Muafaka bila kugusa Mapinduzi 1964

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Najaribu kujiuliza kama kweli muafaka, mapatano na umoja wa Zanzibar na hatima ya Taifa letu vinaweza kufikiwa bila kuzungumzia kwa uwazi na ukweli matukio yaliyosababisha mapinduzi ya 1964, matukio yenyewe ya mapinduzi na kilichotokea usiku ule wa damu, machozi, na machungu; usiku uliozaa Zanzibar ya leo na matukio yaliyotokea baada ya mapinduzi. Ule usiku wa kukumbukwa.

Haya madai ya Uhizbu n.k yanatulazimisha kuangalia kama kweli muafaka unaweza kuwa wa kina, wa kweli, na wenye kuleta hatima ya umoja na mshikamano kwa watu wa Unguja na Pemba pasipo kugusia tukio ambalo naamini ni kiini na mzizi wa mgogoro wa leo?

Je mtu aweza kuukausha mti kwa kukata majani na matawi tu bila kung'oa mizizi?

Mjadala is open.
 
Mwanakijiji,
Mapinduzi has nothing to do with this! isipokuwa MUUNGANO wenyewe.. serikali iliyojengwa wakati wa Muungano ilikuwa sii kabisa, hadi pale kuundwa kwa CCM na kuvunja vyama vyote ndio sababu kubwa...
Sasa ni wakati muafaka wa kulitazama upya swala la kuzitambua serikali mbili yaani ya Bara na Visiwani ktk Muungano huu..
Trust me hakuna mtu anaweza kunambia hapa itakuwa vipi ikiwa Muafaka umepitishwa kisha CUF wakashinda uchaguzi mkuu... Rais akitoka CUF, Je, bara pia itabidi tuwe na waziri kiongozi> au nini itakuwa nafasi ya Waziri mkuu bara! kwa sababu hadi sasa hivi Bara inatambulika ktk maandishi na maneno ya mtaani lakini hakuna nchi inayojulikana kama Tanzania Bara kikatiba. Zanzibar ipo kwa sababu wanayo serikali yao hivyo swala sio CUF na CCM isipokuwa kutambua ardhi kwanza kisha mnajenga Uongozi wa hizo nchi tofauti na kuunda uongozi bila kutambua Muungano wa nchi hizi mbili.
 
Yaliyotokea siku ile:
kujiandaa kufyatua risasi
Preparing_to_fire_on_prisoners_3.jpg


Baada ya kufyatuliwa
Prisoners_dead_3_.jpg.jpg


kupelekwa kaburini
Truck_trasporting_bodies2.jpg


Kaburi la wengi

Mass_grave_4.jpg

Hiyo ni sehemu tu ya picha chache ya kile kilichotokea. Machungu ya Zanzibar hayakuanzia kwenye Muungano. Yalifikia kilele usiku ule wa Januari 12, 1964.
 
Mwanakijiji,
Ningeomba maelezo zaidi ya habari hii kwa sababu nataka kufuatilia swala hili vizuri hasa hiyo tarehe ya mauaji haya..
Ikiwa tunaambiwa Mapinduzi yalifanywa na wahuni kina Okello ambaye alikuwa na kazi ya utumwa kupasua mawe kule Pemba na makuli wa bandarini waliochoka hawa watu waliweza vipi ku mobilize gari, sehemu ya kuzikia hawa watu na kadhalika...Picha hizi zinaonyesha Authority kubwa zaidi ya wahuni..
Kumbuka pia kulingana na habari nilizozipata, Mapinduzi haya chini ya Okello na kina Babu yalidumu mwezi mmoja tu kabla ASP hawajachukua nchi.
 
Mwanakijiji,
Ningeomba maelezo zaidi ya habari hii kwa sababu nataka kufuatilia swala hili vizuri hasa hiyo tarehe ya mauaji haya..
Ikiwa tunaambiwa Mapinduzi yalifanywa na wahuni kina Okello ambaye alikuwa na kazi ya utumwa kupasua mawe kule Pemba na makuli wa bandarini waliochoka hawa watu waliweza vipi ku mobilize gari, sehemu ya kuzikia hawa watu na kadhalika...Picha hizi zinaonyesha Authority kubwa zaidi ya wahuni..
Kumbuka pia kulingana na habari nilizozipata, Mapinduzi haya chini ya Okello na kina Babu yalidumu mwezi mmoja tu kabla ASP hawajachukua nchi.

Mkandara ndio maana kuna haja ya kuelewa nini kilitokea; hebu jiweke upande wa watoto wa hao waliorundikwa namna hiyo... fikiria mnaamna asubuhi harufu ya damu na sauti ya kilio... uchungu ule wa siku ile unaweza kukoma kwa siku moja?
 
Inaelekea yaliyotokea usiku ule ni tofauti sana na mambo tunayoyafahamu kutokana na jinsi tulivyofubdishwa.
 
Navyofahamu mimi mauaji mengi yalifanywa na Karume baada ya kupata upinzani moja kwa moja kisiasa kama inavyotokea leo huko Unguja na Pemba.
Lakini napoona picha kama hizi za mauaji siku ya Mapinduzi najaribu kuelewa nini thamani ya Mapinduzi na what a simple mistake ya kumweka Sultan kunavyoweza kugharimu maisha ya watu..hapo hapo najiuliza ikiwa kweli hivi hawa kina Okello walipata wapi uwezo huo wamagari, kuchimba wakaburi wakati tunaambiwa walikuwa walalahoi...
Je, isije kuwa ni ndani ya utawala Karume nje kabisa ya siku ya Mapinduzi kwani navyojua mimi Karume hakuwepo Unguja wala Pemba usiku huo..
 
Inaonyesha sasa tunaelekea kuleee tunako kutaka 'mimba haijifichi'
mmkjj mungu akuweke
 
Hili la mapinduzi tutakuja kulizungumza tu kama Mitchell Report ilivyofuatilia suala la Northern Island, kama Tutu na T & R Commission, kama Nuremberg Trial, kama mahakama za Gacaca na ICTR n.k

Sasa hivi hatujakaa chini kuzungumza lakini siku moja kama si sisi basi watoto wetu au watoto wa watoto wetu watakuja kulizungumza.

Kumuondoa Sultani tu haiwezi kuwa sababu ya kuhalalisha unyama. Kama Sultani alikuwa mnyama hivyo je leo kuwatendea watu wa Pemba jinsi wanavyotendewa siyo unyama? Kwanini Unyama wa Sultani ni mbaya sana lakini huu wa kizazi chetu unavumilika?
 
..Wapemba hubezwa na Waunguja kwamba hawakushiriki mapinduzi.

..Tena nasikia kwamba Pemba walipewa taarifa tu kwamba Sultani amepinduliwa.

..Sasa haya manunguniko ya Wapemba kuhusu Mapinduzi yanatoka wapi? May be there is something we dont know.

..Kwa mtizamo wangu wako Waunguja walioathirika vibaya na Mapinduzi ambao wamejibanza kwenye grievences za Wapemba za kutengwa na serikali ya Mapinduzi.

..Wenye matatizo na Mapinduzi wakae kando watoe malalamiko yao.

..Wapemba nao wakae kando na CUF yao watoe madukuduku yao.

NB:

..Truth Commision ni sawa lakini isiishie kuchunguza madhambi yalitokea siku na baada ya Mapinduzi tu. Sultani naye lazima achunguzwe.

..Kuna dukuduku lilolosababisha Mapinduzi na umwagaji damu uliotokea. Sasa ni lazima dukuduku hilo liwe addressed wakati tuna-address umwagaji damu siku ya Mapinduzi.
 
Mkuu Mwanakijiji,

Hayo makaburi ya halaiki ulotuonesha katika picha yako wapi katika Zanzibar ya leo? Yaani waweza kututajia angalao jina la kijiji au mtaa au sehemu yanakopatikana makaburi hayo? Nauliza maana ninao mshangao mkubwa kuhusu jinsi jambo kama hili linavyoweza kufichika tusisikie japo tetesi miaka yote hii (kabla sijajiita "kilaza", maana nimesoma historia hadi university, na nimebahatika kutembelea maeneo rasmi na yasiyo rasmi ya kihistoria, lakini kuhusu yalipo makaburi haya sijapata kusikia japo fununu!) Nafahamu kuwa watu wengi waliuawa wakati wa mapinduzi ya Zanzibar, na hesabu zilikuwa zinatofautiana kati ya duru za Okello na zile za CIA na vyombo vya habari vya kimagharibi. "Field Marshal" John Okello alikuwa na tabia ya kutaja idadi ya kutisha kwa kila kitu alichotangaza, haieleweki ni kwa kutojua thamani halisi ya namba hizo au ni sehemu ya "mkwala" wake. Mfano alipotangaza redioni kuhusu kupinduliwa kwa sultani, alidai jeshi lake lina wapiganaji milioni 99! Hiki chenyewe kilikuwa kituko maana Tanganyika wakati huo ilikuwa na watu wasiozidi milioni 12. Duru nyingine zinakadiria wapiganaji waliofanikisha mapinduzi hawakuzidi watu 300. Kuhusu waliouawa, Okello alidai kwa usiku wa mapinduzi tu waliua watu zaidi ya elfu mia moja, na hawaoni shida kuua wengine ikibidi! Alitishia pia kwamba jeshi lake liko tayari kutoa adhabu mara 888 kwa yeyote atakayepinga mapinduzi hayo! Alikuwa na mikwala sana huyu jamaa! Lakini kumbukumbu nyingine zilizopo zinaonesha hawakuuawa wengi kiasi hicho siku ya mapinduzi, mauaji mengi yalifanywa na makundi ya watu dhidi ya waliokuwa na chuki nao (hata zisizokuwa za kisiasa), na hii ilikuwa rahisi kwa kuwa nchi haikuwa tena na vyombo vya kulinda usalama, kulikuwa na "lawlessness" au tuiite "anarchy", fujo tupu. Hapo ndipo watu walipovamiwa majumbani mwao na kukatwa vichwa mbele ya wake na watoto wao, wanawake walibakwa, na uporaji ulikuwa wa kutisha. Hakuwepo mtu mwenye uwezo au nafasi ya kuratibu mauaji ya halaiki ama hata hayo maziko ya halaiki. Okello mwenyewe alishindwa kutuliza au kudhibiti fujo hizi, na kuna wakati alitangaza kwenye radio kuwa atakayekamatwa anafanya uporaji angeuawa, lakini bado haikusaidia. Kilichosaidia kutuliza fujo zile ilikuwa ni jeshi la polisi kutoka Tanganyika ambalo lilitumwa huko, na wakafanikiwa kunyamazisha.

Kumbukumbu pekee katika picha inayoashiria kuwepo kwa mauaji yaliyoratibiwa ya halaiki ni filamu iliyotengenezwa na mtengeneza filamu wa kiitaliano, na kuanza kuoneshwa kwenye mwaka wa 1966 kama documentary. Huyo mtengenezaji alidai amepiga picha hizo akiwa kwenye helikopta wakati mapinduzi yakiwa yanaendelea, na ukiiangalia filamu hiyo utaona watu wanavyopangwa katika mstari, kupigwa risasi, kupakiwa katika malori na kupelekwa kwenye shimo kubwa lililokwisha kuchimbwa tayari kwa maziko ya jumla. Yeyote anayetazama filamu hiyo atashangaa jinsi mtengenezaji alivyoweza kuwafuatilia wauaji hao wenye bunduki kwa karibu kiasi hicho, wanayotekeleza mauaji hatua kwa hatua bila yeye kudhurika! Au labda alikuwa mmoja wao? Katika eneo jingine kwenye documentary hiyo amewafuatilia watu waliokimbilia pwani ili wakapande mitumbwi watorokee bara, kumbe wanafuatwa kwa nyuma na "wanamapinduzi", kufika pwani wakamiminiwa risasi wote, kisha wauaji wakachimba shimo mchangani na kuwafukia kwa jumla. Nilijiuliza huyu mzungu alikuwa na helikopta ngapi, na alijiaminije kuwa asingetunguliwa? Mauaji ya halaiki ya Rwanda yalifanyika katika kipindi ambacho teknolojia ilikuwa kubwa kuliko mwaka 1964, lakini hakuna documentary yoyote ya filamu inayoonesha jinsi yanavyofanyika, ziko zinazoonesha matokeo ya mauaji hayo (maiti zilizolundikana kwenye majengo, barabarani, mtoni nk) na wakimbizi wanaokimbia vita wanaosimulia yaliyowapata. Na hayo makaburi ya halaiki ukienda Rwanda hata leo utaoneshwa.

Nahisi mzee Mwanakijiji amepata picha hizo kutoka kwenye hiyo documentary ninayosema. Hebu na nyie itazameni mniambie mpigaji wa picha hizi alikuwa wapi? Je tuna uhakika hakukuwa na uhariri wa kuganga hizi picha kuleta ujumbe alioutaka huyo mtaliano? Nimeshuhudia leo Tv ya BBC wakiomba radhi kwa kuonesha picha za tsunami ya Indonesia na kudai ni kimbunga cha Burma! Tuna uhakika gani hapa panapooneshwa na huyu mzungu ni Zanzibar kweli?

Napinga mauaji, lakini napinga pia upotoshaji wa aina yoyote, na kwa mazingira yetu upo upotoshaji wa historia unaofanywa na wazungu kwa manufaa yao!

Hebu tazameni wenyewe hizi documentaries, nawawekea link hapa chini, nayi mtoe maoni yenu:
[media]http://www.youtube.com/watch?v=ZSkamXwMDYk[/media]
[media]http://www.youtube.com/watch?v=kT1LCuxXdcg&feature=related[/media]

Na hapa chini wazungu wanadai kuwa hata wakati wa maasi ya jeshi ya 1964, kulikuwa na mauaji mengi sana yaliyofanywa na waafrika dhidi ya wazungu, na anaonesha jinsi maiti walivyofurika huko Bagamoyo, na jinsi waarabu na wazungu walivyokuwa wanashambuliwa na kuuawa hadharani huko Dar es salaam! Hebu itazameni msikilize na lugha za hao wanaodaiwa kuwa ni "waasi" halafu mniambie ni lugha za Tanzania kweli hizo? Hata mwaka 1964 nadhani watanzania walikuwa wakizungumza kiswahili! Angalieni kipande kwenye link hapa chini:

[media]http://www.youtube.com/watch?v=0ZouHC9GfxY&feature=related[/media]
Huyo aliyetengeneza filamu hiyo hapo juu ndiye aliyetengeneza pia kipande hiki hapa chini, ambapo anazugumzia jinsi mwafrika alivyo mpumbavu kulinganisha na mzungu! Itazameni mniambie mtu anayezungumza mambo kama haya dhidi yenu anaweza kuwasemea mema?
[media]http://www.youtube.com/watch?v=n0KLhSwMvcs&feature=related[/media]

Angalia hapa anavyozungumzia "the new African":
[media]http://www.youtube.com/watch?v=vD3bwEI316I&feature=related[/media]

Jitahidini muangalie series yote ya "Africa Blood and Guts", inapatikana kwenye youtube, ziko parts 1-10. Halafu mrudi hapa mniambie tuna sababu gani ya kuwaamini hawa wazungu?
 
Kithuku... hoja yangu ina lengo la kuzua maswali; maswali ambayo yana lengo la kutufanya tuangalie historia yetu sisi wenyewe na kuiandika kwa usahihi na kwa ukweli.

a. Je kulikuwa na mauaji wakati wa mapinduzi?
b. Yalikuwa yaukubwa wa kiasi gani?
c. Waliouawa nani aliwazika/walizikwa wapi?
d. WAliouawa walidhurika vipi na nani hasa alihusika na mauaji?

Na kubwa ni kuweza kuangalia kama hali ya kisiasa ya leo inaweza kuunganishwa na matukio ya mapinduzi?
 
naam sasa ndio utamu unapokuja hapo.

nilisema kule mwanzo mkuu mwanakijiji amekuja na picha za maigizo ambazo hazikuwahi kutokea ktk hali halisi zanzibar.

mimi ni mtu wa wastani ktk ufahamu huambiwa na kujiambia, nimezaliwa zanzibar na kukuwa zanzibar hadi nilipopata wasaa wa kugura kwetu ni kupendako kuliko popote pale. mbali ya kuwa nnaipenda Tanzania na CCM mzuri lkn uzanzibari wangu ni juu kuliko vyote nilivyovitaja hapo juu.

hakuna pahala ambapo panasemwa kuwa pamezikwa watu kama ilivyoonesha picha za mwanakijiji na kama ipo ni rahisi tungeenda na kuchimbua na kuona ushahidi wa mifupa kama ilivyo kwa nchi nyengine ilivyotokea


zanzibar ni nchi ambayo tukubaliane ni nchi ambayo siasa imo kwenye damu ya kila mzanzibar na kw propaganda ndio wenyewe na kila mtu hujua jinsi gani avutie kwake.

ili wanaopinga mapinduzi yaonekane hayafai na hayana maana ni kuonesha jinsi gani waliuwawa watu wengi kiasi ambacho hakina idadi na wengine hudai waliouwawa ni waarabu tu wakati sio kweli waliouwawa wamo waarabu wahindi waafrika na hata magowa inategemea wewe unaunga mkono upande gani.

niliwahi kutoa ushahidi babu zangu wawili baba mmoja mama mmoja mmoja alikuwa hizbu na mwengine alikuwa ASP ilipopinduliwa serikali kama sio kaka yake kumkingia kifua angeuwawa na yote kwa sababu ya maneno yake kabla ya mapinduzi.

ASP na wao kutaka kuonesha umuhimu wa mapinduzi wanapropaganda zao huzitawanya na nnaamini wengine mshawahi kuzisikia:

Beit la jaib limejengwa kwa vichwa vya watu yaani kila kwenye nguzo mmefukiwa vichwa vya watu kisha ikasimamishwa nguzo. (akili kichwani mwako)

waarabu waliwafagilisha mabibi zetu kwa maziwa yao utajiuliza mwenyewe vipi ziwa liweze kufagia?


biashara ya utumwa ilipokuwa ikiendelea baadhi ya wake wa mfalme husema nnataka nimuone mtoto alivyokaa tumboni basi huletwa kijakazi na kupasuliwa tumbo na kisha huangalia mtoto alivyokaa

pia husemwa wengine hupandishwa kwenye minazi halafu watu hujifundishia shabaha


na mengi kuliko hayo husemwa ila kwangu naamini ni propaganda ya mwamba ngoma huvitia kwa ke
 
Inaelekea yaliyotokea usiku ule ni tofauti sana na mambo tunayoyafahamu kutokana na jinsi tulivyofubdishwa.

Mie sifahamu zaidi kuhusu what happened in Zanzibar LAKINI naamini kuna ukweli unafichwa katika historia ya nchi yetu. Umefika wakati sasa tuelezwe ukweli kuhusu Zanzibar na isiwe porojo za wanasiasa oh fulani aliongoza Mapinduzi, oh Baba yangu alipigania Mapinduzi wa Wazanzibar kumbe haikuwa hivyo. Nafikiri bado wapo watu wengi wanaishi wanaweza kutueleza The ALL ISSUE na tusitegemee yale ambayo tumekuwa tukiambia tangu Misingi 7 (Shule ya Msingi)
 
suala la kujiuliza ni nini sababu ya mapinduzi? yalikuwa na umuhimu gani kwa mzanzibari? au ilikuwa ni kujivutia tu uongozi kwa watu wachache?

nauliza masuala haya kwa sababu kwanza, mapinduzi yalifanyika mwezi mmoja tu baada ya uhuru wa zanzibar chini ya sultan ( mornachy system). na kuliundwa baraza la mawaziri kutokana na upigaji kura.

kwanini mapinduzi yasisubiri kuona iwapo hii demokrasia iliyotumika was successfull or not?

mbili, siwezi kuzungumzia sana mapinduzi yenyewe, lakini baada ya mapinduzi watu walipokonywa mali zao, na walifanyishwa forced marriage.
ati wasichana wenye asili ya kiarabu lazima waolewe na waliojiita waafrika halisi. watu walikuwa wanafungwa na kupigwa bila sababu za msingi. hizo ni facts wala hazipingiki.

na hadi leo ni madukuduku ya watu, na wanashindwa kusema kwa kuwa mapinduzi yamekuwa kama kitu kisichopaswa kuzungumzia, isipokuwa kwenye propaganda za mikutano ya ccm.

hakuna anayeweza kurudisha wakati, lakini suala la kuzungumzia uhalali na umuhimu wa mapinduzi ni zuri kwa psychological stability ya watu wengi zanzibar.
 
Mtu wa pwani... ni watu wangapi waliuawa kwenye mapinduzi? walizikwa wapi na nani?

waliofia mjini walizikwa mwanakwerekwe na waliofia mashamba walizikwa mashamba lakini idadi haivuki hata watu manne.

zaidi tafuta kitabu cha mapuri usome kuhusu mapinduzi
 
Mtu wa Pwani, yaani Mapuri ni uninterested party katika sakata hili? Kwanini niyaamini maneno ya Mapuri?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom