Muasisi wa CHADEMA atofautiana na Wabunge wa CHADEMA

Mashayo

Member
May 29, 2007
22
0
Soma hizi habari tatu kwa makini, kisha naomba maoni yako:-

"Wabunge wa Chadema walikataa bungeni Pinda asiwe Waziri Mkuu na pia chama hicho hakimtambui Jakaya Kikwete kuwa ni Rais halali wa Tanzania. "
(Source: HABARI LEO HabariLeo | Wabunge Chadema wasusa

"SIKU mbili baada ya Mbunge wa Jimbo la Katavi, Mizengo Pinda, kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete na kupitishwa na Bunge, kushika wadhifa wa uwaziri mkuu, Muasisi wa Chadema, Edwin Mtei, amepongeza uteuzi huo.."
(Source: MWANANCHI:Muasisi wa Chadema ampongeza Pinda)

"Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wameamua kutoka nje ya Bunge mara baada ya Rais wa nchi, Jakaya Kikwete kuanza kuhutubia Bungeni. Wabunge hao wametimiza adhima yao ya kutoka nje ya Bunge kama walivyoahidi hapo mwanzo kwa kile kinachodaiwa kuwa hawamtambui Dkt Kikwete kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania." (Source: Global Publishers, BREAKING NEWS: WABUNGE WA CHADEMA WATOKA BUNGENI! - Global Publishers)

Je hii habari ya pili kama ilivyotolewa na gazeti la MWANANCHI ni ya kweli? Na kama ni ya kweli, Je Mzee wetu Edwin Mtei alitamka pongezi hizi kama yeye (at personal level) au kama chama? Na kama alitamka kama chama, je kuna haja ya chama kubatilisha tamko hili?

NB: Ninavyofahamu, Uteuzi wa Waziri Mkuu ni moja ya shughuli ya Raisi. Waziri Mkuu ni Kiongozi Mkuu wa shughuli za serikali bungeni. Kupongeza uteuzi huo ni kumpongeza Raisi kwa kufanya shughuli yake kwa ufanisi. Ukipongeza shughuli za Raisi kwa lugha nyingine ni kusema unamtambua Raisi. Kama nimeelewa tofauti naomba nieleweshwe tafadhali.
 
Soma hizi habari tatu kwa makini, kisha naomba maoni yako:-

"Wabunge wa Chadema walikataa bungeni Pinda asiwe Waziri Mkuu na pia chama hicho hakimtambui Jakaya Kikwete kuwa ni Rais halali wa Tanzania. "
(Source: HABARI LEO HabariLeo | Wabunge Chadema wasusa

"SIKU mbili baada ya Mbunge wa Jimbo la Katavi, Mizengo Pinda, kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete na kupitishwa na Bunge, kushika wadhifa wa uwaziri mkuu, Muasisi wa Chadema, Edwin Mtei, amepongeza uteuzi huo.."
(Source: MWANANCHI:Muasisi wa Chadema ampongeza Pinda)

"Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wameamua kutoka nje ya Bunge mara baada ya Rais wa nchi, Jakaya Kikwete kuanza kuhutubia Bungeni. Wabunge hao wametimiza adhima yao ya kutoka nje ya Bunge kama walivyoahidi hapo mwanzo kwa kile kinachodaiwa kuwa hawamtambui Dkt Kikwete kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania." (Source: Global Publishers, BREAKING NEWS: WABUNGE WA CHADEMA WATOKA BUNGENI! - Global Publishers) "usilete sorce kama hii hapa wengine hatuthubutu hata kusoma ukurasa wa kuokota "

Je hii habari ya pili kama ilivyotolewa na gazeti la MWANANCHI ni ya kweli? Na kama ni ya kweli, Je Mzee wetu Edwin Mtei alitamka pongezi hizi kama yeye (at personal level) au kama chama? Na kama alitamka kama chama, je kuna haja ya chama kubatilisha tamko hili?

NB: Ninavyofahamu, Uteuzi wa Waziri Mkuu ni moja ya shughuli ya Raisi. Waziri Mkuu ni Kiongozi Mkuu wa shughuli za serikali bungeni. Kupongeza uteuzi huo ni kumpongeza Raisi kwa kufanya shughuli yake kwa ufanisi. Ukipongeza shughuli za Raisi kwa lugha nyingine ni kusema unamtambua Raisi. Kama nimeelewa tofauti naomba nieleweshwe tafadhali.

Tatizo liko wapi?? Umeambiwa mzee Mtei ni kiongozi wa CHADEMA?? Mbona CCM huwa hawasikilizi ushauli wa kina BUTIKU,WARIOBA nk, hiyo haimaanishi utashi wao ndio maamuzi ya CHAMA,chama kina viongozi.
 
Sio Mtei tu, hata viongozi na wabunge wengine wa chadema hawatambui. Kutokumtambua Rais ni utashi binafsi wa Mbowe uliopokelewa kwa "ndio" na Dr. Slaa na sasa wameushinikiza kwa other Chadema juniors. Zitto na Ndesamburo hawaungi hili.
 
Tatizo liko wapi?? Umeambiwa mzee Mtei ni kiongozi wa CHADEMA?? Mbona CCM huwa hawasikilizi ushauli wa kina BUTIKU,WARIOBA nk, hiyo haimaanishi utashi wao ndio maamuzi ya CHAMA,chama kina viongozi.

kamati kuu ya Chadema hii hapa:
1.Freeman Aikael Mbowe -Mwenyekiti
2.Said Amour Arfi (MB)- M/Mwenyekiti Bara
3.Said Issa Mohamed- M/mwenyekiti Zanzibar
4.Dr Wilbrod Peter Slaa- Katibu Mkuu
5. Zitto Zuberi Kabwe- Naibu Katibu Mkuu Bara
6.Hamad Mussa Yusuph-Naibu Katibu Mkuu Zanzibar
6. Edwin Mtei- Mwenyekiti Mstaafu
7.Bob N Makani- Mwenyekiti Mstaafu
8.Philemon Ndessamburo(MB)
9.Mhonga Said Ruhanywa (MB)
10.Shaban Mambo-Mwenyekiti Umoja wa Madiwani
11.Lazaro Massai-Mwenyekiti wa Halmashauri Karatu
12.Philip Shelembi
13.Susan Lyimo(MB)
14.Mwanamrisho Abama-Zanzibar
15.Prof Mwesiga Baregu
16.Dk Kitilla Mkumbo
17.Nassor Ally Salim -Zanzibar
18.Regia Estelatus Mtema- Mjumbe mdogo kuliko wote kwa kuchaguliwa
19.Shida Salum Bitaliho
20.Leticia G Mosore-Mwenyekiti -Baraza la Wanawake CHADEMA(BAWACHA)
21.Susan H Kiwanga
22.Grace Kiwelu(MB)
23.Paul Herman Sule- Katibu wa Umoja wa Madiwani
24.Charles Mwera(MB) na Mwenyekiti wa Halmashauri Tarime
25.Nyangaki Silungushela- Mwenyekiti Baraza la Wazee CHADEMA
26.John Mnyika-Mkurugenzi
27.John Mrema-Mkurugenzi
28.Benson Kigaila-Mkurugenzi
29.Msafiri Mtemelwa-Mkurugenzi
30.Victor P Kimesera-Mkurugenzi

For more refer here https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...okana-na-kikao-cha-kamati-kuu-ya-chadema.html
 
Sio Mtei tu, hata viongozi na wabunge wengine wa chadema hawatambui. Kutokumtambua Rais ni utashi binafsi wa Mbowe uliopokelewa kwa "ndio" na Dr. Slaa na sasa wameushinikiza kwa other Chadema juniors. Zitto na Ndesamburo hawaungi hili.
Mmmmh! Zito na Ndesamburo walitoka hawakutoka ukumbini? Acha kuwatukana wabunge wa CHADEMA kuwa hawana maamuzi yao wenyewe.
 
Back
Top Bottom