Muelekeo wa kozi ya Aircraft Eng Tanzania

texaz mc

JF-Expert Member
Jan 15, 2016
371
203
Habari wadau wote wa elimu.

Swala langu ni kuhusu hii kozi ya AIRCRAFT ENGINEERING inaonekana itakua na soko kubwa mpk kufikia 2025-2030. Huu mtazamo wangu ni kutokana na haya yafuatayo;

1. Leo kwenye hotuba ya Rais ameainisha kwamba kwenye hii kozi mwaka huu imetoa wahitimu 16 tu. Hivyo inaonekana watu hawajaijua au hawajajikita kuisomea wakiamini kwa Tanzania itakua ngumu kupata kazi zake.

2. Mimi naamini hao wahitimu 16 woote watapata ajira kwenye sekta hiyo kutokana na kutokuwepo kwa upinzani kwenye kozi hii.

3. Kuwepo na chuo kimoja tu kinachotoa kozi hii ambacho ni NIT hivyo kupelekea kudahili wanafunzi wachache tofauti na kozi zingine kama comp eng ambayo inapatikana vyu vingi kama MUST, DIT n.k.

4. Ugumu wa kozi hii ambapo watu wengi hudhani kuwa ni mojawapo ya kozi ngumu sana.

5. Kununuliwa kwa ndege nyingi kwa miaka ijayo.

6. Pia mh. Rais amesema, kutokana na ndege hizo kuhitaji maintanance kila baada ya miezi kadhaa hivyo serikali itahitaji kutumia kiasi kikubwa cha fedha takribni dola million 3 kuzipeleka nje ya nchi kutokana na UPUNGUFU WA WATAALAMU KATIKA FANI HII.

Hivyo hapa ameahidi kukiboresha chuo cha NIT kimiundombinu na kuwapatia ndege ndogo kwa ajili ya mafunzo ya vitendo(KWA SABABU WATAANZISHA KOZI YA URUBANI MIAKA IJAYO)

Mimi nimeona hivyo kwa mtazamo wangu, karibuni wadau wote wa elimu tulijadili hili.
 
By the way ukisomea uwalimu utakufa maskini, tuna, mshahara laki tano, ndio kazi gani hiyo


Unachokisema kinaweza kuwa cha kweli lakini nimesomeshwa mie na wadogo zangu kwa mshahara wa mwalimu wa shule ya msingi, tena wale wa UPE.

Mzee wa watu akaranya mitihani yake ya form four, cheti kilitumwa lakini alikua ameshatangulia mbele za haki.

Kuna wenzako wanaitamani hiyo laki tano kwa mwezi hawaipati. Jaribu kuwa makini kuchagua maneno ya kutumia mkuu.

Nafanya kazi na watu wamesoma na wanapokea pesa nene lakini hawajawahi kuwa na kauli za kukatisha tamaa kama hizi unazozileta kuhusu waalimu.

Bila hao waalimu wanaopikea 500k ungesoma?

Mwisho wa siku, unatumiaje unachokipata na sio unapata kiasi gani ndio kinakufanya ufanikiwe.
 
Habari wadau wote wa elimu.
Swala langu ni kuhusu hii kozi ya AIRCRAFT ENGINEERING inaonekana itakua na soko kubwa mpk kufikia 2025-2030. Huu mtazamo wangu ni kutokana na haya yafuatayo;-
1. Leo kwenye hotuba ya Rais ameainisha kwamba kwenye hii kozi mwaka huu imetoa wahitimu 16 tu. Hivyo inaonekana watu hawajaijua au hawajajikita kuisomea wakiamini kwa TZ itakua ngumu kupata kazi zake.
2. Mimi naamini hao wahitimu 16 woote watapata ajira kwenye sekta hiyo kutokana na kutokuwepo kwa upinzani kwenye kozi hii.
3. Kuwepo na chuo kimoja tu kinachotoa kozi hii ambacho ni NIT hivyo kupelekea kudahili wanafunzi wachache tofauti na kozi zingine kama comp eng ambayo inapatikana vyu vingi kama MUST, DIT n.k
4. Ugumu wa kozi hii ambapo watu wengi hudhani kuwa ni mojawapo ya kozi ngumu sana.
5. Kununuliwa kwa ndege nyingi kwa miaka ijayo.
6. Pia mh. Rais amesema, kutokana na ndege hizo kuhitaji maintanance kila baada ya miezi kadhaa hivyo serikali itahitaji kutumia kiasi kikubwa cha fedha takribni dola million 3 kuzipeleka nje ya nchi kutokana na UPUNGUFU WA WATAALAMU KATIKA FANI HII.

Hivyo hapa ameahidi kukiboresha chuo cha NIT kimiundombinu na kuwapatia ndege ndogo kwa ajili ya mafunzo ya vitendo(KWA SABABU WATAANZISHA KOZI YA URUBANI MIAKA IJAYO)

Mimi nimeona hivyo kwa mtazamo wangu, karibuni wadau wote wa elimu tulijadili hili.
Ww kasome tu au mwanao aende ila kwa mm dalili nazo ona ndege zinaenda na Magu
 
Petroleum eng udsm, petroleum geoscince MRI ,oil and gas dit wote Hawa wapo mtaani tu
Hawawezi kosa dili mkuu trust me, lakini simshauli mtu asomee ualim kama ndio carrier ya kufa nayo, mimi mwl wangu wa primary saiz ni mhandis wa majengo ana mahela, ualimu hauna hata marupurupu, utaishia kukalia madawati ya watoto,
 
USHAURI WA BURE.

usisome kozi kwa mkumbo hasa wa kisiasa. Utalia na kusaga meno ukimaliza.

Waulize petroleum walipo... Usiamini maneno ya wanasiasa hasa hawa wa ccm!

Kama unasoma soma ila sio usome kisa mwanasiasa kasema ina demand.
 
Back
Top Bottom