa KUTOKANA NA KUKOSEKANA UMEME hospitalini hapo na si hakuna kifo kilichotokea. Hili suala lina unatata na kwa vile Muhimbili ndiyo historically hawaaminikiwi na jamii inabidi watoe ufafanuzi. Waseme tu kama kuna vifo vilivyotokea siku hiyo vilisababishwa na nini! Haya majibu ya mume wa Hillary Clinton hayawasaidii. Au mwenzetu na wewe uko Muhimbili?

Kusema kweli sijakuelewa kuhusu"hillary Clinton".

Hapana sipo Muhimbili na sina interest yoyote na Muhimbili ila kutibiwa au kwenda kutembelea wagonjwa.

Nilichokiele\za mimi ni sababu ambazo nimeona haziingii kichwani na haziwezekani technically na nimesema wazi kabisa labda kuwe na sababu nyingine. Na nimejaribu ku-encourage waandishi kuwa hii ndio nafasi yao ya kutujulisha umma kuwa wako right na Muhimbili wako wrong, wakishindwa kwa hili sijui ninani wakulaumiwa.

Muhimbili siitetei hata kidogo kwa mambo mengi ya msingi lakini nina principal ya "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni".
 
Kusema kweli sijakuelewa kuhusu"hillary Clinton".

Hapana sipo Muhimbili na sina interest yoyote na Muhimbili ila kutibiwa au kwenda kutembelea wagonjwa.

Nilichokiele\za mimi ni sababu ambazo nimeona haziingii kichwani na haziwezekani technically na nimesema wazi kabisa labda kuwe na sababu nyingine. Na nimejaribu ku-encourage waandishi kuwa hii ndio nafasi yao ya kutujulisha umma kuwa wako right na Muhimbili wako wrong, wakishindwa kwa hili sijui ninani wakulaumiwa.

Muhimbili siitetei hata kidogo kwa mambo mengi ya msingi lakini nina principal ya "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni".

Mume wa Hillary Clinton alipoulizwa kama aliwahi kuvuta bangi wakati wa ujana wake alijibu" nilijaribu lakini sikumeza moshi". na kwa Monica akasema," naomba mnisikilize kwa makini, sijawahi kuwa na UHUSIANO wa kimapenzi na mwanamke huyo". Kwa kifupi, ni majibu ya kiwakili ya kukwepa kusema ukweli!

Nimekuelewa, Mkuu. Nilikuwa nakutania tuu kuhusu kufanyakazi Muhimbili.
 
Kama hawa Waandishi wamezua mambo ya uongo basi watake responsibility!

Kuandaika mambo ya uongo sii poa kabisa!

Taabu ya waandishi Tz sii wepesi kuomba msamaha kama wamekosea.. wanapenda sana malumbano!
 
Back
Top Bottom