BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Hivi nchi ingekuwa na sheria, hawa mapapa mafisadi wangekuwa na kiburi walichokuwa nacho!? Sitta bora ukae kimya tu na kuwaacha wenye uchungu wa Tanzania kupambana na hawa mafisadi bila woga. Maana uongozi uliokuwepo unawaogopa na sababu za kuogopwa kwao zinajulikana.
SPIKA wa Bunge la Tanzania Samuel Sita, amewataka wafanyabiashara na wanasiasa wanaotuhumiana kupitia vyombo vya habari kuachana na tabia hiyo na kuziacha sheria za nchi zichukue mkondo wake.
Akijibu swali kutoka kwa mmoja wa wanahabari aliyetaka kujua maoni yake kuhusiana na wafanyabiashara wanao hukumiana kwa kuitana mafisadi, Sita alisema kitendo hicho siyo kizuri kwa sababu kuna sheria.
"Nasita kidogo kuwasema wafanyabiashara kwa sababu labda wana maslahi yao binafsi, lakini suala la kuhukumiana siyo zuri, tuache sheria zifuate mkondo wake, kama mtu tayari kafikishwa mahakamani tuache mahakama ifanye kazi na pale itokapo hukumu ndio tumuite fisadi au majina yote yale mabaya," alisema Sita.
Sita ambaye alikuwa mgeni rasmi katika siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, aliyasema hayo jana nje ya ukumbi wa Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Mapema wakati akitoa hotuba yake Sita aliwataka wanahabari kutokubali kutumiwa na wanasiasa na matajiri ili kutoa habari zisizo na tija kwa nchi pamoja na kuingiza chuki na ubinafsi.
Katika hatua nyingine Sita aliwataka wanahabari kushikamana kuhakikisha sheria zinazokandamiza uhuru wa vyombo vya habari nchini zinabadilishwa.
Sita ambaye alitolea mfano sheria ya magazeti ya mwaka 1976 pamoja na sheria ya usalama wa taifa ya mwaka 1995, aliitaka serikali kuzipeleka bungeni sheria zinazolalamikiwa ili ziweze kufanyiwa marekebisho.
"Natoa wito kwa serikali kuziwasilisha bungeni mapema iwezekanavyo sheria zote zinazo lalamikiwa ili ziweze kufanyiwa marekebisho, binafsi naunga mkono jitihada zote zitakazo leta uhuru wa vyombo vya habari nchini," alisema Sita.
Siku ya uhuru wa vyombo vya habari huadhimishwa duniani kila mwaka Mei 3.
Date::5/4/2009
Sita aonya malumbano yasiyo na tija
Fredy Azzah
Mwananchi
Sita aonya malumbano yasiyo na tija
Fredy Azzah
Mwananchi
SPIKA wa Bunge la Tanzania Samuel Sita, amewataka wafanyabiashara na wanasiasa wanaotuhumiana kupitia vyombo vya habari kuachana na tabia hiyo na kuziacha sheria za nchi zichukue mkondo wake.
Akijibu swali kutoka kwa mmoja wa wanahabari aliyetaka kujua maoni yake kuhusiana na wafanyabiashara wanao hukumiana kwa kuitana mafisadi, Sita alisema kitendo hicho siyo kizuri kwa sababu kuna sheria.
"Nasita kidogo kuwasema wafanyabiashara kwa sababu labda wana maslahi yao binafsi, lakini suala la kuhukumiana siyo zuri, tuache sheria zifuate mkondo wake, kama mtu tayari kafikishwa mahakamani tuache mahakama ifanye kazi na pale itokapo hukumu ndio tumuite fisadi au majina yote yale mabaya," alisema Sita.
Sita ambaye alikuwa mgeni rasmi katika siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, aliyasema hayo jana nje ya ukumbi wa Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Mapema wakati akitoa hotuba yake Sita aliwataka wanahabari kutokubali kutumiwa na wanasiasa na matajiri ili kutoa habari zisizo na tija kwa nchi pamoja na kuingiza chuki na ubinafsi.
Katika hatua nyingine Sita aliwataka wanahabari kushikamana kuhakikisha sheria zinazokandamiza uhuru wa vyombo vya habari nchini zinabadilishwa.
Sita ambaye alitolea mfano sheria ya magazeti ya mwaka 1976 pamoja na sheria ya usalama wa taifa ya mwaka 1995, aliitaka serikali kuzipeleka bungeni sheria zinazolalamikiwa ili ziweze kufanyiwa marekebisho.
"Natoa wito kwa serikali kuziwasilisha bungeni mapema iwezekanavyo sheria zote zinazo lalamikiwa ili ziweze kufanyiwa marekebisho, binafsi naunga mkono jitihada zote zitakazo leta uhuru wa vyombo vya habari nchini," alisema Sita.
Siku ya uhuru wa vyombo vya habari huadhimishwa duniani kila mwaka Mei 3.