Muda si mrefu tutakuwa kama Ulaya - huduma za jamii bure

gwamaka aswile

Senior Member
Mar 26, 2015
186
106
SERIKALI imeendelea kuongeza makusanyo ya mapato yake kufikia karibu Sh trilioni 1.5 katika kipindi cha Januari mwaka huu. Hii ni habari njema kwa Watanzania, kwasababu inaonesha jinsi vyanzo vyetu vya mapato vinaweza kututoa katika utegemezi wa hali ya juu kwa wahisani.

Juhudi hizi zitatufikisha kwenye utegemezi mdogo au kutuondoa huko kabisa, ikiwa vyanzo hivyo vitadhibitiwa vizuri kuhakikisha havitumiwi kujaza mifuko ya wachache. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile, makusanyo ya Januari yamevunja rekodi ya yale ya Desemba mwaka jana ambayo yalikuwa Sh trilioni 1.4.

Katika mkutano wake na wanahabari uliofanyika Dar es Salaam juzi, Dk Likwelile alisema, sasa Serikali inajivunia kugharamia miradi ya maendeleo kwa kutumia fedha za ndani, bila kutegemea za wahisani.

Aidha, aliwaeleza kuwa, makusanyo ya mapato kwa sasa ni mazuri na kila mwenye jukumu la kusimamia mapato hayo na kuyakusanya anawajibika katika eneo analopaswa, ilimradi kuhakikisha ukusanyaji haukwami.

Pia, Dk Likwelile alisema Serikali ina uhakika wa kuvuka lengo la kukusanya mapato yake yote, lengo likiwa kupunguza utegemezi na kuendesha miradi yake muhimu ya maendeleo bila kusubiri fedha za wahisani.

Alisema hilo linawezekana kutokana na mfumo mzuri uliopo sasa wa kubana matumizi yasiyo ya lazima pamoja na kuhakikisha kila anayepaswa kulipa kodi analipa kwa wakati kwa kiasi kinachostahili, si vinginevyo.

Pamoja na Dk Likwelile kueleza mafanikio hayo ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Dk John Magufuli, Watanzania wamekuwa wakijionea wenyewe matokeo chanya ya utendaji wa Serikali hiyo katika kuhakikisha maendeleo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo ya afya, elimu, uchumi na nyingine.

Hizo zote zimeanza kufanikiwa kwasababu ya kubana matumizi yasiyo ya lazima, ambayo tunaamini watanzania wengi watakuwa mashahidi kwamba Rais Magufuli amekuwa chachu kuu ya kuyabana, hivyo kutuonesha njia nyeupe ya kuelekea kuyafikia maendeleo tunayoyataka.

Majibu ya swali hili; endapo Tanzania inaweza kufanya mambo yake ya maendeleo kwa asilimia kubwa ya fedha zake na kidogo kutoka kwa wahisani au bila kutegemea mkono wa huruma kutoka kwa yeyote nje ya mipaka yake, tayari yameanza kutolewa na Serikali hii tena kwa vitendo, kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa kwa mafanikio ikiwemo ya barabara.

Hongera Serikali kwa hatua hiyo tunayoamini kuwa itatunyanyua na kuwa kidedea miongoni mwa nchi zinazoendelea, kwamba tumethubutu na kuweza kukanyaga hatua nyingi mbele bila utegemezi.

Uthibitisho kuwa tunaweza kuleta maendeleo unaonekana kwa kila mzalendo anayeukubali ukweli, kutokana na makusanyo ya mapato na fedha zinazotengwa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya vipaumbele.

Dk Likwelile alisema, kwa mwezi huu wa Januari, Serikali imetenga Sh bilioni 318.406 kutoka vyanzo vya ndani kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo iliyopewa kipaumbele. Tuunge mkono juhudi hizo kwa kulipa kodi na kutunza miradi.
 
SERIKALI imeendelea kuongeza makusanyo ya mapato yake kufikia karibu Sh trilioni 1.5 katika kipindi cha Januari mwaka huu. Hii ni habari njema kwa Watanzania, kwa sababu inaonesha jinsi vyanzo vyetu vya mapato vinaweza kututoa katika utegemezi wa hali ya juu kwa wahisani.

Juhudi hizi zitatufikisha kwenye utegemezi mdogo au kutuondoa huko kabisa, ikiwa vyanzo hivyo vitadhibitiwa vizuri kuhakikisha havitumiwi kujaza mifuko ya wachache. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile, makusanyo ya Januari yamevunja rekodi ya yale ya Desemba mwaka jana ambayo yalikuwa Sh trilioni 1.4.

Katika mkutano wake na wanahabari uliofanyika Dar es Salaam juzi, Dk Likwelile alisema, sasa Serikali inajivunia kugharamia miradi ya maendeleo kwa kutumia fedha za ndani, bila kutegemea za wahisani.

Aidha, aliwaeleza kuwa, makusanyo ya mapato kwa sasa ni mazuri na kila mwenye jukumu la kusimamia mapato hayo na kuyakusanya anawajibika katika eneo analopaswa, ilimradi kuhakikisha ukusanyaji haukwami.

Pia, Dk Likwelile alisema Serikali ina uhakika wa kuvuka lengo la kukusanya mapato yake yote, lengo likiwa kupunguza utegemezi na kuendesha miradi yake muhimu ya maendeleo bila kusubiri fedha za wahisani.

Alisema hilo linawezekana kutokana na mfumo mzuri uliopo sasa wa kubana matumizi yasiyo ya lazima pamoja na kuhakikisha kila anayepaswa kulipa kodi analipa kwa wakati kwa kiasi kinachostahili, si vinginevyo.

Pamoja na Dk Likwelile kueleza mafanikio hayo ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Dk John Magufuli, Watanzania wamekuwa wakijionea wenyewe matokeo chanya ya utendaji wa Serikali hiyo katika kuhakikisha maendeleo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo ya afya, elimu, uchumi na nyingine.

Hizo zote zimeanza kufanikiwa kwa sababu ya kubana matumizi yasiyo ya lazima, ambayo tunaamini Watanzania wengi watakuwa mashahidi kwamba Rais Magufuli amekuwa chachu kuu ya kuyabana, hivyo kutuonesha njia nyeupe ya kuelekea kuyafikia maendeleo tunayoyataka.

Majibu ya swali hili; endapo Tanzania inaweza kufanya mambo yake ya maendeleo kwa asilimia kubwa ya fedha zake, na kidogo kutoka kwa wahisani au bila kutegemea mkono wa huruma kutoka kwa yeyote nje ya mipaka yake, tayari yameanza kutolewa na Serikali hii tena kwa vitendo, kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa kwa mafanikio ikiwemo ya barabara.

Hongera Serikali kwa hatua hiyo tunayoamini kuwa itatunyanyua na kuwa kidedea miongoni mwa nchi zinazoendelea, kwamba tumethubutu na kuweza kukanyaga hatua nyingi mbele bila utegemezi.

Uthibitisho kuwa tunaweza kuleta maendeleo unaonekana kwa kila mzalendo anayeukubali ukweli, kutokana na makusanyo ya mapato na fedha zinazotengwa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya vipaumbele.

Dk Likwelile alisema, kwa mwezi huu wa Januari, Serikali imetenga Sh bilioni 318.406 kutoka vyanzo vya ndani kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo iliyopewa kipaumbele. Tuunge mkono juhudi hizo kwa kulipa kodi na kutunza miradi.
Ili uonekane kidogo hoja yako ina maana zaidi ungekokotoa vizuri kuelezea bajeti ya serikali kwa mwaka ni sh. Ngapi na hizo tunazokusanya kwa mwezi kwa mwaka ni sh.ngapi
Na kama he kwa bajeti yetu zinatosheleza? Kuliko kuisifu serikali jumla.
Wahisani hawakwepeki.
Rudi jipange upya.
 
Ili uonekane kidogo hoja yako ina maana zaidi ungekokotoa vizuri kuelezea bajeti ya serikali kwa mwaka ni sh. Ngapi na hizo tunazokusanya kwa mwezi kwa mwaka ni sh.ngapi
Na kama he kwa bajeti yetu zinatosheleza? Kuliko kuisifu serikali jumla.
Wahisani hawakwepeki.
Rudi jipange upya.
Mkuu hawa watu ni wapuuzi sana wanapenda kuongelea mambo mahimu kiujumla jumla bila kuchambua sijui maana yake nini, jamani hata km umbavu Na ulofa tulo nao sio kiasi hiki cha kutupeleka km makondoo
 
Jambo moja ni kukusanya. Jambo la pili ni matumizi sahihi.

I hope JPM atafanya yote mawili inshalah!
 
Habari hizi ni CHUNGU na UTAAMU !!
CHUNGU kwa waTanzania sbb patakuwa na zahama na mparaganyo kupata huduma muwafaka ...
Taamu kwa majirani wa Tanzania ..wananchi wa nchi jirani watamiminika hapa nchini kuhemea Ofa hiyo ya chee/bure!!

God bless Tanzania.

Miaka ya nyumba na haswa ktk serikali ya awamu ya kwanza ilijisahau , ikakaribisha wageni bila mpango wakaja kuhujumu mfumo wa elimu na ajira nchini !!! rejea Profesa Msangi!!
 
as long as tutalipa kodi ipasavyo my dear'si bure ni kodi zetu ndo zitaendesha life zetu ambavyo ndo inatakiwa iwe we are late... tangu tumeanza kulipa kodi hadi sasa tungepaswa kuwa tuna hizi huduma
 
Ukukwesa makambo nkamu vati?
Pspf wanaidai serikali zaidi ya billion 500, hapo bado hatujui wengine wanadai kiasi gani kama CWT hawa walikopwa kwenye mishemimishe za uchaguzi, Nssf, Ppf, commercial banks etc. Hayo ni yandani tu.
 
Nguvu ya soda hii.
Hata awamu iliopita tulipewa matumaini km haya lkn Tukaachwa na njaa zetu.

Tunataka kuona mabadiliko sio namba tu.
Akusanye trions 500 au shs mia 500 sisi haitusaidii kitu km mabadiliko hakuna.

Kwenda kujaza magodoro na vitanda futi 3 muhimbili hata mtu wa kawaida tu anaweza kufanya.

Tusileteane Usanii hapa.
Kwanza ile mahakama ya Mafisadi alioahidi ataijenga Kwa siku 100 za kwanza ktk ofisi iko wapi?
 
Ili uonekane kidogo hoja yako ina maana zaidi ungekokotoa vizuri kuelezea bajeti ya serikali kwa mwaka ni sh. Ngapi na hizo tunazokusanya kwa mwezi kwa mwaka ni sh.ngapi
Na kama he kwa bajeti yetu zinatosheleza? Kuliko kuisifu serikali jumla.
Wahisani hawakwepeki.
Rudi jipange upya.


Wewe ndiyo unapaswa ujipange upya, hakuna mahali ambapo mleta mada wala iliposema kwamba wahisani wanakwepeka bali mleta mada ametumia neno kupunguza utegemezi wa wahisani, yaani lengo la Serikali ni kujitegemea kwa 100% na hili huwezi kulifanya kwa mara moja bali hatua baada ya hatua hivyo hata kama tukiweza kupunguza kwa mwaka huu utegemezi mpaka 30% ktk karibia 40% bado tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana mbele na kama tukiendelea hivi hivi in maana ndani ya miaka michache tutajitegemea kwa 100% ndicho alichomaanisha!
 
Back
Top Bottom