Muda wa Kurudisha Fomu za Kuomba Uongozi wa Kitaifa na Mabaraza waongezwa

kibaja

Member
Jun 5, 2012
98
123
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kimeongeza muda wa kuomba nafasi ya kugombea Uongozi wa Kitaifa hadi tar 30/08/2014 saa kumi alasiri.

Taarifa za awali za Chama ni kuwa mwisho wa kurudisha fomu ilikuwa tarehe 25/08/2014.

Muda huo umeongezwa kutokana na maombi mengi ya wanachama mikoani ambapo chaguzi bado zinaendelea.

Mkurugenzi wa Organizesheni, Mafunzo na Usimamizi wa Kanda Benson Kigaila amesema mpaka sasa kwa majimbo ni 93% yaliyomaliza uchaguzi kwa tz nzima. Majimbo yaliyosalia ni 16 tu. Kauli ya Benson ameitoa leo akizungumza na Waandishi wa habari.

Kwa upande wa Mikoa ni 19 kati ya Mikoa 32 ya Kichama tayari imemaliza Uchaguzi. Kwa hali hiyo ni asilimia 59.4 % ya mikoa imemaliza mpaka jana jioni. Leo kuna mikoa 6 inafanya uchaguzi na ukikamilika itakuwa imebaki mikao 7. Mwisho wa uchaguzi wa mikoa ni tar 30/08/2014.

Wagombea wote wameaswa kufuata Kanuni za Uchaguzi pamoja na Mwongozo wa Chadema dhidi ya rushwa ambao umeambatanishwa kwenye fomu za maombi.

Naomba kuwasilisha.

Kibaja wa Msharabwe.
 
Chaguzi zinaendelea vizuri na Uchaguzi Mkuu wa Chama tarehe ni ileile yaani tar 14/09/2014
 
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kimeongeza muda wa kuomba nafasi ya kugombea Uongozi wa Kitaifa hadi tar 30/08/2014 saa kumi alasiri.

Taarifa za awali za Chama ni kuwa mwisho wa kurudisha fomu ilikuwa tarehe 25/08/2014.

Muda huo umeongezwa kutokana na maombi mengi ya wanachama mikoani ambapo chaguzi bado zinaendelea.

Mkurugenzi wa Organizesheni, Mafunzo na Usimamizi wa Kanda Benson Kigaila amesema mpaka sasa kwa majimbo ni 93% yaliyomaliza uchaguzi kwa tz nzima. Majimbo yaliyosalia ni 16 tu. Kauli ya Benson ameitoa leo akizungumza na Waandishi wa habari.

Kwa upande wa Mikoa ni 19 kati ya Mikoa 32 ya Kichama tayari imemaliza Uchaguzi. Kwa hali hiyo ni asilimia 59.4 % ya mikoa imemaliza mpaka jana jioni. Leo kuna mikoa 6 inafanya uchaguzi na ukikamilika itakuwa imebaki mikao 7. Mwisho wa uchaguzi wa mikoa ni tar 30/08/2014.

Wagombea wote wameaswa kufuata Kanuni za Uchaguzi pamoja na Mwongozo wa Chadema dhidi ya rushwa ambao umeambatanishwa kwenye fomu za maombi.

Naomba kuwasilisha.

Kibaja wa Msharabwe.
Tunashukuru kwa taarifa.

Muda umeongezwa vibaraka wasipate kisingizio kuwa hawakujua kama kuna uchaguzi.

Demokrasia inajengwa na inatakiwa ionekane ikijengwa, demokrasia sio bla bla za mdomoni.
 
Kila kitu ndani ya chadema kiko trasparent tofauti na magamba ambayo kazi yao kila jambo siri
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom