Mufti wa Tanzania: Bakwata haitavumilia kuvunjiwa heshima wala kunyanyaswa

Bakwata ni taasisi iliyosajiliwa kwa mujibu wa sheria za nchini tanzania inakatiba yake na miongozo yake juu ya uendeshaji dini ya uislam.nchi yetu inaruhusu uhuru wa kuabudu kwa kila raia wake ilimladi hauvunji sheria za nchi.

BAKWATA siyo UISLAM bakwata ni taasisi kama zilivyo taasisi nyingine za ALHIKMA,ANSARI SUNNA.SALAFY.ISLAMIC F.hizi taasisi zote zina waislam wanaowaongoza kwa taratibu wanazozifaham wao kwa elimu waliyokuwa nayo.Bakwata wanapoendesha shughur zao waendeshe wanavyotaka wao tumewaacha na misikiti yao na madrasa zao

inaumiza sana kuona chombo kilichokuwa cha mwanzo hapa tanzania kusajiliwa leo hakina maendeleo yoyote zaidi ya kutumika kuudumaza uislam kilal kukicha.hatufurahi kuona waislam tumeshindwa kuwa na hospitar zetu zinazoendeshwa kwa taratibu za dini.tumeshindwa kuwalipa mishahara walimu wa madrasa zetu.tumekalia kuangalia suruali fupi na ndefu,mfuga ndevu na asiyefuga ndevu,kaswali leo iddi ataswali kesho idi.Bakwata fanyeni yenu nasisi tunafanya yetu hatupaswi kukaa majukwaani na kulishiana vitisho
uko sahihi sheikh BAKWATA ni dumavu tangu ilipoasisiwa miaka ya uhuru, ila unapoilaumu na kuishangaa inabidi ujuwe yafuatayo:
i)ndio msimamizi mkuu wa masuala ya Uislam nchini haijalishi dhehebu gani
ii)kusema ni sawa na taasisi zingine itakuwa umekosea na kuidhalilisha kwa kiwango hali ya juu, kumbuka serikali haisajili taasisi yoyote ya Kiislam bila katiba yake kupitiwa na BAKWATA.
III)iltaka kujenga taasisi za elimu na afya lakini ilizuiwa na serikali ya rais yule ambaye alitaka kila kitu cha umma na sio binafsi
iv)kuilaumu leo kwa makosa ya nyuma itakuwa huisaidii bali ni kuikandamiza tu kama una ushauri peleka.
 
Mtumeee..! Muft anaongea kama Magufuli au wakuu wa mikoa.
Unaweza sema kiongozi wa BAKWATA kaandikiwa hotuba na BASHITE.
Sasa ni mwendo wa kupotea ukikosoa BAKWATA.

Nchi imejamba hii tena shuzi mtengua udhu kabisa.
Muda wote wapi na BASHITE unafikiri fikra zake zitakuaje?
 
Naomba ufafanuzi zaidi na wala siyo namvunjia adabu Mufti....
Je itakuwa sawa kwa Ansar Sunna kufunga au kuswali kwa kufuata mwezi wa kimataifa
Vipi kuhusu hawa Ibadhi hawafungi mikono wakati wa swala
Shia wanachanganya swala nao pia itakuwaje
Mbona hatuna hata Sheikh mmoja wa Mkoa Mshia au Bohora
Mbona watendaji woote wa Bakwata ni wa dhehebu moja tu...
Tushikane na kamba ya ALLAH na wala tusifarakane na tuendelee kumcha ALLAH kwa kumtwii na pia kumtwii Mtume wake (SAW) na walioko kwenye Mamlaka
EAMWS ndiyo iliunganisha madhehebu yote ya Kiislam ikafungiwa na aliyeiasisi Bakwata. "Divide and rule".

Hayo mengine ya kufunga na kufungua mikono ni poa tu, hayaathiri swalat.

La Mashia kuunganisha swala pia ni poa tu, haliathiri swalat. Mradi wakati umezingatiwa.

Hilo la kufuata "mwezi wa kimataifa" naomba rekebisha. Wao hawafati mwezi wa Kimataifa wanafata inapotangazwa Saudi Arabia. Hili halipo poa.

Binafsi nafata nchi niliopo. Mufti wa nchi husika anavyoamua ndivyo hivyo hivyo.
 
uko sahihi sheikh BAKWATA ni dumavu tangu ilipoasisiwa miaka ya uhuru, ila unapoilaumu na kuishangaa inabidi ujuwe yafuatayo:
i)ndio msimamizi mkuu wa masuala ya Uislam nchini haijalishi dhehebu gani
ii)kusema ni sawa na taasisi zingine itakuwa umekosea na kuidhalilisha kwa kiwango hali ya juu, kumbuka serikali haisajili taasisi yoyote ya Kiislam bila katiba yake kupitiwa na BAKWATA.
III)iltaka kujenga taasisi za elimu na afya lakini ilizuiwa na serikali ya rais yule ambaye alitaka kila kitu cha umma na sio binafsi
iv)kuilaumu leo kwa makosa ya nyuma itakuwa huisaidii bali ni kuikandamiza tu kama una ushauri peleka.
Wangekuwa wanapokea ushauli ungesaidia kujenga na kuendeleza uislam.serikali haitaki viongozi wa BAKWATA wenye elimu nzuri ya dini na kisekula.wao wanapenda tuongozwe na viongozi ambao wakikaa nao kwenye vikao watakachosema serikali basi kiwe hichohicho.

tembea vizuri katika viongozi wa bakwata wa wilaya na mikoa ndio utalifaham hilo.kuhusu kubaniwa kujenga mashule na mambo mengine,tumeona taasisi ya islamic ya morogoro wanashule na redio kuna MARKAZI nyingi zinashule. haya mambo yalitakiwa yawe makubwa kwa Bakwata kwasababu ndio waliopewa mali nyingi za waislam kabla ya uhuru na baada ya uhuru.
 
Bakwata viongozi wake wanachaguliwa na serikali,,uliona wapi wakritu wanachaguliwa viongozi na serikali,Waislamu wenye uelewa ndio maana wanaipinga bakwata
 
wapi kasema ataroga acha uzushi
Kijana inainekana hujui maneno ya kiutu uzima
Ina maana Mufti angesema "Nitawachukulia hatua kali wale wote wanaonifuatafuata"... wewe huenda ukauliza hivi atawakanyagakanyaga?!
 
kumbe Bakwata imeanzishwa na serikali, nazidi kushangaa tu mimi.
Mjanja...
Historia ya BAKWATA tunaweza kusema ni ''one epic story'' ambayo
Hollywood wanaweza kutengeneza movie ya kushinda Academy
Award.

Historia yake inawahusu wapigania uhuru na wanachama wakubwa
wa TANU kama Tewa Said Tewa na Bi. Titi Mohamed na viongozi wa
serikali wa juu kabisa kama Rashid Kawawa na Abeid Amani Karume.

Historia yake inawagusa wana habari maarufu wa wakati wao kama
Benjamin William Mkapa aliyekuwa Mhariri wa The Nationalist,
Brendon Grimshaw
Mhariri wa Tanganyika Standard na Martin Kiama
Mkurugenzi wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD).

1565721329807.png

Sheikh Hassan bin Ameir akipeana mikono na Rais Julius Nyerere katika sherehe za kuweka jiwe la msingi
wa Chuo Kikuu cha Waislam katikati ni Tewa Said Tewa

Historia yake inagusa maofisa wa vyombo vya usalama wa nyakati zile
kama Rashid Kayugwa kutka Usalama wa Taifa, IGP Hamza Aziz na
Geoffrey Sawaya, Director of Criminal Investigation (DCI).


1565713043746.png

Sheikh Hassan bin Ameir
1880 - 1979

Historia yake inamgusa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir
ambae licha ya kuwa alikuwa ''alim,'' mkubwa lakini alikuwa mwanasiasa
aliyesaidia sana kuingiza wafuasi wake wa Tariqa Kadiriyya na Makhalifa
wao katika harakati za kukabiliana na ukoloni wa Waingereza.

Huyu ndiye Mzanzibari pekee aliyepigana bega kwa bega na Baba wa
Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
katika kuikomboa Tanganyika.

Najua nazidi kukuchanganya kwa sababu historia hii ni ngeni sana kwako.
 
swali lako la kwanza kama mwezi umeoneka sehemu yoyote wanaruhusiwa kufunga au kufungua sio bakwata wanavyotaka wao kufungua mpaka rais au waziri awe na nafasi ya kuhudhuria sherehe ya eid ndio wapange. swali la pili kufunga mkono na kufungua hakuna tatizo lolote hata ansar sunna anaweza kufungua mikono na sala ikawa ipo pale pale.swali la tatu shia wanachanganya swala, ndugu yangu shia hawapo katika uislamu wao na makatoliki wapo sawa . mfano huwezi wewe umtukane mke wa rais makufuli halafu rais makufuli akupende sio rahisi. mashia wanamtukana mke wa mtume bibi aisha halafu vipi wawe kipenzi wa mtume wanawatukana maswahaba marafiki wa mtume vipi wawe waislamu unaweza ukatamka ashhadu leo kesho bila wewe kujua ukawa kafiri kwa maneno yako na matendo yako. pia hatuwezi kuongozwa na mshia au bohora maana hao wawili wanafanana tabia zao
Shukran kwa majibu yako,je hivyo ndivyo BAKWATA inavyo amini,kama nilivyo muelewa MUFTI itakuwa kosa yoyote yule awe Shia,Answar nk..nk...kutangaza mwezi isipokuwa yeye tu.
 
Ukweli ni kwamba viongozi wengi wa dini ni wachawi iwe uislam au kikristo tena ni wachawi wa viwango vya juu sana.
Sema Neno Na Roho Zipate Kupona
Itapendeza Ukitiririka Hapa Ama Kufungua Thread Kwaajili Ya Kiongozi Huyo
 
Wakati fulani nilikatiza soko la Tandika, nikakuta ndugu zangu kadhaa wa kiislamu wakibishana kuhusu BAKWATA na uuislamu. Moja wao alisema BAKWATA haiwawakilishi waislamu bali ni chombo cha dola ndani ya uislamu. Nkabaki mdomo wazi huku nikiendelea na safari yangu.
 
Kila mtu ana tafsiri yake kama alivyosema, ila kuitaka serikali imuelewe, tafsiri yangu ni kwamba serikali ishiriki katika kuwadhibiti watakaoshindwa kuiheshimu BAKWATA
Swadakta!!! Huyu anakwazwa Sana na wale wanaokula Eid siku tofauti na ile inayotangazwa na BAKWATA
 
Mufti inabidi apewe tafsiri halisi ya UISLAMU na BAKWATA ili ajue kutofautisha.. Kuikataa BAKWATA sio kuukataa UISLAMU.. Kama yeye ameamua kutetea BAKWATA na kukosa uvumilivu na watu wengine basi ajue wengine wataendelea kupigania UISLAMU dhidi ya mabaya yote ambayo waislamu wanafanyiwa hasa kunyimwa haki zao za msingi.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom