Muhimbili: Rais Magufuli awatembelea na kuwapa pole majeruhi wa ajali ya moto Morogoro

wakatanta

JF-Expert Member
Feb 5, 2018
2,593
3,148
Rais John Magufuli, amewatembelea majeruhi walionusurika na ajali ya moto uliotokana na lori la mafuta kupinduka na kulipuka mkoani Morogoro jana Agosti 10, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Majeruhi hao walifikishwa hospitalini hapo jana saa nne usiku.

index.jpg

AJALI YA MOTO MOROGORO: RAIS MAGUFULI AWATEMBELEA MAJERUHI, AWAPA 500,000 KILA MMOJA

Majeruhi hao 43 wamelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili walipopelekwa kutoka hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Kati ya 46 waliofikishwa jana, watatu wamefariki dunia leo

Aidha, Rais Magufuli amewashukuru wauguzi pamoja na madaktari kwa huduma nzuri na kuwazawadia Tshs. milioni 1

Amewaagiza kuwahudumia majeruhi hao na kuwapatia mahitaji yoyote wanayohitaji kwa gharama ya Serikali
Rais wa wanyonge Dr. John Pombe Magufuli tunashukuru kwa upendo wako,kwa faraja uliyowapa wagonjwa hakika waliokata tamaa ya maisha sasa wamepata ahueni kwa ujio wako hapa Hospitali ya Muhimbili..

Wagonjwa wanapokea laki tano taslimu, wagonjwa waliopo ICU wanapewa milioni moja wagawane kwa ajili ya mahitaji

Madaktari wanapewa milioni moja kwenye chumba wagawane kama motisha

Asante mzee
 
Rais wa wanyonge Dr john pombe magufuli tunashukuru kwa upendo wako,kwa faraja uliyowapa wagonjwa hakika waliokata tamaa ya maisha sasa wamepata ahueni kwa ujio wako hapa hospital ya muhimbili..

Wagonjwa wanapokea laki tano cash
Wagonjwa Waliopo ICU wanapewa million moja wagawane kwa ajili ya mahitaji

Madaktari wanapewa milioni moja kwenye chumba wagawane kama motisha

Mwisho ameagiza majeruhi wote watibiwe kwa gharama yoyote ile na serikali itagharamia
Asante mzee
 
Je wale wagonjwa walilazwa sehemu nyingine vipi nao wamepewa ??
Rais wa wanyonge Dr john pombe magufuli tunashukuru kwa upendo wako,kwa faraja uliyowapa wagonjwa hakika waliokata tamaa ya maisha sasa wamepata ahueni kwa ujio wako hapa hospital ya muhimbili..
Wagonjwa wanapokea laki tano cash
Asante mzee
 
Pia kawapatia laki 5 kila mgonjwa,hakika ni kiongozi bora sana
Tatizo sio kugawa laki tano, laki tano ina maana gani kwa watu walikufa na kujeruhiwa? leo unatoa laki tano na kesho tena utatoa? Hiyo akili au ujinga?

Kikosi cha moto kiboreshwe, jeshi la polisi liboreshwe!!

Bado hatujajifunza kwenye ile ajali ya meli...


Huu ni upumbavu mkubwa sana.
 
Rais wa wanyonge Dr john pombe magufuli tunashukuru kwa upendo wako,kwa faraja uliyowapa wagonjwa hakika waliokata tamaa ya maisha sasa wamepata ahueni kwa ujio wako hapa hospital ya muhimbili..
Wagonjwa wanapokea laki tano cash
Madaktari wanapewa milioni moja kwenye chumba wagawane kama motisha
Asante mzee
Kugawa laki tano ni upuuzi bila kuboresha kikosi cha zima moto!!

Moto unatoa alafu zima moto halina maji alafu unaenda kutoa laki tano kwa majeruhi?

Hii ni akili? Na kesho ikitokea tena ajali utatoa laki ngapi?

Bado hatujajifunza kwenye ile ajali ya meli...
 
Sana!Ila ingekuwa mimi ningewapa bima ya NHIF kwa wale ambao hawana!

Kwa mtu ambaye hana bima ya afya malipo kwa mwaka ili apate bima ya afya ni sh. 1,500,000 ambapo ataitumia yeye na mume/mke na wategemezi wanne.( I stand to be corrected)
 
Kugawa laki tano ni upuuzi bila kuboresha kikosi cha zima moto!!

Moto unatoa alafu zima moto halina maji alafu unaenda kutoa laki tano kwa majeruhi?

Hii ni akili? Na kesho ikitokea tena ajali utatoa laki ngapi?

Bado hatujajifunza kwenye ile ajali ya meli...

Mkuu ngoja kwanza hili lipite kuna majeruhi wapo humu ndio kichwa cha familia huko nyumbani ni njaa tupu watoto hawapati ugali,
Mh Rais ameliona hili
 
Rais John Magufuli, amewatembelea majeruhi walionusurika na ajali ya moto uliotokana na lori la mafuta kupinduka na kulipuka mkoani Morogoro jana Agosti 10, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Majeruhi hao walifikishwa hospitalini hapo jana saa nne usiku.

Au serikali imetengeneza ujanja ili namba wani aonekane anahuruma.toeni elimu hawa hawataungua tena
 
Back
Top Bottom