Muda wa kuoa umefika

Status
Not open for further replies.

kiduni

JF-Expert Member
Jun 26, 2015
348
341
Umri ndo huu umefika, sikutaka kukurupuka kuja hapa kuandika maana kuna kuna wengi wenye kutafuta waume niliona isiwe shida ya nami kuandika niliwafuata baadhi ya wale niloona wana vigezo ninavyovihitaji.

Nilokutana nayo;
1. Wengi hawakunijibu.
2. wachache walinijibu mawasiliano yaliishia kabla hata ya kupewa maelezo ya kina kuwahusu.
3. Wachache tuliwasiliana mpaka tukapeana namba za simu ila hatukufika mwisho maana wote niliwasiliana nao pale ninapowatafuta nilipokua kimya nao walinikaushia hivyo nikaamua kuwapotezea maana nafsi ilikataa kuwaamini na nilihisi hawana malengo kama walivyojinasibisha.

NATANGAZA NIA RASMI.
Nahitaji nipate mwanamke wa kuoa mwenye sifa zifuatazo
1. Mwanamke anayestahili kuwa mama i.e nitakayesaidiana nae kwenye malezi ya watoto sio kutegemea wafanyakazi wa ndani
2. Umri miaka 23-27
3. Mjuzi wa mapishi ningependa nile chakula kinachopikwa na yeye
4. Elimu kidato cha 4-Shahada ya 1 isiwe ya sheria
5. Rangi yoyote ila asiwe mweusi kupindukia
6. Urefu asiwe mfupi saizi ya kati napendelea
7. Asiwe mnene sana na asiwe mwembamba sana
8. Kama hajaajiriwa basi awe mwenye kujituma nikitoa mtaji asizamishe hela nitakayotoa
9. Asiwe muongeaji kupitiliza mdomo uwe na brake busara kwenye uongeaji jambo muhimu
10. Heshima awe nayo kwake, kwangu, wazazi wake, wazazi wangu na jamii kiujumla.

Sifa zangu
1. Elimu yangu shahada ya 1 uhasibu
2. Ajira nimejiajiri nafanya biashara zangu
3. Urefu futi 5 na inch 7.4
4. Rangi mweusi wa wastani
5. Ninajiheshimu, naheshimu jamii

NB:- VIGEZO NA MASHARTI KUZINGATIWA SIJAANDIKA KILA KITU KUNIHUSU HAYO NI MACHACHE MNO KATI YA MENGI NA PIA KUANDIKA HAIMAANISHI HUKU MITAANI SITAFUTI ZOEZI LIPO HAPA MTANDAONI NA HUKU MTAANI KAMA KUNA AMBAYE ATAKUA NA VIGEZO VYA ZIADA ATAPENDELEWA.
 
Check na Miss Natafuta. She is always available for a serious man who wants to get married! She is the nice woman to make a wife...
 
Imekaribia au inaelekea kuisha!!

Sasa huyo umemuita wa nini uchawi unaanzaga hivyo hivyo.
Haya nanyamaza sisy mtoto mbichi kabisa jamani huyo dada yangu ndiyo kwanza juzi kavunja peepeteo la mchele wa nyumbani
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom