Mubashara: Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Frederick Sumaye Kuzungumza na Taifa Kuitia wandishi wa Habari Makao Makuu ya Chadema

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Kuanzia saa 5:00 asubuhi hii tutakuwa mubashara kupitia ukurasa wa face book wa Chadema Media, M/kiti wa Chadema Kanda ya Pwani na Waziri Mkuu mstaafu Mhe. FREDERICK SUMAYE, atazungumza na taifa kupitia waandishi wa habari, leo Jumatatu 24 Desemba 2018. Usikose.
=====

Updates



Katiba mpya ingetupatia Tume Huru ya Uchaguzi, na katika nchi nchini nyingi Tume ya uchaguzi ndiyo chanzo cha machafuko, hapa kwetu Tume inafanya kazi kwa maelekezo ya watawala" Frederick Sumaye

Hakuna uwanja mpana wa kufanya siasa, ukiongea ama kutoa mitazamo yako ya siasa unaishia kukamatwa - Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye

Mfumo ambao haukubali kukosolewa au Serikali isiyokubali kukosolewa kwa kiongozi wake, ni mfumo wa kiimla au udikteta - Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye.

"Kama mchakato wa Katiba mpya ulioanzishwa na Serikali ya CCM ya awamu ya 4 haukuwa na baraka na wala haukuwa halali, basi waliofanya mchakato huo wachukukiwe hatua kwakuwa wametumia vibaya fedha za Serikali" - Sumaye

"Utawala Bora ni ule unaozingatia sheria na haki za Binadamu, Rais kupiga marufuku mikutano ya kisiasa ni kuvunja sheria za nchi kwa sababu kunakandamiza haki za raia kutoa mawazo ya kisiasa" Frederick Sumaye

Vyama vya siasa viachwe vifanye kazi yao bila kuingiliwa na mamlaka yeyote, kwa kua kila chama kina haki ya kufanya siasa - Frederick Sumaye.

Kuhusiana na Muswada wa mabadiliko ya Sheria ya vyama vya siasa, Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye, amesema endapo Muswada huo utapita basi Demokrasia ya vyama vingi itakua imezikwa kabisa, na anaefikiri amepona kwenye msafara huo anajidanganya

Kuhusu marekebisho ya muswada wa sheria ya vyama vya siasa Frederick Sumaye amesema endapo marekebisho hayo yakipita Demokrasia ya vyama vingi vya siasa Tanzania, hii itajenga hali kwa vyama vingine kuonekana kama vibaraka wa chama tawala.

"Huenda watanzania wengi hawajui kama kushamiri kwa vyama vingi vya upinzani ndio kuwepo na kuimarika kwa demokrasia hapa nchini, watanzania wasikubali kudanganywa" Frederick Sumaye

"Kuna haja gani ya uwepo wa vyama vingi kama vinazuiwa kufanya siasa zao, zinazokandamizwa na vyombo vya dola" - Frederick Sumaye

"Tunaitaka Serikali yetu kama ni sikivu iuondoe huu muswada kwa sababu unaua Demokrasia yetu ambayo iko kwenye Katiba ya nchi na ukipitisha hii unavunja Katiba kipengele cha tatu" Frederick Sumaye

"Inawezekana Takwimu za Benki Kuu zinaonyesha uchumi umekuwa sana, lakini sisi wananchi tunakuambia tuna hali mbaya sana, tukumbuke kuwa mtu mwenye njaa hatawaliki" Frederick Sumaye akizungumzia hali ya uchumi nchini

"Ombi letu kuhusu suala la Katiba bila kujali nafasi zetu wote tulinde katiba inayotuweka madarakani na tunayoapa nayo" Frederick Sumaye

Hivi juzi kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa barabara kule Kimara, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, alimuahidi Rais kua, ifikapo 2020 atamkabidhi madiwani, wabunge na mameya wote wakitokea Chama cha Mapinduzi, hii maana yake ni kwamba anataka kufuta upinzani.

Hata mimi niliwahi kumtetea Mh. Paul Makonda, kutokana na namna ya elimu yake alivyoipata pata, nalisema elimu aliyonayo tofauti na majukumu aliyopewa, huyo aliyempa hiyo kazi ni vema angembadilishia kitengo - Frederick Sumaye.

Kwa taarifa tulizonazo umma wote wa Tanzania umechoka kuona haya yanayoendelea, umma umechoka kusikia haya mambo,lakini umma umekufa ganzi kwa ajili ya woga -Frederick Sumaye
 
Kuanzia saa 5:00 asubuhi hii tutakuwa mubashara kupitia ukurasa wa face book wa Chadema Media, M/kiti wa Chadema Kanda ya Pwani na Waziri Mkuu mstaafu Mhe. FREDERICK SUMAYE, atazungumza na taifa kupitia waandishi wa habari, leo Jumatatu 24 Desemba 2018. Usikose.
=====

Updates
Anaongea kama Kaimu Mwenyekiti!
 
Napenda amshauri mkuu pia mazingira mabaya aliyopandikiza kwa maelekezo,Baraka zake kwa siasa za hovyo Tanzania, ndio leo KUB na wengine wana kesi lukuki,vifungo ,kupotea,mateso na vifo.CDM INA wafuasi wangapi!? Watanzania na wana ccm wangapi wanafurahia upuuzi huu kuharibu umoja na ustawi wa taifa letu!?
Mkono wa amani ni suluhu kubwa kuliko jeshi na vifaru.
 
Kuanzia saa 5:00 asubuhi hii tutakuwa mubashara kupitia ukurasa wa face book wa Chadema Media, M/kiti wa Chadema Kanda ya Pwani na Waziri Mkuu mstaafu Mhe. FREDERICK SUMAYE, atazungumza na taifa kupitia waandishi wa habari, leo Jumatatu 24 Desemba 2018. Usikose.
=====

Updates
Anazungumza na taifa kupitia ukurasa wa facebook?Hiki kituko kweli ina maana chadema hakuna fedha ya kurusha matangazo live kupitia Tv channel yoyote.
 
Huyo Anaitwa Mr ziro kila akalosema ni ziro kabisa et atazungumza na Taifa kutokea ufipa taifa gani hilo? linalomjuwa Mr Ziro!!!
Acha dharau hata baba yako ni zero huwezi kukwambia mtu mzima kama yule Taifa linamheshimu halafu mjinga mmoja unamtukana kwanini usikae kimya
 
Back
Top Bottom