MUAFAKA: Kusuasua na Ufafanuzi wa Kikwete - Je, Yote ni Msukumo Kutoka Nje?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Muafaka: JK sasa mambo mazito

2008-05-14 16:09:08
Na Usu-Emma Sindila, Buguruni

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bwana Jakaya Kikwete sasa amewekwa kwenye mtihani mgumu kufuatia chama cha upinzani cha CUF, kuapa kwamba, kamwe hakitarudi kwenye meza ya mazungumzo.

Kinachofanya mambo yawe mazito kwa kiongozi huyo wa nchi, ni chama hicho kumbwagia sakata hilo zito JK na kukataa kata kata kuendelea kulijadili kama vyama.

Katibu Mwenza wa CUF, Bw. Ismail Jussa Ladhu, kurudi kwenye meza ya mazungumzo na CCM ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi.

Bw. Ladhu ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Makao Mkuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni, amesema kwa sasa mtu pekee anayeweza kuokoa jahazi
hilo ni rais Kikwete.

``Tukubali, tusikubali rais Kikwete ndiye mwenye uwezo wa kuokoa jahazi hili, na hatuwezi kurudi katika meza ya mazungumzo tena, kwa kuwa ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi wetu,`` akasisitiza.

Amesema bado nafasi ipo na kwamba kama JK atakaoonyesha nia ya kutaka kuzungumza nao, watampa nafasi na ushirikiano unaotakiwa.

Licha ya chama hicho kumwachia jukumu hilo zito rais Kikwete, kimetaka suala hilo lisichezewe shere kwani ni zito na linahusu mustakabali wa taifa.

Amesema kwa hatua iliyofikiwa sasa, ni budi suala hilo likashughulikiwa kama yalivyoshughulikiwa masuala ya Kenya, Comoro na la sasa la Zimbabwe.

Bw. Ladhu amesema njia pekee za kuweza kufikia makubaliano katika mazungumzo hayo ya muafaka, ni kwa CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na kamati ya mazungumzo ya vyama vyote viwili na endapo Halmashauri Kuu ya CCM imeyakubali kimsingi, basi wakubali kutia saini na utekelezaji uanze mara moja.

Amesema njia nyingine ni kwa Rais Kikwete kuchukua hatua za haraka kuitisha mkutano wa pamoja kati yake na wadau wakuu wa masuala hayo ya Zanzibar, ambao ni Rais Amani Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad kujadili na kukubaliana juu ya mapendekezo yaliyotolewa na NEC.

Chama hicho kimewaomba wanachama wake wa Zanzibar
na Bara kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki.

SOURCE: Alasiri
 
Muafaka: JK sasa mambo mazito

2008-05-14 16:09:08
Na Usu-Emma Sindila, Buguruni

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bwana Jakaya Kikwete sasa amewekwa kwenye mtihani mgumu kufuatia chama cha upinzani cha CUF, kuapa kwamba, kamwe hakitarudi kwenye meza ya mazungumzo.

Kinachofanya mambo yawe mazito kwa kiongozi huyo wa nchi, ni chama hicho kumbwagia sakata hilo zito JK na kukataa kata kata kuendelea kulijadili kama vyama.

Katibu Mwenza wa CUF, Bw. Ismail Jussa Ladhu, kurudi kwenye meza ya mazungumzo na CCM ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi.

Bw. Ladhu ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Makao Mkuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni, amesema kwa sasa mtu pekee anayeweza kuokoa jahazi
hilo ni rais Kikwete.

``Tukubali, tusikubali rais Kikwete ndiye mwenye uwezo wa kuokoa jahazi hili, na hatuwezi kurudi katika meza ya mazungumzo tena, kwa kuwa ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi wetu,`` akasisitiza.

Amesema bado nafasi ipo na kwamba kama JK atakaoonyesha nia ya kutaka kuzungumza nao, watampa nafasi na ushirikiano unaotakiwa.

Licha ya chama hicho kumwachia jukumu hilo zito rais Kikwete, kimetaka suala hilo lisichezewe shere kwani ni zito na linahusu mustakabali wa taifa.

Amesema kwa hatua iliyofikiwa sasa, ni budi suala hilo likashughulikiwa kama yalivyoshughulikiwa masuala ya Kenya, Comoro na la sasa la Zimbabwe.

Bw. Ladhu amesema njia pekee za kuweza kufikia makubaliano katika mazungumzo hayo ya muafaka, ni kwa CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na kamati ya mazungumzo ya vyama vyote viwili na endapo Halmashauri Kuu ya CCM imeyakubali kimsingi, basi wakubali kutia saini na utekelezaji uanze mara moja.

Amesema njia nyingine ni kwa Rais Kikwete kuchukua hatua za haraka kuitisha mkutano wa pamoja kati yake na wadau wakuu wa masuala hayo ya Zanzibar, ambao ni Rais Amani Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad kujadili na kukubaliana juu ya mapendekezo yaliyotolewa na NEC.

Chama hicho kimewaomba wanachama wake wa Zanzibar
na Bara kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki.

SOURCE: Alasiri

Mheshimiwa Ismael Jussa Ladhu (Kumbaro wa Shamba) Kwa nini unashadidia tu Rais Karume akutane na Seif. Mdau mkubwa wa suala la muafaka nni CCM Bwana rudi mezani ukutane na Kamati ya mazungumzo iliyoteuliwa.
 
Mheshimiwa Ismael Jussa Ladhu (Kumbaro wa Shamba) Kwa nini unashadidia tu Rais Karume akutane na Seif. Mdau mkubwa wa suala la muafaka nni CCM Bwana rudi mezani ukutane na Kamati ya mazungumzo iliyoteuliwa.


And u dont see how much CCM are not serious on this, kama kushare power kati ya CUF an CCM ni uhaini, JK alifata nini Kenya? kwa nini kama kiongozi wa jumuiya ya Africa asikatae share of power ya ODM na na chama cha Kibaki kama ni uhaini

yeye si bingwa msuluhishi, haoni kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo nyumbani kwake.... si muda mrefu atajulikani how incompitent he is usoni mwa hao mataifa nayo jitutmua kujionyeshe na kutafuta sifa
 
hivi kule zanzibar mshindi si anajulikana kuwa ni CCM, na mazungumzo yanalenga kuweka mazingira sawa ya kuondosha manun'guniko yasioisha kila uchaguzi?


sasa hali inafananaje na kenya ambapo mshindi wa moja kwa moja hakuwepo?
 
Muafaka: JK sasa mambo mazito

2008-05-14 16:09:08
Na Usu-Emma Sindila, Buguruni

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bwana Jakaya Kikwete sasa amewekwa kwenye mtihani mgumu kufuatia chama cha upinzani cha CUF, kuapa kwamba, kamwe hakitarudi kwenye meza ya mazungumzo.

Kinachofanya mambo yawe mazito kwa kiongozi huyo wa nchi, ni chama hicho kumbwagia sakata hilo zito JK na kukataa kata kata kuendelea kulijadili kama vyama.

Katibu Mwenza wa CUF, Bw. Ismail Jussa Ladhu, kurudi kwenye meza ya mazungumzo na CCM ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi.

Bw. Ladhu ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Makao Mkuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni, amesema kwa sasa mtu pekee anayeweza kuokoa jahazi
hilo ni rais Kikwete.

``Tukubali, tusikubali rais Kikwete ndiye mwenye uwezo wa kuokoa jahazi hili, na hatuwezi kurudi katika meza ya mazungumzo tena, kwa kuwa ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi wetu,`` akasisitiza.

Amesema bado nafasi ipo na kwamba kama JK atakaoonyesha nia ya kutaka kuzungumza nao, watampa nafasi na ushirikiano unaotakiwa.

Licha ya chama hicho kumwachia jukumu hilo zito rais Kikwete, kimetaka suala hilo lisichezewe shere kwani ni zito na linahusu mustakabali wa taifa.

Amesema kwa hatua iliyofikiwa sasa, ni budi suala hilo likashughulikiwa kama yalivyoshughulikiwa masuala ya Kenya, Comoro na la sasa la Zimbabwe.

Bw. Ladhu amesema njia pekee za kuweza kufikia makubaliano katika mazungumzo hayo ya muafaka, ni kwa CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na kamati ya mazungumzo ya vyama vyote viwili na endapo Halmashauri Kuu ya CCM imeyakubali kimsingi, basi wakubali kutia saini na utekelezaji uanze mara moja.

Amesema njia nyingine ni kwa Rais Kikwete kuchukua hatua za haraka kuitisha mkutano wa pamoja kati yake na wadau wakuu wa masuala hayo ya Zanzibar, ambao ni Rais Amani Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad kujadili na kukubaliana juu ya mapendekezo yaliyotolewa na NEC.

Chama hicho kimewaomba wanachama wake wa Zanzibar
na Bara kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki.

SOURCE: Alasiri

BUBU

Mzee tunakuomba next time post paragraph moja au mili za mwanzo kusha weka lina kwa sababu ya masuala ya copyright.

hilo ni ombi tuu

mfano hivi:


Jeshi la Polisi nchini, limesema halitawaruhusu ndugu wa watuhumiwa wa `uhaini` waliokamatwa kisiwani Pemba kwenda kuwajulia hali mahala wanakohifadhiwa.

Aidha, jeshi hilo limesema ndugu hao wasiwe na wasiwasi kwani ndugu zao wako salama na wakiumwa wanapatiwa huduma za kimatibabu kama binadamu wengine.


http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/05/15/114417.html

hii itatuondolea kadhia ya kujibu barua za hawa watu wenye mipango ya ku sue na ma lawyers ambao wanahustle kutafuta kesi kwa niaba ya haya magazeti

Nia si kuharibu bali nia ni kuwekana sawa na kulindana
 
BUBU

Mzee tunakuomba next time post paragraph moja au mili za mwanzo kusha weka lina kwa sababu ya masuala ya copyright.

hilo ni ombi tuu

mfano hivi:




hii itatuondolea kadhia ya kujibu barua za hawa watu wenye mipango ya ku sue na ma lawyers ambao wanahustle kutafuta kesi kwa niaba ya haya magazeti

Nia si kuharibu bali nia ni kuwekana sawa na kulindana

asante Gt kwa kuliona hilo.
 
Marufuku kuwaona

2008-05-15 09:14:57
Na Dunstan Bahai


Jeshi la Polisi nchini, limesema halitawaruhusu ndugu wa watuhumiwa wa `uhaini` waliokamatwa kisiwani Pemba kwenda kuwajulia hali mahala wanakohifadhiwa.

Aidha, jeshi hilo limesema ndugu hao wasiwe na wasiwasi kwani ndugu zao wako salama na wakiumwa wanapatiwa huduma za kimatibabu kama binadamu wengine.

Kauli hiyo ilitolewa na Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Bw. Khamis Mohammed Simba, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu.

Bw. Simba alikuwa ameombwa aeleze waliko watuhumiwa hao na kama ndugu wanaweza kwenda kuwajulia hali.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI..

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL
COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,

DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI..
Sasa wakati wa kurudi mezani,Rais aviambia CCM and CUFAsema vyama hivyo vinakubaliana kimsingi na kuwa tofauti ni utekelezajiRAIS Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa baada ya vyama CCM na CUF kuwa vimeweka misimamo yao kuhusu Mwafaka hadharani, sasa ni wakati wa kurudi mezani kuendeleza majadiliano.
Rais pia amesema kuwa anaamini kuwa majadiliano hayo hatimaye yatazaa matunda mazuri kwa mustakabali wa Tanzania.Rais ameyaeleza hayo kwa nyakati tofauti leo katika majadiliano na wageni ambao alikutana nao Ikulu,mjini Dar es Salaam.

mazungumzo yake na Waziri wa Nchi wa Ufaransa anayeshughulikia Mahusiano ya Kimataifa na Nchi Zinazozungumza Kifaransa, Alain Joyandet, Rais ametumia muda kumwelezea mgeni historia ya majadiliano ya mwafaka na sababu za msingi zilizopelekea kuanzishwa kwa majadiliano hayo.“Naamini mambo yatakwenda vizuri.

Hatimaye tutafanikiwa katika hili la mazungumzo la Mwafaka,” amesema Rais Kikwete na kuongeza kuwa, kimsingi, CCM na CUF vinakubaliana kuhusu mambo ya kufanyika juu ya Mwafaka, na kuwa tofauti ni katika utekelezaji wa hayo yaliyokubaliwa.“CCM wanataka suala hilo kubwa la msingi liamuliwe moja kwa moja na wananchi.

CUF wao wanataka wanasiasa kuamua kwa niaba ya wananchi. Hivyo, tofauti iko katika namna ya kutekeleza yaliyokubaliwa,” amesema.Rais pia amemweleza Waziri huyo kuwa uamuzi wa kuwa na Serikali Shirikishi katika Zanzibar ulichukuliwa miaka saba iliyopita, mwaka 2001, wakati wa majadiliano yaliyozaa Mwafaka wa Kwanza kati ya CCM na CUF.

Rais amesisitiza kuwa uamuzi wa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM katika kikao chake cha karibu cha Butiama, Musoma haukubadilisha makubaliano ya msingi kati ya vyama hivyo.“Kilichofanyika ni CCM kuongeza mapendekezo mawili ili nayo yajadiliwe na timu za vyama hivyo viwili.”Amesema kuwa pendekezo moja ni kuwashirikisha wananchi kuamua utekelezaji wa mwafaka kati ya vyama hivyo,na la pili ni kuweka utaratibu wa ukomo wa utekelezaji (sunset clause) wa mwafaka huo.

Amesema “mwafaka unalenga kuitoa Zanzibar katika matatizo ya sasa ya kisiasa. Hauwezi kuwa utaratibu wa daima dumu na kuwa ukifika wakati kuwa mfumo huo wa utawala wa kisiasa umekamilisha kazi yake, basi unaweza kuondolewa na Zanzibar ikarudi katika ushindani wa kawaida wa kisiasa.”Amesema kuwa hivyo ndivyo ilivyokuwa katika nchi za Afrika Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),na sasa katika Kenya.

Katika mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Kenya, Adam Woods, Rais amesisitiza kuwa bado iko nafasi ya kuokoa mazungumzo hayo ya Mwafaka.“Wote sasa wamezungumza kiasi cha kutosha. Sasa ni wakati wa kukaa chini na kuendelea na mazungumzo,” Rais amemweleza Balozi huyo.Amesisitiza: “Maamuzi ya CCM hajabadilisha jambo lolote la msingi katika makubaliano ya Mwafaka –no deviation on fundamental agreement – Tulichofanya sisi ni kuongeza jambo la kuwashirikisha wananchi na kuwataka wanaoendesha majadiliano kulifikiria na hili.”
---------------
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
15 Mei, 2008
 
"Maamuzi ya CCM hajabadilisha jambo lolote la msingi katika makubaliano ya Mwafaka –no deviation on fundamental agreement – Tulichofanya sisi ni kuongeza jambo la kuwashirikisha wananchi na kuwataka wanaoendesha majadiliano kulifikiria na hili."

pole pole anaanza kujikosha, kujitoa kwenye majigambo ya wenzake wa CCM!!

Nini maana ya "kulifikiria", rejea kauli za Makamba, Kingung'e, Shamhuna, Karume, ... CCM inajikanyaga sana, kwani kila mtu ndani ya chama ni msemaji!!
 
ccm huwashindi kwa kubadilisha maneno kama vinyonga.
na hii yote inachochewa na kila mmoja kuwa msemaji wa chama. jana tu UVCCM wamesema kama itakuwa noma na iwe, leo kikwete anatwambia walitaka suala la kura ya maoni lifikiriwe na wanaojadili muafaka.
ni kutudanganya kama watoto wadogo, lakini tanzania ya leo siyo ile ya zamani ambalo kila linalosemwa na rais halipimwi
 
na wale wapemba wanaobebwa usiku na kupelekwa kusikojulikana kwa kisingizio cha uhaini? ni mwalimu nyerere peke yake aliyeweza kugeuza upepo wa hardliners mwaka 1992, pale UVCCM walipomwalika mwanzo ili atoe maoni yake kuhusu kuwepo kwa vyama vingi, wengi wakiwa kwenye usingizi wa chama kimoja, na wengine wakiapa kuwa vyama vingi vikija watajichimbia kwenye mashimo eti wafie huko, yeye aliwaambia wampe sababu za mwaka 1992 za kutokuwa na vyama vingi~!!!, wakamshangaa na leo vyama vingi vipo, kama kikwete anataka historia awaite hardliners akina karume na wengine na awaaulize je mnazo sababu za mwaka 2008 za kutokuwa na serikali ya mseto zamzibar? bila shalka hawana watabaki kuzungumzia historia ta hizbu na ASP!!!, hapo jibu la makato liwe rudini zanzibar mkaiunde hiyo serikali au andikeni barua za kujiuzulu kama aboud jumbe... je kiwete anaweza??
 
Wacheni kumpa bichwa Kikwete ,hivi ni wapi alisuluisha ? Maana katika makubaliano nilichoona ni Kofi Oginga na Kibaki akina Kikwete wakiwepo nyuma kama mashaidi tu,inawezekana ni shaidi mzuri tu ,hata uko Butiama si amieenda kushuudia tu ,wakati alikuwa anatudanganya kuwa atahakikisha matatizo yataisha muda si mrefu ,kumbe jamaa ameenda kuzidisha matatizo ,watu wengine mi huwaga nawatizama tu maana haifai kuingiliana katika anga ,kila nikimuangalia Muungwana naona ni mtu wa maneno mengi anaweza akazuga zuga hapa na kutuwacha hoi ,hivi nasubiri hotuba yake ya kila mwisho wa mwezi nipate kufurai ,kusema kweli mi hufurahi na huwa nafarijika kila nikimsikiliza ,maana akimaliza basi na mimi huwaga nimeshiba kabisa,kumbe sijakula kitu.
 
Cuf Sasa Wekeni Sharti Lingine Kwamba Hakuna Maongezi Kwani Kama Mazungumzo Yangeisha Haya Sasa Ni Maongezi,so Hakuna Maongezi Hadi Wapemba Wanaotaka Jamuhuri Yao Waachiwe
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI..

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL
COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,

DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI..
Sasa wakati wa kurudi mezani,Rais aviambia CCM and CUFAsema vyama hivyo vinakubaliana kimsingi na kuwa tofauti ni utekelezajiRAIS Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa baada ya vyama CCM na CUF kuwa vimeweka misimamo yao kuhusu Mwafaka hadharani, sasa ni wakati wa kurudi mezani kuendeleza majadiliano.
Rais pia amesema kuwa anaamini kuwa majadiliano hayo hatimaye yatazaa matunda mazuri kwa mustakabali wa Tanzania.Rais ameyaeleza hayo kwa nyakati tofauti leo katika majadiliano na wageni ambao alikutana nao Ikulu,mjini Dar es Salaam.

mazungumzo yake na Waziri wa Nchi wa Ufaransa anayeshughulikia Mahusiano ya Kimataifa na Nchi Zinazozungumza Kifaransa, Alain Joyandet, Rais ametumia muda kumwelezea mgeni historia ya majadiliano ya mwafaka na sababu za msingi zilizopelekea kuanzishwa kwa majadiliano hayo.“Naamini mambo yatakwenda vizuri.

Hatimaye tutafanikiwa katika hili la mazungumzo la Mwafaka,” amesema Rais Kikwete na kuongeza kuwa, kimsingi, CCM na CUF vinakubaliana kuhusu mambo ya kufanyika juu ya Mwafaka, na kuwa tofauti ni katika utekelezaji wa hayo yaliyokubaliwa.“CCM wanataka suala hilo kubwa la msingi liamuliwe moja kwa moja na wananchi.

CUF wao wanataka wanasiasa kuamua kwa niaba ya wananchi. Hivyo, tofauti iko katika namna ya kutekeleza yaliyokubaliwa,” amesema.Rais pia amemweleza Waziri huyo kuwa uamuzi wa kuwa na Serikali Shirikishi katika Zanzibar ulichukuliwa miaka saba iliyopita, mwaka 2001, wakati wa majadiliano yaliyozaa Mwafaka wa Kwanza kati ya CCM na CUF.

Rais amesisitiza kuwa uamuzi wa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM katika kikao chake cha karibu cha Butiama, Musoma haukubadilisha makubaliano ya msingi kati ya vyama hivyo.“Kilichofanyika ni CCM kuongeza mapendekezo mawili ili nayo yajadiliwe na timu za vyama hivyo viwili.”Amesema kuwa pendekezo moja ni kuwashirikisha wananchi kuamua utekelezaji wa mwafaka kati ya vyama hivyo,na la pili ni kuweka utaratibu wa ukomo wa utekelezaji (sunset clause) wa mwafaka huo.

Amesema “mwafaka unalenga kuitoa Zanzibar katika matatizo ya sasa ya kisiasa. Hauwezi kuwa utaratibu wa daima dumu na kuwa ukifika wakati kuwa mfumo huo wa utawala wa kisiasa umekamilisha kazi yake, basi unaweza kuondolewa na Zanzibar ikarudi katika ushindani wa kawaida wa kisiasa.”Amesema kuwa hivyo ndivyo ilivyokuwa katika nchi za Afrika Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),na sasa katika Kenya.

Katika mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Kenya, Adam Woods, Rais amesisitiza kuwa bado iko nafasi ya kuokoa mazungumzo hayo ya Mwafaka.“Wote sasa wamezungumza kiasi cha kutosha. Sasa ni wakati wa kukaa chini na kuendelea na mazungumzo,” Rais amemweleza Balozi huyo.Amesisitiza: “Maamuzi ya CCM hajabadilisha jambo lolote la msingi katika makubaliano ya Mwafaka –no deviation on fundamental agreement – Tulichofanya sisi ni kuongeza jambo la kuwashirikisha wananchi na kuwataka wanaoendesha majadiliano kulifikiria na hili.”
---------------
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
15 Mei, 2008

Crap! Wananchi waamue nini? Mwafaka unakubaliwa kwanza kisha mabadiliko ya katiba ndio kura ya maoni. Wito wa kura ya maoni kwa CCM ni hewa maana hawasemi kura ya maoni ya nini? Utakuwa vipi na kura ya maoni bila mwafaka?
 
Mh. Zitto, I wish viongozi wengi wangekuwa na ujasiri kama wako wa kuja kujadili mambo hapa.... ili siye tusiofungamana na siasa za vyama tupate mwangaza zaidi na misimamo ya kivyama kuhusiana na jambo muhimu kama hili...
 
Niliwahi kuandika hivi katika makala yangu kuhusu mwafaka.

Hivyo, CCM imekosea kimantiki kupendekeza kura ya maoni kwa ajili ya mwafaka wake na CUF. CCM walipaswa kwanza kuukubali Mwafaka wakaweka sahihi makubaliano hayo na baadae kufanya mabadiliko yanayostahili katika Katiba ya Zanzibar. Hapa ingeweza kupitisha sheria inayotaka sehemu Fulani Fulani za katiba mabadiliko yake yapitishwe kwa wananchi kupitia kura ya maoni na hivyo kuipeleka katiba hiyo kupigiwa kura. Kimsingi Sio mwafaka unaopaswa kupigiwa kura kama wanavyosema CCM bila kujua, bali ni ama Katiba ya Zanzibar au Mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar.
Kama CCM ilishindwa kuona suala hili la wazi kabisa na la msingi basi haina haki ya kuwa chama tawala, na kwa kweli watakuwa hawana hata hadhi ya kuwa chama cha siasa maana haya ni masuala ya msingi ambayo kiongozi yeyote wa siasa anapaswa kuyajua.
 
Crap! Wananchi waamue nini? Mwafaka unakubaliwa kwanza kisha mabadiliko ya katiba ndio kura ya maoni. Wito wa kura ya maoni kwa CCM ni hewa maana hawasemi kura ya maoni ya nini? Utakuwa vipi na kura ya maoni bila mwafaka?

CRAP CRAP CRAP PWA PWA PWA ....
 
Kwa uzoefu wa miafaka duniani kote kanuni ni hii

Mazungumzo - Mwafaka - Sheria/Katiba - Utekelezaji

au

Mazungumzo - Mwafaka - Sheria/Katiba - Kura ya wananchi - Utekelezaji
Nchi zote zimepita hivi na zote ambazo Ikulu imezitaja hapa hakukuwa na kura ya maoni kuwauliza wananchi ' mnataka mwafaka au hamtaki?'
 
Ndugu Zitto,
Mimi naomba sana kueleimishwa ktk hili..
Ni sababu zipi zinazotunga huu Muafaka wa vyama viwili jinsi ya kutawala nchi zima?..
je unatokana na uchaguzi wa mwaka 2000 au 2205 na kama ndivyo... Je matokeo ya uchaguzi huo yako wapi ambayo yanahallalisha kuundwa kwa Muafaka huu.
Tatizo langu kubwa sio kufikia Muiafaka wa kisiasa kati ya CCM na CUF isipokuwa vipengele vilivyosimamiwa..
Kwa nini iundwe serikali ya Mseto - what if - Jahazi Asili au United People Demokratic (UPDP) cha Fahmi Nassoro kikishinda uchaguzi mwaka 2010 kutakuwepo na utaratibu gani..
Sina wasiwasi na Chadema kwa sababu nyie tayarc mmekwisha jenga muafaka kati yenu na CUF hivyo siwezi kuingilia zaidi isipokuwa kwa chama kama CCM< nashindwa kuelewa sababu inayounda muafaka unaohusu Mustakabali wa nchi nzima kusimamiwa na vyama viwili tu.
Na mwisho, napenda kuuliza what's wrong kuuliza wananchi kwanza? kuna tatizo gani hapa ikiwa CCM wanataka swala hili liamuliwe na wananchi badala ya vyama viwili.. Kama alivyosema JK hili ndilo tatizo hadi sasa hivi kwa nini CUF hawatakli wananchi washirikishwe hali sauti hii ikipelekwa kwa wananchi itawageuka CUF zaidi kwa kutaka kuingia mkataba kisiri...
Je, Muafaka huu una kwa jinsi wanavyotaka CUF una tofauti gani (kwa wananchi) kati yake na ile mikataba ya madini?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom