Elections 2010 Mugabe amponza Kikwete

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Kuhudhuria kwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe wakati wa kuapishwa kwa rais Kikwete kunaelezwa na wanazuoni huenda ikawa sababu ya nchi nyingi hasa za magharibi kusita kumpongeza rais Kikwete aliyeapishwa leo.

Nchi hizo za magharibi zenye ushawishi mkubwa duniani zikiwemo Marekani na Uingereza, pamoja na kuwakilishwa na mabalozi wake inasemekana hadi sasa hazijatuma salamu za pongezi za kuchaguliwa kwa Kikwete kitu ambacho si kawaida yake.

Ikumbukwe kuwa wakati wa uchaguzi uliopita wa Zimbabwe ambao ulilalamikiwa sana na UK na USA kuwa haukuwa huru na wa haki umepelekea hadi leo Mugabe na familia yake kunyimwa hati ya kuingia katika nchi hizo isipokuwa kuhudhuria mikutano ya UN pekee.

Wachambuzi wa mambo wanahisi tukio la leo kwa Mugabe kuhudhuria linaweza kuwa limetia doa mahusiano ya Tanzania na nchi hizo ikizingatiwa kuwa kuna madai yanayotolewa na chama cha upinzani Tanzania kuwa kulikuwa na udanganyifu wa kura wakati wa kuhesabu.
 
wakimnyime kwenda US watatusaidia kiasi furani maana hizo safari zina tucost sana halafu ukimuuliza anasema anaenda kuhemea ****
 
kuhudhuria kwa rais wa zimbabwe robert mugabe wakati wa kuapishwa kwa rais kikwete kunaelezwa na wanazuoni huenda ikawa sababu ya nchi nyingi hasa za magharibi kusita kumpongeza rais kikwete aliyeapishwa leo.

Nchi hizo za magharibi zenye ushawishi mkubwa duniani zikiwemo marekani na uingereza, pamoja na kuwakilishwa na mabalozi wake hadi inasemekana hadi sasa hazijatuma salamu za pongezi za kuchaguliwa kwa kikwete kitu ambacho si kawaida yake.

Ikumbukwe kuwa wakati wa uchaguzi uliopita wa zimbabwe ambao ulilalamikiwa sana na uk na usa kuwa haukuwa huru na wa haki umepelekea hadi leo mugabe na familia yake kunyimwa hati ya kuingia katika nchi hizo isipokuwa kuhudhuria mikutano ya un pekee.

Wachambuzi wa mambo wanahisi tukio la leo kwa mugabe kuhudhuria linaweza kuwa limetia doa mahusiano ya tanzania na nchi hizo ikizingatiwa kuwa kuna madai yanayotolewa na chama cha upinzani tanzania kuwa kulikuwa na udanganyifu wa kura wakati wa kuhesabu.

eu walishakata fungu,uk na us wakikata fund pia mbona tutakula hata vyura!!!
 
Itakuwa jambo la mbolea donors wakikata funds ili serikali itie akili na kusikiliza malalamiko hasa ya uchakachuaji wa kura
Mbaya zaidi walimwalika so it was intentional
 
Uchunguzi wa Mwananchi ulibaini kuwa kabla na baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Dk. Slaa alikuwa kwenye ofisi za makao makuu ya Chadema ambako ilielezwa kuwa alikuwa na "vikao muhimu".
Kaimu katibu mkuu wa Chadema, John Mnyika ambaye pia ni mbunge mteule wa Jimbo la Ubungo, alisema Dk Slaa alikuwa akikutana na mabalozi wa nchi mbalimbali na kwamba aliendelea na vikao hivyo jana na pia alikutana na viongozi wa dini mbalimbali nchini.

Hata hivyo, Mnyika hakuwa tayari kueleza kilichokuwa kikijadiliwa katika vikao hivyo baina ya Dk. Slaa na mabalozi kwa upande mmoja, pia viongozi wa dini kwa upande mwingine.
Gazeti la Mwananchi
 
nchi hii ipigwe BAN tule mapka vyura ndo tutatia akili...mijitu mijizi ya kura vibaya sanaaa
 
nchi hii ipigwe BAN tule mapka vyura ndo tutatia akili...mijitu mijizi ya kura vibaya sanaaa

Ya Mugabe yana sura 2:

Kwanza, alionewa kweli na wakoloni na ndiyo maana aliwafurumisha.
Pili, njia aliyotumia kuwafurumsha ndo pekee inayoweza kuwa CRITISIZED.

For me Mugabe is a HERO, but on another hand, he did it wrongly!
 
Interesting news. I didn't know Zimbabwe's dictator was good friends with Tanzania's dictator.
 
Interesting news. I didn't know Zimbabwe's dictator was good friends with Tanzania's dictator.

Vijana someni historia ili mjue mchango wa nchi hii kwa ukombozi wa nchi kama Zimbabwe. Wakina Mugabe wamelelewa hapa kwetu kisiasa kwahiyo uhusiano wa CCM na ZANU PF ni wa damu!! Ndio maana huwezi kusikia hata siku moja Tanzania ikimcriticize Mugabe.
 
OMG Wamarekani hawajatupigia chafya usoni, labda uturi tuliojipaka hauwavutii, tutafute mwingine.

Issue ya Mugabe na Kikwete ilianza kupamba moto Zambia katika mkutano wa SADC, mara baada ya Kikwete kuchukua urais. Kikwete akataka kujifanya ana kibesi cha urais kumsema Mugabe, Mugabe alimpaka undiplomatically basically akimwambia kaa chini dogo sie tumecheza na baba zako kina Nyerere huu mpira mkubwa huuwezi, kuanzia siku hiyo Kikwete akawa na heshima kwa Mugabe, na huwezi kumsikia anamletea kibesi. Ndiyo maana Mugabe anamhusudisha.

Ukiweka maanani historia ya ukombozi wa Zimbabwe, kuanzia Mugabe alivyokuwa anakaa Four Flats pale Upanga na kuendesha ki VW Beetle chake mpaka anakuwa freedom fighter, Lancaster House Talks, mpaka Mugabe kuchukua nchi na hata baadaye Mkapa alivyomkingia kifua kwenye CHOGM Australia basi Mugabe hawezi kukosa shukurani kwa wabongo.

Mugabe mwenyewe chaguzi zake kuiba kura alikuwa anajifunza kwa CCM, CCM katika uchaguzi wa pili kutoka mwisho ilimpeleka Kingunge Ngombale Mwiru na January Makamba waende kuwa "waangalizi" officially lakini unoficially Mzee Kingunge alienda na victory blueprint.

Kwa hiyo siwezi kushangaa Mugabe akitinga Ikulu kumpongeza Kikwete.
 
Kuhudhuria kwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe wakati wa kuapishwa kwa rais Kikwete kunaelezwa na wanazuoni huenda ikawa sababu ya nchi nyingi hasa za magharibi kusita kumpongeza rais Kikwete aliyeapishwa leo.

Nchi hizo za magharibi zenye ushawishi mkubwa duniani zikiwemo Marekani na Uingereza, pamoja na kuwakilishwa na mabalozi wake inasemekana hadi sasa hazijatuma salamu za pongezi za kuchaguliwa kwa Kikwete kitu ambacho si kawaida yake.

Ikumbukwe kuwa wakati wa uchaguzi uliopita wa Zimbabwe ambao ulilalamikiwa sana na UK na USA kuwa haukuwa huru na wa haki umepelekea hadi leo Mugabe na familia yake kunyimwa hati ya kuingia katika nchi hizo isipokuwa kuhudhuria mikutano ya UN pekee.

Wachambuzi wa mambo wanahisi tukio la leo kwa Mugabe kuhudhuria linaweza kuwa limetia doa mahusiano ya Tanzania na nchi hizo ikizingatiwa kuwa kuna madai yanayotolewa na chama cha upinzani Tanzania kuwa kulikuwa na udanganyifu wa kura wakati wa kuhesabu.


Wanaweza kumzuia Kikwete kwenda USA na UK. Sasa Chai za Obama itakuwaje?
 
WATCH OUT.
For me Mugabe is HERO.
Believe on me my people we will never develop economically until we build capacity to deal with those western countries.
We dont need foreign AID anymore.
Hakuna nchi tajiri itakayoweka ubalozi nchini kwako kama hakuna ubadilishanaji wa resources.
Nendeni mkafanye tafiti kwenye migodi yetu ambayo mnalalamikia kila siku ndo mtajua mmarekani anazo kampuni ngapi kule ambazo zimesajiliwa kama za wa cananda na bado uranium mliogundua mtaampa achimbe yeye na nyinyi mtaambiwa msijenge power plant coz hamna uwezo wa kuzuia maadhara ya vinu vya nuklia ila tuuzieni sisi nasi tutawasaidia mitambo ya umeme ya kutumia diesel.
CHINA IS DEFINED BY BAD GOVERNMENT ALL OVER THE WORLD BY WESTERN COUNTRIES kwa sababu haikubaliani na unyonyaji unaofanywa na western countries...na kwa sasa inafanya vizuri kuliko hata nchi zilizoendelea kiuchumi.
 
hivi mlitaka kikwete asimualike Mugabe kwa sababu ya kumuogopa mzungu? na asingeli mualika ningezidi kuamini kuwa Kikwete hafai kuongoza watanzania ndani ya bara la afrika kwa kuwa matendo yake yote ni kwa ajili ya kum please mzungu tu.
 
hivi mlitaka kikwete asimualike Mugabe kwa sababu ya kumuogopa mzungu? na asingeli mualika ningezidi kuamini kuwa Kikwete hafai kuongoza watanzania ndani ya bara la afrika kwa kuwa matendo yake yote ni kwa ajili ya kum please mzungu tu.

Usiombe uwe na ndugu kama Luteni anakaa mjini, halafu wewe ndiye unatoka shamba mambo ya mjini huyajui, nguo za mjini huna etc. Inaonekana kwa kufuatilia logic ya "Mugabe kumponza Kikwete" Luteni anakuchunia ndugu yake kama hakujui, ili mradi usije kumletea gozigozi za shamba wakati anatanua na washkaji zake wa mjini.

I kid Luteni, my point is, sovereignty is paramount. Kama tunamualika au hatumualiki Mugabe, iwe kwa sababu za mahusiano ya Mugabe / Zimbabwe na Tanzania, sio kwa kuwaangalia Wamarekani.

Whats next, tutataka State Department ituandikie foreign policy, nani wa kucheza naye, nani wa kufanya naye biashara, na nani wa kumuita terrorist ?

I mean mimi simpendi Mugabe, lakini this is too much. Ningeelewa mtanzania kuwa concerned Kiwete kumualika muuaji Mugabe, lakini kuwa concerned kwa sababu atatuharibia kwa Wamarekani ni utumwa wa kileo tu.
 
nchi hii ipigwe BAN tule mapka vyura ndo tutatia akili...mijitu mijizi ya kura vibaya sanaaa

Hatuwezi kula vyura ndugu yangu. Badala yake itatusaidia kukumbuka tunu za awali kabisa za utawala wa TANU na Mwl. Nyerere kuwa "nchi hii itajengwa na watanzania wenyewe, kila mtanzania, kila mzalendo na hasa kila mjamaa" Huu ndio ulikuwa mwanzo wa dhana ya kujitegemea ambayo viongozi wetu wameiweka kapuni na kuhubiri kuombaomba aka kuhemea.

Zamani hawa wanaoitwa wafadhili walikuwa na majina stahiki kama wakoloni mamboleo, mabeberu, wanyonyaji, makupe nk. Sijawahi kusikia katika siku za hivi karibuni kiongozi yeyote wa CCM akitumia majina hayo japo ukweli unabaki palepale kuwa huu tunaouita utandawazi ni uleule uliokuwa ukiitwa ukoloni mamboleo (neo colonialism) enzi hizo na Mwl Nyerere na viongozi wengine wenye akili wa Africa enzi hizo.
 
I like Mugabe's statement: The only white man you may Trust is a dead white Man.

Jamaa Mugabe anawachukia wazungu kupita maelezo na hana imani nao kabisa na its sad kuona hapati support ya kutosha from other African leaders may be Gadaffi, jamani tutaendekeza kunyenyekea westerners hadi lini?? wanakuja kwa gia ya kuwekeza wakiondoka kama mkataba ulikuwa wa uvuvi wanakuwa wamevua kila kitu hadi mayai ziwa linabaki tupu na hamna tulichofaidika na huo uvuvi, to me Mugabe is a HERO hata kama anatumia mabavu, ana machungu na Africa tofauti na maraisi wengine waonao nyenyekea wazungu na kuwa omba omba hadi karne hii.:doh:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom