Mufti Abubakari Zuberi ahimiza uharaka kesi ya mashehe wa Uamsho

🤣🤣🤣 Niliona dalili! Serikali na BAKWATA wanavyotuchezea akili, yaani serikali inaitaka BAKWATA itoe tamko ikiwa tayari imekwishaamua kuwaachia!
Hahahaahaa hata mimi nilishtuka. Ndo Utajua ni kias gani BAKWATA wako "well connected"
 
Yaani Bakwata inatoa tamko tu watu wanaachiwa,

Naiona hatari ya mambo kama haya kama taasisi za kidini zinakua na nguvu namna hii katika mihimili yetu ya dola.

Tunatengeneza mfumo ambao kila dini itakua inapambana kuweka viongozi wa juu wa nchi ili kunufaika na mfumo.
 
Dalili hizi zimeanza kuonekana baada ya Shehe Mkuu wa BAKWATA Mufti Zuberi kuzitaka mamlaka kuharakishwa kusikilizwa kwa shauri lao. Ni dhahiri shahiri serikali haiwezi kupuuza ombi lake na hivyo DPP ama atashauriwa kulifuta shauri hilo au ataanzisha mchakato wa kusikilizwa shauri hilo haraka.

========

Alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mkutano wa viongozi wa dini waliokutana kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali yanayoendelea nchini.

Alisema ni miaka mingi sasa tangu kesi hiyo ianze kusikiliwa na kuomba wenye mamlaka ya kusimamia kesi kufanya haraka kusikiliza ili ifikie muafaka.

“Hatuwezi kuingilia mambo ya kisheria, lakini ninachoweza kuomba ni uharakishwaji wa kusikiliza kesi yao, kesi hii imekaa miaka mingi, suala hili niombe mamlaka husika ziharakishe kuisikiliza kwa sababu imekaa miaka mingi,” alisema Mufti na kuongeza:
“Usikilizwaji wa kesi kwa haraka na hukumu ikatolewa itajulikana nani ana hatia gani na achukuliwe hatua gani na nani hana, kuliko kukaa ndani muda mrefu bila kufahamu hatma yao.”

Miongoni mwa mambo mengine ambayo viongozi hao wa dini walizungumzia ni kuhusu vitendo vya ukatili vinavyoendelea kwa watoto na kuwataka wazazi kuwajibika katika malezi ya watoto wao.

“Hawa watoto ndiyo viongozi wa nchi tunaowategemea kesho, kwa hiyo tusipowajibika katika kuwatunza na kuwalinda tunakuwa tunaharibu taifa letu, ni vema kila mzazi, mlezi na jamii yote iwajibike katika kumlinda mtoto,”alisema Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)Jimbo la Mashariki na Pwani, Dk. Alex Malasusa.

Alisema: “Asilimia kubwa ya watoto huharibika tabia kutokana na kukosa uangalizi wa wazazi ambao wanabanwa na shughuli za kila siku, hivyo wanapaswa watenge muda wa malezi. Tuombe kwamba kila unapobarikiwa kupata mtoto, uwajibike pia na katika kumlea na kumlinda.”

Machi 28, mwaka huu Rais Samia Suluhu Hassan wakati akipokea taarifa ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ya mwaka 2019/2020, aliiagiza kuharakishwa kwa kesi, kuziondoa zisizo na msingi ili kuondokana na idadi kubwa ya kesi ambazo serikali imekuwa ikishindwa.

Vilevile, Juni 13, mwaka huu, viongozi wa dini Zanzibar, walimwomba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi, kuangalia suala la viongozi hao wa uamsho ambao wako mahabusu kwa muda mrefu.

Miongoni mwa mambo waliyomwomba ni kuangalia kama wana hatia au la, badala ya kuendelea kusota rumande bila kujua hatima yao.

Chanzo: Nipashe

Unafiki tu anataka kuchukua credit sasa, huyu alikuwa wapi miaka yote mbona hatukumsikia akiongea na Mwendazake, wakati siku zote walikuwa wanakutana kwenye mialiko mbali mbali.

Hongera Mama Samia.
 
Baada ya kugundua kuwa DPP amesha sain hati ya kuwafutia mashtaka watuhumiwa kilichobaki ni utekelezaji (kuachiwa) ndio unaamua kujitokeza kuomba swala la masheikh lifatiliwe! Kipindi chote ulikuwa wapi kusema? ulimuogopa nani na ulichoogopa hasa ni nini? na kama uliamua tu kukaakimya kwanini uliamua hivyo? Na kinachokufanya useme sasahivi ni nini? Kwani ungeendelea kukaakimya nini kingetokea?

Wakati wafuasi wako team Bakwata wakimshambulia sheikh Ponda Kwa issue hii ya kuachiwa Kwa hawa masheikh mbona hukujitokeza kutoa neno juu ya msimamo wako? Walichokuwa wakikisema wafuasi wako dhidi ya sheikh Ponda yalikuwa ni maelekezo kutoka kwako?

Katiba ya Bakwata inapaswa kufanyiwa marekebisho huu utaratibu wa Muft kutawala mapaka kifo uondolewe.

Uongozi ni uwajibikaji, hatuwezi kuwa na kiongozi ambae kazi yake ni kutangaza mwezi na kuomba dua kwenye majanga na sherehe za kitaifa, huku maadili kwenye jamii yanaporomoka, watu wanadhulumiwa haki zao, hakuna hospital, hakuna shule (madrasa) Migogoro ya miskiti mingi chanzo ni Bakwata, hata wanapopatikana wafadhili kujenga chule, hospital au mskiti mnawaletea zengwe wanaondoka, wale wanaoamua kufanya ufadhili mwisho wa siku mnageuza huo ufadhili kuwa vitega uchumi vyenu.

Nyumba za waqfu mmezigeuza vitega uchumi, watu mpaka wamekuwa wazito kutoa zaka maana wapokeaje (wasimamizi) ni nyinyi ili muwafikishie walegwa (jamii) Kwa utaratibu maalumu, matokeo yake nyinyi ndio mmekuwa wadau No1 kanakwamba hakuna wakundi mengine.

Badirikeni acheni mazoea.
 
Alikuwa wapi kipindi cha nyuma badala ya kusubiria movie iishe ndipo atoe sauti
 
Baada ya kugundua kuwa DPP amesha sain hati ya kuwafutia mashtaka watuhumiwa kilichobaki ni utekelezaji (kuachiwa) ndio unaamua kujitokeza kuomba swala la masheikh lifatiliwe! Kipindi chote ulikuwa wapi kusema? ulimuogopa nani na ulichoogopa hasa ni nini? na kama uliamua tu kukaakimya kwanini uliamua hivyo? Na kinachokufanya useme sasahivi ni nini? Kwani ungeendelea kukaakimya nini kingetokea?

Wakati wafuasi wako team Bakwata wakimshambulia sheikh Ponda Kwa issue hii ya kuachiwa Kwa hawa masheikh mbona hukujitokeza kutoa neno juu ya msimamo wako? Walichokuwa wakikisema wafuasi wako dhidi ya sheikh Ponda yalikuwa ni maelekezo kutoka kwako?

Katiba ya Bakwata inapaswa kufanyiwa marekebisho huu utaratibu wa Muft kutawala mapaka kifo uondolewe.

Uongozi ni uwajibikaji, hatuwezi kuwa na kiongozi ambae kazi yake ni kutangaza mwezi na kuomba dua kwenye majanga na sherehe za kitaifa, huku maadili kwenye jamii yanaporomoka, watu wanadhulumiwa haki zao, hakuna hospital, hakuna shule (madrasa) Migogoro ya miskiti mingi chanzo ni Bakwata, hata wanapopatikana wafadhili kujenga chule, hospital au mskiti mnawaletea zengwe wanaondoka, wale wanaoamua kufanya ufadhili mwisho wa siku mnageuza huo ufadhili kuwa vitega uchumi vyenu.

Nyumba za waqfu mmezigeuza vitega uchumi, watu mpaka wamekuwa wazito kutoa zaka maana wapokeaje (wasimamizi) ni nyinyi ili muwafikishie walegwa (jamii) Kwa utaratibu maalumu, matokeo yake nyinyi ndio mmekuwa wadau No1 kanakwamba hakuna wakundi mengine.

Badirikeni acheni mazoea.
msumari wa mwisho kabisaa katika jeneza.
 
..Nadhani Mufti " alitonywa " kuwa serikali inatarajia kuwaachia huru Mashekhe wa Uamsho, ndipo na yeye akajitokeza kuigiza kuwatetea.
 
Back
Top Bottom