Kingsharon92
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 7,554
- 9,531
Hii tabia wanayo watu wengi sana hasa kwa walio mikoa mingine au nchi nyingine kikazi ki utafutaji unakuta mtu amezaliwa mwanza akazamia moro kajenga huko na watoto ila utamsikia mimi nikifa mkanizike kwa mababu zangu mwanza mnipeleke kabisa sasa tuwaambie wenye tabia kama hizo muandae kabisa na pesa za kuwapeleka makwenu mkiwa marehemu mpige hesabu kabisa kutoka huko mliko mpaka walikozikwa mababu zenu ni kiasi gani muweke benki ili mkikabidhi jezi msihangaishe watu mpaka wanakopa pesa wanauza vitu ili mpelekwe kwenu msiba unaisha watu wana madeni ya kutosha ili hali hata moro kuna Ardhi ya kukuhifadhi