Muafaka CCM na CUF, pande mbili za shilingi!

MwanaCCM

Senior Member
Feb 5, 2007
110
23
Habari za Masiku wana-JamboForum, soma hii habari kuhusu Mkutano wa CCM na CUF!

Makatibu wakuu CCM, CUF wakutana

MAKATIBU Wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama Cha Wananchi (CUF), leo wanakutana pamoja kuzungumzia mambo mbalimbali kuhusu muafaka katika Hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.

Mara ya mwisho
CUF ilipokutana na waandishi wa habari, ilisema imeridhishwa na hatua iliyofikiwa katika mazungumzo yanayoendelea baina yake na CCM yenye lengo la kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa visiwani Zanzibar.

CUF kilisema mazungumzo hayo yaliyoanza Januari 17, mwaka huu, yanaendelea vizuri na hadi sasa hakuna kiongozi yeyote aliyekwenda nje ya mstari katika mazungumzo hayo.

Kauli hiyo, ilitolewa na Mwenyekiti wa
CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, alipokuwa akisoma maazimio ya kikao cha kawaida cha Baraza Kuu la Uongozi wa chama hicho, kilichofanyika jijini Dar es Salaam, Februari 27-28, mwaka huu.

Akisoma maazimio hayo, Profesa Lipumba alisema kutokana hali hiyo, Baraza Kuu limeiagiza timu ya
CUF katika mazungumzo hayo, kutoa ushirikiano wa hali ya juu ili kuhakikisha kuwa yanafanikiwa.

Wakati
CUF wakisema wamefurahishwa na mazungumzo hayo, kamati ya vyama vya CCM na CUF inayoshughulikia mazungumzo ya muafaka, mwezi uliopita, wajumbe wa vyama hivyo walijichimbia Bagamoyo, lakini habari za ajenda zilizojadiliwa ndani, ziligubikwa na usiri mkubwa.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo, Kingunge Ngomable-Mwiru, zilieleza kikao cha kamati hiyo kilifanyika katika Hoteli ya Oceanic kwa maelewano makubwa.

Wajumbe wa
CCM katika mazungumzo ya Bagamoyo, waliongozwa na Kingunge ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia siasa na uhusiano wa jamii, na CUF waliongozwa na kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed.

Tokea Rais Jakaya Kikwete aingie madarakani, amekuwa akirudia mara kwa mara kwamba mpasuko wa Zanzibar ni ajenda yake kuu. Hata hivyo, siku za hivi karibuni alisema kwamba mazungumzo baina ya vyama hivyo yako katika hali nzuri.

Hivi karibuni Kamati Kuu ya
CCM iliyoketi jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine, ileleza kufurahishwa kwake na ripoti ya maendeleo ya mazungumzo hayo na ikaagiza kuwa kasi ya mazungumzo hayo iendelee.

Haijulikani ni mbinu zipi hasa zinazotumika kuondoa kutokuelewana kwa
CCM na CUF visiwani Zanzibar, ingawa CUF wamekuwa wakipendekeza siku zote kuwa njia ya pekee ya kumaliza mpasuko uliopo ni kuunda serikali itakayoshirikisha watu kutoka vyama vyote viwili.

Hata hivyo, upande wa
CCM visiwani wamekuwa wakipinga kwa nguvu kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa, siku zote wakisema ushindi wao katika uchaguzi unawapa mamlaka ya kisheria ya kuunda serikali
 
CUF wajitoa rasmi kwenye mazungumzo ya muafaka na CCM.

Kwa habari za uhakika ni kuwa chama cha CUF leo kimejitoa rasmi kwenye mazungumzo ya muafaka yaliyokuwa yanaendelea na CCM juu ya mpasuko wa kisiasa kule Zanzibar .

Tamko rasmi la chama hicho limetolewa na mwenyekiti wake Prof> Lipumba leo majira ya saa sita mchana .

Nalitafuta tamko then ntaliweka ila atakayelipata mapema basi aliweke.
 
duh hii kweli ni cracking news.

sasa mambo yataendaje kule kwetu zeni, mama weeeeeeee hatari inazidi kutusogelea, eee jamani tuhurumieni tushachoka jamani na hii hali ya kuwa roho juu kama wagonjwa wa pressure.

nyie CUF mmefikiri mara ngapi? tafadhalini msije kuwaambia dada zetu na kaka zetu waingie barabarani
 
Mbona mi nimesikia kuwa Lipumba kasema wanataka ateuliwe mpatanishi wa kimataifa?

Kasema anaona mazungumzo yamekwama kwani yanatakiwa yaishe tarehe 15 Agosti lakini mpaka sasa hawajafikia muafaka wa masuala ya msingi, hususan kuwepo kwa serikali ya mseto Zanzibar.
 
Makamba na Lipumba wote wamezungumza na BBC leo , sikiliza matangazo ya DIRA ya dunia katika www.bbcswahili.com

Mwanagenzi mpatanishi wa kimataifa ni moja ya masharti ya CUF lakini wameonya hila zilizopo na upande wake Makamba kasema kuwa alimtafuta Katib Mkuu Seif wakutane baada ya ziara yake ya Kigoma, aliporejea Mhe. Seif akawa na shughuli,

There is an interesting feature and live interview with Makamba, listen to www.bbcswahili.com[, then chagua DIRA YA DUNIA/url]
 
Kama hawa waheshimiwa wawili walikuwa wote pale Mlimani wakibukua tena uchumi si warudishe nyuma tofauti zao? Au Lipumba aanze au ajiunge na CCM aache mivutano isio na maana. Mheshimiwa Jaji Warioba wala hakosei anachosema.Wanasiasa wa Tanzania wanahitaji 'shakeup' ya hali ya juu na hii itafanywa na kwa kukumbushwa kupitia masanduku ya kura na wananchi kuwa waungwana kidogo.
 
jamani zanzibar ishaumia na inaendelea kuumia.
zanzibar ni bomu linalosubiri kupasuka, kuweni na huruma jamani.

jitahidini baada ya wale waliouwawa kwa siasa iwe basi, tunaoumia sote si CUF wala si CCM peke yao.

si kama kweli tunapenda kukaa huku milele twatamani kwetu ila hali hii yatukatisha moyo
 
Au Lipumba aanze au ajiunge na CCM aache mivutano isio na maana. Mheshimiwa Jaji Warioba wala hakosei anachosema.

Hivi mtu mwenye akili timamu anaweza akasema Lipumba analeta mivutano isiyo na maana? CCM imetupumbaza akili amna hii kiasi cha kutokuona kwamba inachofanya sasa ni KUITUMIA CUF kwa kisingizio cha mwafaka ambao hawana dhamiri ya kuutekeleza? Chanzo cha zogola Zanzibar na vifo vya ndugu zetu siyo CUF. CUF wana-rect baada ya kuteswa. Nyerere alitufundisha kwamba tumenyanyaswa vya kutosha, tumepuuzwa na kuonewa vya kutosha. CUF wanaposema imetosha kwa nini wapenda amani wasiwaunge mkono?

Matatizo ya Zenji yanatokana na CCM, halafu ikishavuruga inawaita CUF wake mezani kuandaa mwafaka ambao baada ya miaka mitano unakuwa haujajibu hoja za uchaguzi uliopita, halfu unafuata uchaguzi mwingine, hivyo hivyo kwa mzunguko.

Mimi nadhani Lipumba na wenzake wamechelewa kureact, na kama ni uvumilivu wanastahili sifa. CCM wanajua wafanyalo, CUF ndio wanaanza kung'amua baada ya kutumiwa. Jamii ya wapenda haki na amani lazima iwaunge mkono. Jamani tusiwabeze watu wanaoonewa na kunyanyaswa...
 
Afadhali tutaanza kuona mikimiki maana zimepita siku vijana wa kazi hawajafanya mazoezi juu ya viungo vya binadamu wenzao.

CUF tunasubiri songombingo zenu kwa hamu kubwa, vinginevyo mtasahaulika kwenye siasa za bongo.
 
Hivi mtu mwenye akili timamu anaweza akasema Lipumba analeta mivutano isiyo na maana? CCM imetupumbaza akili amna hii kiasi cha kutokuona kwamba inachofanya sasa ni KUITUMIA CUF kwa kisingizio cha mwafaka ambao hawana dhamiri ya kuutekeleza? Chanzo cha zogola Zanzibar na vifo vya ndugu zetu siyo CUF. CUF wana-rect baada ya kuteswa. Nyerere alitufundisha kwamba tumenyanyaswa vya kutosha, tumepuuzwa na kuonewa vya kutosha. CUF wanaposema imetosha kwa nini wapenda amani wasiwaunge mkono?

Matatizo ya Zenji yanatokana na CCM, halafu ikishavuruga inawaita CUF wake mezani kuandaa mwafaka ambao baada ya miaka mitano unakuwa haujajibu hoja za uchaguzi uliopita, halfu unafuata uchaguzi mwingine, hivyo hivyo kwa mzunguko.

Mimi nadhani Lipumba na wenzake wamechelewa kureact, na kama ni uvumilivu wanastahili sifa. CCM wanajua wafanyalo, CUF ndio wanaanza kung'amua baada ya kutumiwa. Jamii ya wapenda haki na amani lazima iwaunge mkono. Jamani tusiwabeze watu wanaoonewa na kunyanyaswa...

Ni mvutano usio na maana kwa sababu wanadanganya wananchi kwamba Tanzania ina siasa zilizo wazi zenye kurutubisha demokrasia. Lakini(behind the scenes) wanakunywa kahawa na pamoja na wanakuwa na good time. Halafu nomba utumie kauli zenye heshima hapa penye forum mimi ni mtu mweye akili timamu, tafwadhali.
 
Si kwamba Mimi ni mwanachama au Shabiki wa CUF,La Hasha!,Lakini Utanzania na Uzalendo wangu unanilazimisha nione kuwa hapa CUF wanazungumza suala la maana,Ukweli wa mambo ni kwamba Waungwana wa Chama TAWALA hawajatoa kipaumbele kwa suala zima la "MUAFAKA",na matokeo yake ni kuwaadhibu Raia wa Pemba wasio na HATIA,Kwa sababu tu!Imani zao kiitikadi haziwakubali na Waungwana wa CCM.

Wana Jambo embu fuatilieni mazungumzo ya Lipumba na BBC na baadaye msikilizeni Mzee Makamba anavyozungumza na Charles Hillary kwenye simu!,Haihitaji shule kubwa kuona kwamba CCM wanaficha kitu!.Makamba anazungumza Juu juu tu!Inawezekana kuwa Seif ana matatizo,lakini Seif hayupo peke yake,anawakilisha kundi kubwa la watu ambalo ni lazima tulisikilize na kulijali kwani nao ni WA-TANZANIA!

Kwa Mtazamo wangu,naona umefika wakati sasa kwa Viongozi wakuu wa vyama hivyo kulizungumza jambo hilo!,na sio kumtuma Makamba(ambaye anawaona CUF wakosaji kabla ya kukaa nao kwenye Meza) na huyu Seif (Kwa hulka yake hakubali kushindwa).naona ni kipindi Muafaka kwa Kikwete na Lipumba kulipa nafasi suala hili!,Haipendezi na wala sio haki,kutafuta suluhisho kwa masuala ya Rwanda na Zimbabwe wakati nyumbani mambo sio Shwari!

Waungwana kwa mara nyingine naomba mumsikilize Makamba anamuona kila mtu anayemuuliza mambo ya Muafaka kama yupo Upande wa CUF,Imebidi Charles abadili Lugha,kwani Swali lake lililoanzia na "sasa" lilimfanya Makamba aanze kufoka!.Sasa kama ndio Viongozi wetu hawa ambao hawataki Challenge,hatuwezi kufikia makubaliano kwa majadiliano,kwa sababu ukimshinda kwa Hoja!,Hatokubali.
 
...hawa wanasiasa ni selfishness tuu inawasumbua na wala hawaangalii maslahi ya wengine ila ni yao tuu,ndio maana kuna umuhimu kweka mbele utaifa kuliko chama chochote cha siasa tukijifunza hilo tutaendelea haraka sana.
 
Tatizo hapa ni kuwa, kuna daraja la watu ambao wanaamini kuwa wameumbwa kutawala wengine. Mpaka sasa nashindwa kuelewa kuwa huo muafaka kuwa wa pande mbili tu, yaani ccm na cuf. hii ndo inaitwa gawanya utawale.

NIMESIKITIKA SANA
 
Ni mvutano usio na maana kwa sababu wanadanganya wananchi kwamba Tanzania ina siasa zilizo wazi zenye kurutubisha demokrasia. Lakini(behind the scenes) wanakunywa kahawa na pamoja na wanakuwa na good time. Halafu nomba utumie kauli zenye heshima hapa penye forum mimi ni mtu mweye akili timamu, tafwadhali.

Richard,

Sijasema huna akili timamu, ila nimehoji kama mtu mwenye akili timamu anaweza kuona Lipumba analeta mivutano usiyo na maana. Yeye ndiye anayevutwa, anapojitetea tunamsakama yeye?

lakini wewe una akili timamu. wala usiwe na wasiwasi, isipokuwa unahitaji kuzizamisha ndani ya matatizo ya Zanzibar ukajua kwamba walio madarakani ndio chanzo na hawana nia ya kumaliza mgogoro. Wanachofanya ni kupoteza muda kwa kuwavuta shati CUF na kuweka mitego mipya ya kuwaibia kura uchaguzi ukifika.

CCM wenyewe wanajua kuwa Karume hakushinda, maana walishaapa kwamna: "Mtashinda nyie, tutatawale sisi." CUF ilipodai daftari la wapiga kura, CCM wakakubali, lakini wakasajili hata vijana kutoka Bara kwa pesa mbuzi. Waulize kina Tarimba na Mkamba wakujulishe dili ilivyokuwa.

Halafu CUF walivyolalamikia uchafuzi wa daftari, wakaletwa wahakiki kutoka Afrika Kusini. Walipoanza kusema daftari lina matatizo SMZ ikawafukuza, uchaguzi ukafanyika, tena chini ya mitutu...tume ikamtangaza iliyetaka awe rais saa 10.00 jioni, sherehe ya kumwapisha ikafanyika kesho yake asubuhi saa tatu ukumbini!

Akili timamu zitawatuma wananchi wenye dhamiri njema kuwaonea huruma na kuwatetea wanaoonewa, ambao hata hivyo wameonyesha uvumilivu katika mchakato mzima. Kama wanakunywa chai na wanyannyasaji wao ndio ukomavu huo, ishara kwamba ambo yakiwa shwari wanaweza kusahau yaliyopita mwafaka ukawapo. Lakini kinachofanyika ni maigizo. Akili timamu zitayaona hayo maigizo na kuyakemea badala ya kuyashabikia! Hata hivyo, wewe unazo, hivyo usiwe na shaka wala usikasirike. Mimi nimehoji kama mwenye nazo anaweza kumlaumu Lipumba kwa uvumilivu huo na kusema analeta mivutano isiyo na maana. Tanzania ya kizazi hiki inahitaji wapambanaji wapya...ingawa watu waoga wanajaribu kuwakatisha tamaa kwa kutokuona wanachokitetea.
 
Inawezekana Maalim Seif katofautiana na Profesa? Maalim yuko wapi? Kama yeye ni kiongozi wa timu ya CUF katika mazungumzo haya nadhani ingefaa azungumze yeye kama alivyodai Makamba. Inawezekana Maalim siku hizi karidhika kwani SMZ inamtunza! Kwa hiyo hana haraka kama wenzie!
 
Inawezekana Maalim Seif katofautiana na Profesa? Maalim yuko wapi? Kama yeye ni kiongozi wa timu ya CUF katika mazungumzo haya nadhani ingefaa azungumze yeye kama alivyodai Makamba. Inawezekana Maalim siku hizi karidhika kwani SMZ inamtunza! Kwa hiyo hana haraka kama wenzie!

Mwanamagenzi,

Acha speculations. Unaijua katiba ya CUF? Msemaji Mkuu ni Mwenyekiti, na kwa sasa ni Lipumba, ndiye ametumwa na chama KUSEMA. Sasa ulitarajia waandishi wakishamsikia Lipumba wamtafute na Seif? Hapana, huko tunakwenda mbali. Nakwambia kwa uhakika, hakuna tofauti yoyote kati yao, bali kati ya msimamo wa CUF na wa CCM.
 
Nimemsikilia Katibu Makamba; hana jipya mambo ni yale yale ya CCM kuwafanya Watanzania wajinga. CCM wanaongoza kwa kuwahadaa watanzania; Mwenyekiti wa CUF anasema CUF wamejitoa; yeye anasema Mazungumzo Yanaendelea...sasa yanaendelea kati ya CCM na chama gani?

Then, hadaa nyingine anasema hakuna mgogoro wa kusuluhisha; Mwenye akili ajiulize walikuwa wanakutana wanajadili nini...kwani ulikuwa mkutano wa kujadili posa ule?

CCM hizi tactics zenu zina mwisho; tena sio mbali wananchi wameshaanza kushtuka.
 
Back
Top Bottom