MUFTI, MASHEHE WATIMULIWA IKULU (wapekuliwa kisha wafukuzwa, yumo shehe Yahya.

Domo Kaya

JF-Expert Member
May 29, 2007
531
59
Story na Uwazi,

Mwandishi Elvan Stambuli.

' Mufti wa Tanzania shehe Shaabani Simba alialikwa katika kalamu ya Sikukuu ya Idd ya Rais Jakaya Kikwete Ikulu na kumtuma msaidizi wake Naibu Mufti wa Tanzania Shehe Abubakar Zuberi akiwa na mashehe wengine walijikuta wakitimuliwa Jumamosi iliyopita.

Habari zilizofikia gazeti hili siku ya tukio zinasema wakati wa kwenda Ikulu jijini Dar Es Salaam, Naibu Mufti Shehe Zuberi alifuatana na viongo wa ngazi ya juu wa baraza kuu la waislam Tanzania (BAKWATA) akiwemo katibu wa baraza la Ulamaa na kamishna wa Tume ya kudhibiti Ukwimwi (TACAIDS) sheikh Hassan Chizenga na Mjumbe wa Baraza la Ulamaa, shehe abdallah Nyasi.

Naibu mufti alimuruhusu Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Ali Nguruko kuzungza na Uwazi ambapo alisema wamefedheheshwa sana na waliyofanyiwa Ikilu.

Alifafanua zaid sheikh Nguruko alisema Kikwete aliswali swala ya Iddi katika msikiti wa Al Farouk, makao makuu ya Bakwata na kuwaagiza waende Ikulu ktk karamu aliyoiandaa bila kukosa.

Tuliondoka baada ya kuagana na Rais mstaafu Ali Hassani Mwinyi ambaye pia aliwasili hapa tulipofika getini Ikulu tulipekuliwa kwa kufunuliwa kanzu zetu, hata Naibu Mufti alifunuliwa tilisikitika sana tulijiuliza hawa hawajui kuwa Mashikh hawa ndio waliomswalisha Rais leo.

Aliongeza kuwa kilichowasikitisha zaidi ni kuona raia wa kigeni wakipita na kuingia Ikulu bila ya kupekuliwa kama tulivyofanywa sisi. Kibaya zaidi alisema ni jopo zima la Bakwata kutoruhusiwa kuingia Ikulu kama alivyoagiza Rais Kikwete.'
 
Sasa walitaka wasipekuliwe..Kungelipuka kibomu hata kama sio chao si wangeambiwa ni wao wamepekuliwa kwa usalama wao wenyewe...wao wanalaumu nini sasa//.?
 
Sasa walitaka wasipekuliwe..Kungelipuka kibomu hata kama sio chao si wangeambiwa ni wao wamepekuliwa kwa usalama wao wenyewe...wao wanalaumu nini sasa//.?

Wanacholaumu ni wao kutoruhusiwa kuingia ndani kwenda kupata mnuso
 
Tatizo Watanzania tunapenda kukaribisha wakati hatujamaanisha kweli. Pengine Kikwete naye alitamka kwa kawaida ya Kitanzania "Karibuni jamani!!!" wenzanke wakachukulia serious. Mimi nadhani mwaliko wa tafrija maalum kama hiyo ya Ikulu kulipaswa kuwa na kadi au barua maalum. Sasa je, ilitolewa? na wao walikuwa nayo?
 
Si Mnajua tena mnuso tena wa Ikulu mahanjumati yanakuwa mengi hivyo hata kama Mh. Rais alisema kiutani watu wakamaind ulaji.
 
wamezowea mialiko ya ikulu kila eid!

safari hii JK anamengi kichwani, kawasahau kuwapa mualiko rasmi, inaonyesha akawapa mualiko wa mdomo alipokutana nao msikitini!

watendaji wa ikulu hawajui protocol zinavyoenda, walikuwa wapeleke kadi za mualiko kabla rais hajababaika akatoa mualiko kwa mdomo.
 
Hii si haki kabisa, siku hizi ukipendelea kuvaa kanzu na balagashia, mbele ya walinzi wa usalama unakuwa unatiliwa shaka,na upekuzi unakuwa ni wa kina
 
Hii habari ni ya 2007 vp jamani Masheikh
waliombwa radhi na KURUGENZI YA MAWASILIANO IKULU ?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom