Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,991
- 144,327
Hivi huu utaratibu wa miaka 4 ambao bila shaka ulianza awamu ya Magufuli (mwanzoni ilikuwa miaka 3), ni mtumishi kutakiwa kuwa amefanya kazi kwa miaka 4 mfululizo tangu apande cheo kwa mara ya mwisho au awe amefanya kazi kwa angalau muda wa miaka 4 bila kujali ni kwa miaka 4 mfululizo au sio mfululizo?
Msingi wa swali langu ni kutokana na ukweli kuwa kuna watumishi tangu wapenda cheo mara ya mwisho, inaweza kuwa ni miaka 5 6 au hata 7 iliyopita lakini ndani ya miaka hiyo 6 au 7, kuna kipindi mtumishi huyo alikuwa masomoni kwa mwaka mmoja, miwili au hata mitatu. Sasa nachojiuliza mtumishi huyo anastahili kupanda cheo?
Kwa mfano, mara ya mwisho kupanda cheo ilikuwa May mwaka 2015 na ilipofika Oktoba 2016, akaenda masomoni (full time) kwa miaka 2 kwa maana ya mpaka mwaka July 2018 alipomaliza masomo na kurejea kazini
Sasa mtumishi kama huyu ambae hana miaka 4 mfululizo kufikia mwaka huu wa 2021 lakini tayari ametumika cheo hicho kwa jumla ya miaka 4(including kipindi cha June 2015 mpaka Oktoba 2016 kabla hajaenda masomoni), anastahili kupandishwa cheo?
Ukisoma standing order ya 2009 kipegele cha mambo ya promotion, naona haiko wazi kuhusu hili, hivyo kwa wanaojua, hasa Maafisa Utumishi (kama wamo humu), tunawaomba watupe ufafanuzi.
Karibuni.
Msingi wa swali langu ni kutokana na ukweli kuwa kuna watumishi tangu wapenda cheo mara ya mwisho, inaweza kuwa ni miaka 5 6 au hata 7 iliyopita lakini ndani ya miaka hiyo 6 au 7, kuna kipindi mtumishi huyo alikuwa masomoni kwa mwaka mmoja, miwili au hata mitatu. Sasa nachojiuliza mtumishi huyo anastahili kupanda cheo?
Kwa mfano, mara ya mwisho kupanda cheo ilikuwa May mwaka 2015 na ilipofika Oktoba 2016, akaenda masomoni (full time) kwa miaka 2 kwa maana ya mpaka mwaka July 2018 alipomaliza masomo na kurejea kazini
Sasa mtumishi kama huyu ambae hana miaka 4 mfululizo kufikia mwaka huu wa 2021 lakini tayari ametumika cheo hicho kwa jumla ya miaka 4(including kipindi cha June 2015 mpaka Oktoba 2016 kabla hajaenda masomoni), anastahili kupandishwa cheo?
Ukisoma standing order ya 2009 kipegele cha mambo ya promotion, naona haiko wazi kuhusu hili, hivyo kwa wanaojua, hasa Maafisa Utumishi (kama wamo humu), tunawaomba watupe ufafanuzi.
Karibuni.