Elections 2010 Mugabe anamshauri jk?

niweze

JF-Expert Member
Oct 21, 2009
1,008
116
Tunaona Jinsi Gani JK Anachofanya Tanzania na Tutajiuliza Anavipata Wapi? Zimbabwe na Tanzania Inauhusiano Mkubwa Sana Hasa ZANU-PF na CCM. Ukiangalia Uchaguzi wa Tanzania Ulivyoendeshwa ni Sawa Kabisa na Huko Zimbabwe. ZANU-PF Walifanya Vile Vile na Kuwatishia Wananchi Wao Wapinzani na Kuwaita Kila Aina ya Majina. ZANU-PF Walitumia Vyombo vya Usalama na Vyombo vya Habari Kuwadanganya Wananchi Wao. Sijui Kama Kuna Swali la Kuuliza Ni Nani Anawashauri CCM na JK. NEC Walichokifanya ni Kufuta Matokeo Yote Toka Kwenye Majimbo Nchi Nzima na Kusuka Mapya ya JK. Hapa Ndipo Tulipo Sasa. Haya Chadema na Wananchi Wanataka "Katiba" na Hapa Tutamlinganisha DR Slaa na Morgan Tsvangirai (MDC-T) wa Zimbabwe. Morgan Alifungwa, Mke Wake Kuuliwa na Kukataa Kunyanyaswa Nchini Kwake na Dr Slaa Yupo Karibu Sana Kuwekwa Ndani na Baadhi ya Kikundi cha CCM cha Polisi, Wanachokifanya Wanatafuta Sababu Tu Sasa. Swala la "Katiba" Limekataliwa Tanzania Kama ZANU-PF Zimbabwe, Nani Anamshauri JK?

"Tuna Ushahidi Tosha Tanzania Inaelekea Njia ya Zimbabwe na Ivory Coast. Wengi Tunajua Lazima Tuzuie Nchi Yetu Kwenda Zimbabwe Before It's Too Late"
 
Back
Top Bottom