Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Mataifa wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, yamekubali kumteua Fatou Bensouda kutoka Gambia, kuwa mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama hiyo, inayoshughulikia kesi za uhalifu wa kivita. Kwa sasa Bensouda, mwenye miaka 50, ni naibu wa mwendesha mashtaka mkuu, Luis Moreno-Ocampo, ambaye anamaliza kipindi chake cha miaka tisa mwakani. Bensouda ameibuka kama chaguo la karibuni wanachama wote 120 wa mahakama hiyo, baada ya mgombea mwengine aliyekuwa akipewa nafasi kushikilia wadhifa huo, Jaji Mkuu* wa Tanzania Mohammed Chande Othman, kuondoa jina lake.