Muafaka CCM, CHADEMA waiva

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
Tendwa amewaandikia barua viongozi wa vyama hivyo kuwaagiza kuwa wateue wajumbe watakaounda kamati maalumu itakayoshughulikia suala hilo. Vyama hivyo vimejulishwa juu ya utekelezaji wa maelekezo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wa kuwepo timu ya pamoja kujadili na kuutafutia ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro huo.

Barua ya msajili iliyoandikwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama na Dk Slaa wa Chadema zilipokelewa katika ofisi za vyama hivyo Agosti 17, mwaka huu.

Kutokana na taarifa hiyo ya Tendwa, Chadema tayari imeteua wajumbe wanane watakaongozwa na Dk Slaa katika vikao vya majadiliano na wenzao kutoka CCM, wengine katika timu hiyo ni wajumbe wa kamati kuu, Mabere Marando, Tundu Lissu na Lazaro Massay ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu na mwenyekiti wa mameya na wenyeviti wa halmashauri zinazoongozwa na Chadema.

Wajumbe wengine ni Mbunge wa Arusha, Godbless Lema, Mkurugenzi wa Halmashauri na Bunge, John Mrema, katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa na Diwani wa Kata ya Levolosi ambaye pekee ndiye hakusaini muafaka uliosababisha wenzake kutimuliwa, Ephata Nanyaro.

Dk Slaa alikiri kupokea barua ya msajili iliyowajulisha uwepo wa kamati vya vyama hivyo kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa umeya Arusha na kuteua wajumbe watakaoshiriki kutoka chama chake.

Kwa upande wa CCM, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nnape Nnauye, alikataa kuzungumzia suala hilo akisema kuwa hayo ni majungu. "Hayo ni majungu," alisema Nnauye alipotaka kujua kama Tendwa amethibitisha kwa kinywa chake kuhusu muafaka huo.

Nnauye ambaye amekuwa mmoja wa viongozi wa CCM walio mstari wa mbele kukisafisha chama chake dhidi ya viongozi wenye kashfa za kifisadi, alisema atakuwa tayari kujibu hoja iliyotoka moja kwa moja kinywani mwa Tendwa na siyo maandishi.

Akijibu maswali ya papo kwa papo bungeni hivi karibuni, Waziri Mkuu aliwaruka viongozi wa Chadema waliokuwa wameeleza kuwa kamati ya usuluhishi katika mgogoro wa Arusha itaundwa na kwamba, viongozi wa chama hicho na Pinda walishakubaliana.

Source: Mwananchi
 
ccm waoga kama kunguru, hayo majina ya timu ya cdm yamewatisha.
 
chadema ni chama makini,sidhani kama kinataka kuolewa kama cuf ila kinataka kumaliza tatizo la mgogoro wa arusha.kama ni kweli hapo ndipo mtajua undumilakuwili na uwongo wa waziri mkuu.
pili kama ni ndoa ccm ilishalazimisha na mtoto wa shule(madiwani) kilichotokea mmekiona.
hii ya sasa labda magamba yatake bwana tofauti na hapo mtakuwa mashahidi wa yatakayotokea arusha.
mnajua ni kwanini azimio la kiutu na maadili lilianzia arusha?
arusha ni geneva ya africa na hilo litajidhihirisha kwenye hili.
naelekea church.
 
Chadema wameshamalza kazi yao kutokana na kanun za katba yao. Inakuwa vp tena Tendwa anataka wakae pamoja!. Wanataka cdm watengue uamuz wao?. Madiwan si wamefungua kes mahakaman?. Naona kama Tendwa amekosa kaz ya Kufanya.
 
wachangiajina watanzania kwa ujumla wanapaswa kutambua kuwa migogoro mingi ya kisiasa haiwezi kupata suluhu ya kweli kwa watu kukimbilia mahakamani hasa kwa aina ya uhuru wa mahakama zetu ambazo zimekuwa zikitiliwa shaka kukibeba chama tawala. naunga mkono pande hizi mbili kutafuta suluhu kwa kwa njia ya kukaa pamoja mezani ajili ya kuharakisha maendeleo katika manispaa ya arusha na kuleta utengamano kati ya hizi pande 2 za vyama.
 
Naomba msome tena hizo commentz za CHADEMA & CCM. Huwezi kuongoza watu bila kuwaanmbia unafanya nini! Watu wanataka wajue una mipango gani, umefikia wapi. Hapa, CHADEMA wanaonekana kufaya vyema kwa kusema nini wanafanya, Katibu mkuu wao Dr Slaa anakiri kuwa kuna jitihada zinafanywa ili kusuluhisha mgogoro wa Arusha.

Kama kawaida CCM wanakanusha! Nape anaenda mbali zaidi na kusema hizi habari niz uzushi! Sasa hata kwenye mambo ambayo yako so obvious wanakataa, je, wananchi wawaamini kwa lipi? Kama Nape anatakataa kutoa taarifa umma ukizusha watalalamika? Kwa zama hizi za science & technology ni vigumu sana kuficha habari, na Nape & wenzake wanatakiwa wajue kama wao ccm hawataengea basi watu wengine wataongea but tena at the expense ya ccm! sikio la kufa...!

Dk Slaa alikiri kupokea barua ya msajili iliyowajulisha uwepo wa kamati vya vyama hivyo kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa umeya Arusha na kuteua wajumbe watakaoshiriki kutoka chama chake.

Kwa upande wa CCM, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nnape Nnauye, alikataa kuzungumzia suala hilo akisema kuwa hayo ni majungu. “Hayo ni majungu,” alisema Nnauye alipotaka kujua kama Tendwa amethibitisha kwa kinywa chake kuhusu muafaka huo.
 
Naomba msome tena hizo commentz za CHADEMA & CCM. Huwezi kuongoza watu bila kuwaanmbia unafanya nini! Watu wanataka wajue una mipango gani, umefikia wapi. Hapa, CHADEMA wanaonekana kufaya vyema kwa kusema nini wanafanya, Katibu mkuu wao Dr Slaa anakiri kuwa kuna jitihada zinafanywa ili kusuluhisha mgogoro wa Arusha.

Kama kawaida CCM wanakanusha! Nape anaenda mbali zaidi na kusema hizi habari niz uzushi! Sasa hata kwenye mambo ambayo yako so obvious wanakataa, je, wananchi wawaamini kwa lipi? Kama Nape anatakataa kutoa taarifa umma ukizusha watalalamika? Kwa zama hizi za science & technology ni vigumu sana kuficha habari, na Nape & wenzake wanatakiwa wajue kama wao ccm hawataengea basi watu wengine wataongea but tena at the expense ya ccm! sikio la kufa...!
Nape anaposema hayo ni majungu ana maana gani kama si ujinga ni nini anataka kujifanya yeye anajua sana which is not true.

Unajua CCM bado wanaendesha chama kwa staili ya ujima wanafikiri kukataa na kuficha habari ndio uongozi bora wakati siasa za sasa zinatakiwa ziwe za uwazi achlia mbali ukweli ambao hawauwezi. Bado wanastaili ya mimi sio msemaji wakati wenzao wanasambaza habari hata kupitia Facebook. Kwa kufanya hivyo viongozi wanazidi kujitenga na wanachama wao hasa vijana wanaotaka kujua chama chao kina msimamo gani kwa jambo fulani, mwisho wa siku wanalalamika kukimbiwa na vijana kumbe ni uongozi wao wa kizee wanaudhi sana huwa hawajui tu.
 
Am confused, labda waniambie hawaendi kujadili suala lililo mahakamani.
 
wacha tuvute subira tusikie nini kitasemwa,wasiwasi wangu sidhani kama watakubaliana.
 
Kwa hiyo taratibu za harusi ndio zimeishaanza. Haya ngoja tusubiri kama wamepeana barua za posa ni vizuri
 
ccm waoga kama kunguru, hayo majina ya timu ya cdm yamewatisha.

Jogi na wenzako,

KWANZA NI VIZURI SANA KULIJUA TATIZO LA ARUSHA BILA USHABIKI WA KISIASA. HIVI NINI SABABU YA CCM NA CHADEMA KUKAA MEZANI HASA KWA VIONGOZI WA KITAIFA.. UGOMVI ULIOPO NI KATI YA CHADEMA NA MADIWANI WAKE WA ARUSHA....CCM INAINGIAJE HAPA?

NANI ASIYEJUA KUWA MKAKATI WA VIONGOZI WA CHADEMA TAIFA NI KUTUMIA MGOGORO HUU WA ARUSHA KUMALIZA KESI INAYOWAKABILI, HASA BAADA YA KUONA KUWA IMEWAKALIA VIBAYA? HILI LAO CCM HATUMO.

TUNAJUA MEYA KACHAGULIWA KIHALALI NA MANISPAA INAENDELEA KUJENGWA, IKIZINGATIWA KUWA ILANI INAYOTEKELEZWA NI YETU , HATUNA MUDA WA KUJADILI WALA KULUMBANA KWA MIGOGORO ISIYOTUHUSU...TUNASUBIRI HIZO SIKU 30 ZA WATANI ZANGU...

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE.
 
Jogi na wenzako,

KWANZA NI VIZURI SANA KULIJUA TATIZO LA ARUSHA BILA USHABIKI WA KISIASA. HIVI NINI SABABU YA CCM NA CHADEMA KUKAA MEZANI HASA KWA VIONGOZI WA KITAIFA.. UGOMVI ULIOPO NI KATI YA CHADEMA NA MADIWANI WAKE WA ARUSHA....CCM INAINGIAJE HAPA?

NANI ASIYEJUA KUWA MKAKATI WA VIONGOZI WA CHADEMA TAIFA NI KUTUMIA MGOGORO HUU WA ARUSHA KUMALIZA KESI INAYOWAKABILI, HASA BAADA YA KUONA KUWA IMEWAKALIA VIBAYA? HILI LAO CCM HATUMO.

TUNAJUA MEYA KACHAGULIWA KIHALALI NA MANISPAA INAENDELEA KUJENGWA, IKIZINGATIWA KUWA ILANI INAYOTEKELEZWA NI YETU , HATUNA MUDA WA KUJADILI WALA KULUMBANA KWA MIGOGORO ISIYOTUHUSU...TUNASUBIRI HIZO SIKU 30 ZA WATANI ZANGU...

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE.

Baadhi ya maneno uliyatumia jana kwenye mdahalo, nina imani ni wewe.

Mmoja kati ya wafuasi wako na hasa tulioamini kuwa utatuletea ccm "mpya" anasema waziwazi kuwa katikati ya lawama nyingi dhidi ya ccm ulitakiwa kuwa smart sana. Hilo umeshindwa na unakaribia kuburuzwa na elimu ya cdm kuhusu mambo ya msingi kitaifa inayopenya mioyoni mwa watanzania siku hadi siku.

Take my word, usipoelewa mwl alimaanisha nn kuhusu ccm imara, utajikuta one day ukiwa chama mbadala cha siasa.
 
Jogi na wenzako,

KWANZA NI VIZURI SANA KULIJUA TATIZO LA ARUSHA BILA USHABIKI WA KISIASA. HIVI NINI SABABU YA CCM NA CHADEMA KUKAA MEZANI HASA KWA VIONGOZI WA KITAIFA.. UGOMVI ULIOPO NI KATI YA CHADEMA NA MADIWANI WAKE WA ARUSHA....CCM INAINGIAJE HAPA?

NANI ASIYEJUA KUWA MKAKATI WA VIONGOZI WA CHADEMA TAIFA NI KUTUMIA MGOGORO HUU WA ARUSHA KUMALIZA KESI INAYOWAKABILI, HASA BAADA YA KUONA KUWA IMEWAKALIA VIBAYA? HILI LAO CCM HATUMO.

TUNAJUA MEYA KACHAGULIWA KIHALALI NA MANISPAA INAENDELEA KUJENGWA, IKIZINGATIWA KUWA ILANI INAYOTEKELEZWA NI YETU , HATUNA MUDA WA KUJADILI WALA KULUMBANA KWA MIGOGORO ISIYOTUHUSU...TUNASUBIRI HIZO SIKU 30 ZA WATANI ZANGU...

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE.


Ni kweli unavyosema kuwa CCM haihusiki kama Chadema isivyohusika na uvuaji wa magamba, lakini kwa hili jipya la Mkuchika hata Chadema haihusiki imeshatoa uamuzi wake kuwavua uanachama mpira sasa uko kwa serikali na mahakama, ila ulikuwa huna haja ya kusema zile barua ni majungu, hata kama ulikuwa hujui kama kuna barua zilizotumwa ilikuwa busara kusema huna taarifa lakini kusema ni majungu inaonesha tayari ulikuwa unajua kilichomo.
Kwa upande wa CCM, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nnape Nnauye, alikataa kuzungumzia suala hilo akisema kuwa hayo ni majungu. "Hayo ni majungu,"
 
Nape,

Naona unaishi ahera.

i) kwa kauli hii ni dhahiri kuwa hujui mgogoro ulioko ni arusha unahusu nini. Chadema haina mgogoro na madiwani wake kwani iliisha kuwafukuza uanachama. Ni mtu asiyejua taratibu za sheria tu ndiye anaweza kutoa kauli kama ya kwako, au vinginevyo una agenda ambayo ni vyema ukaiweka hadharani

ii) Kesi cr/c. 5/2011 iliyoko High Court ya Arusha haina uhusiano na Madiwani bali ni kesi ya "unlawfull Assembly". Kesi iliyofunguliwa na Madiwani 5 ambayo hadi sasa sina namba yake inahusu "madiwani watano kuiomba Mahakama iwarudishie Uanachama wao". Hivyo hata wao wanajua kuwa wamevuliwa uanachama. Upotoshwaji wa aina hii ni wa ajabu, lakini tunaelewa kwa magamba hakuna lisilowezekana.

Jogi na wenzako,

KWANZA NI VIZURI SANA KULIJUA TATIZO LA ARUSHA BILA USHABIKI WA KISIASA. HIVI NINI SABABU YA CCM NA CHADEMA KUKAA MEZANI HASA KWA VIONGOZI WA KITAIFA.. UGOMVI ULIOPO NI KATI YA CHADEMA NA MADIWANI WAKE WA ARUSHA....CCM INAINGIAJE HAPA?

NANI ASIYEJUA KUWA MKAKATI WA VIONGOZI WA CHADEMA TAIFA NI KUTUMIA MGOGORO HUU WA ARUSHA KUMALIZA KESI INAYOWAKABILI, HASA BAADA YA KUONA KUWA IMEWAKALIA VIBAYA? HILI LAO CCM HATUMO.

TUNAJUA MEYA KACHAGULIWA KIHALALI NA MANISPAA INAENDELEA KUJENGWA, IKIZINGATIWA KUWA ILANI INAYOTEKELEZWA NI YETU , HATUNA MUDA WA KUJADILI WALA KULUMBANA KWA MIGOGORO ISIYOTUHUSU...TUNASUBIRI HIZO SIKU 30 ZA WATANI ZANGU...

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE.
 
Nape,

Naona unaishi ahera.

i) kwa kauli hii ni dhahiri kuwa hujui mgogoro ulioko ni arusha unahusu nini. Chadema haina mgogoro na madiwani wake kwani iliisha kuwafukuza uanachama. Ni mtu asiyejua taratibu za sheria tu ndiye anaweza kutoa kauli kama ya kwako, au vinginevyo una agenda ambayo ni vyema ukaiweka hadharani

ii) Kesi cr/c. 5/2011 iliyoko High Court ya Arusha haina uhusiano na Madiwani bali ni kesi ya "unlawfull Assembly". Kesi iliyofunguliwa na Madiwani 5 ambayo hadi sasa sina namba yake inahusu "madiwani watano kuiomba Mahakama iwarudishie Uanachama wao". Hivyo hata wao wanajua kuwa wamevuliwa uanachama. Upotoshwaji wa aina hii ni wa ajabu, lakini tunaelewa kwa magamba hakuna lisilowezekana.


Mimi sijaelewa hapa, maelezo ya Nape ni kuwa mgogoro kama upo basi unahusisha, CDM, Mahakama, Madiwani waliokuwa wa CDM na mkurugenzi sasa hapa CCM inaingia vipi? Ulipotakiwa kujibu ulipaswa na wewe uache dharau na uoneshe CCM inahusika vipi. Hayo majadiliano kwa nini yawahusishe CCM wakati wao hawahusiki kwenye huo mgogoro?
 
Hakika uteuzi ndani ya CHADEMA ni kali ajabu; well reasoned!!!!!!!!!! CHADEMA vichwaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mimi sijaelewa hapa, maelezo ya Nape ni kuwa mgogoro kama upo basi unahusisha, CDM, Mahakama, Madiwani waliokuwa wa CDM na mkurugenzi sasa hapa CCM inaingia vipi? Ulipotakiwa kujibu ulipaswa na wewe uache dharau na uoneshe CCM inahusika vipi. Hayo majadiliano kwa nini yawahusishe CCM wakati wao hawahusiki kwenye huo mgogoro?

kuna barua kaandika waziri Mkuchika kwenda kwa mkurugenzi wa halimashauri ya ARUSHA kuwatambua madiwani mpaka kesi itakapoishi mahakamani?

Je Mkuchika ni hakimu au jaji? au msemaji wa mahakama? mahakama ndiyo inapaswa kutoa amri sio na sio mkuchika kama waziri wa serikali ya CCM kama bado unatafuta ccm inausika vipi na mgogoro wa ARUSHA basi huna macho,pua, ngozi wala ubongo.
tumia fahamu zako


TUMEWEZA KUTHUBUTU TUNAENDELEA KUANGUKIA PUA (regea chenge na lowasa bado ni gamba) ccm
 
Jogi na wenzako,

KWANZA NI VIZURI SANA KULIJUA TATIZO LA ARUSHA BILA USHABIKI WA KISIASA. HIVI NINI SABABU YA CCM NA CHADEMA KUKAA MEZANI HASA KWA VIONGOZI WA KITAIFA.. UGOMVI ULIOPO NI KATI YA CHADEMA NA MADIWANI WAKE WA ARUSHA....CCM INAINGIAJE HAPA?

NANI ASIYEJUA KUWA MKAKATI WA VIONGOZI WA CHADEMA TAIFA NI KUTUMIA MGOGORO HUU WA ARUSHA KUMALIZA KESI INAYOWAKABILI, HASA BAADA YA KUONA KUWA IMEWAKALIA VIBAYA? HILI LAO CCM HATUMO.

TUNAJUA MEYA KACHAGULIWA KIHALALI NA MANISPAA INAENDELEA KUJENGWA, IKIZINGATIWA KUWA ILANI INAYOTEKELEZWA NI YETU , HATUNA MUDA WA KUJADILI WALA KULUMBANA KWA MIGOGORO ISIYOTUHUSU...TUNASUBIRI HIZO SIKU 30 ZA WATANI ZANGU...

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE.

Mheshimiwa Nape mwana wa Nnauye,

Mgogo wa Arusha kwa vyovyote vile ccm inahusika, Meya anayesababisha ugomvi ni wa ccm, Mkuchika aliyewatambua wale madiwani ni wa ccm.

Ndugu yangu nilidhani utakisaidia chama ulipoteuliwa but naona kama wewe ndo utakimalizia kabisa. Badala ya kujifanya wababe eti hakuna mgogoro ni afadhali uukubali ukweli uliopo kisha sote kama watanzania tutafute njia.

Ukaidi huu utaiangusha ccm na mbaya zaidi utamwaga damu ya watanzania zaidi ya iliyokwishamwagwa hadi sasa kabla ya anguko lenyewe.
 
Nape,

Naona unaishi ahera.

i) kwa kauli hii ni dhahiri kuwa hujui mgogoro ulioko ni arusha unahusu nini. Chadema haina mgogoro na madiwani wake kwani iliisha kuwafukuza uanachama. Ni mtu asiyejua taratibu za sheria tu ndiye anaweza kutoa kauli kama ya kwako, au vinginevyo una agenda ambayo ni vyema ukaiweka hadharani

ii) Kesi cr/c. 5/2011 iliyoko High Court ya Arusha haina uhusiano na Madiwani bali ni kesi ya "unlawfull Assembly". Kesi iliyofunguliwa na Madiwani 5 ambayo hadi sasa sina namba yake inahusu "madiwani watano kuiomba Mahakama iwarudishie Uanachama wao". Hivyo hata wao wanajua kuwa wamevuliwa uanachama. Upotoshwaji wa aina hii ni wa ajabu, lakini tunaelewa kwa magamba hakuna lisilowezekana.

Dr. Slaa hawa hawawezi kukaa na CDM kujadili Mgogoro wa Arusha maana waliutengeneza makusudi lakini la pili hawana mtu yeyote anayeweza kukaa mezani kujadili kitu chochote cha maana. Wewe kwa akili yako unaona Mtu kama Nape anaupeo wowote wa kufikiri kujadili jambo lolote la maana badala ya kuishi kwa maagizo ya kutumwa na kuimba beti za nyimbo alizo kalilishwa!

CCM yenyewe ina migogoro ndani ya chama chao ambayo huo wa Arusha ni mdogo sana lakini wameshindwa kuijadili na kuimaliza leo mwaka karibia wa nne CCM inayumba kwa migogoro ndani ya chama, Septemba hii inakwenda kufa baada ya NEC-CCM; Watu ambao wanaishi kwa migogoro kiasi hicho na ambao hata migogoro ya ndani ya chama imewashinda kutatuwa na wapo njiani kufa kwa migogoro ndani ya chama chao, mnategemea mkaenao kuongea nini?

Mimi nashauri CDM iachane na CCM mmeonyesha nia yenu nzuri na Jamii imeona, kama hawataki achaneni nao siku zote vyama vilivyoota ukurutu vinaji-behave hivyo, na mara zote hiyo uwa ni ishara ya sikio la kufa, ni bora wafanye jambo lolote kwa kulazimisha na bila idhini ya Umma kama walivyozoea lakini CDM hisibembeleze kuongea nao, CDM has nothing to loose sasa mbele ya CCM, hasiyeona na kujua hilo ana akili kama ya Qadhaffi! Hata Qadhaffi one month past alisema atapiga Ulaya kama nzige, tulisubiri tuone hao nzige wa Libya wakishambulia Ulaya, leo anaishi kwenye maandaki, kwa hiyo husishangae maneno ya Nape kama kasuku!

The end is coming soon, Watanzania wameshaamua acha CCM iendelee kulala.
 
Nape,

Naona unaishi ahera.

i) kwa kauli hii ni dhahiri kuwa hujui mgogoro ulioko ni arusha unahusu nini. Chadema haina mgogoro na madiwani wake kwani iliisha kuwafukuza uanachama. Ni mtu asiyejua taratibu za sheria tu ndiye anaweza kutoa kauli kama ya kwako, au vinginevyo una agenda ambayo ni vyema ukaiweka hadharani

ii) Kesi cr/c. 5/2011 iliyoko High Court ya Arusha haina uhusiano na Madiwani bali ni kesi ya "unlawfull Assembly". Kesi iliyofunguliwa na Madiwani 5 ambayo hadi sasa sina namba yake inahusu "madiwani watano kuiomba Mahakama iwarudishie Uanachama wao". Hivyo hata wao wanajua kuwa wamevuliwa uanachama. Upotoshwaji wa aina hii ni wa ajabu, lakini tunaelewa kwa magamba hakuna lisilowezekana.
Asante Dr. kwa ufafanuzi,

Kama kesi iliyofunguliwa na madiwani ni kuomba kurudishiwa uanachama kwanini Mkuchika awatambue hata kabla ya mahakama kutoa hukumu nilitegemea aseme anasubiri uamuzi wa mahakama.

Kitu kingine kinachonichanganya nasikia madiwani wamekata rufaa kwenye Baraza kuu la chama hawaoni watasababisha mgongano wa maamuzi, mfano mahakama ikubaliane na uamuzi wa kamati kuu ya kuvuliwa uanachama baadae Baraza kuu liwarudishie and vice versa, mahakama na serikali zitakuwa upande gani. Nafikiri huu ni mwendelezo wa serikali kuingilia mihimili mingine ya utawala, i think sooner than later ukweli utajulikana who is behind the scene, lakini mimi kwa upande mwingine nafurahi haya kutokea ili wananchi wazidi kuielewa serikali yao vizuri ili wakati wa kutoa maamuzi wasije kujutia uamuzi wao..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom