Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,875
Wilaya nne za mkoa wa Mtwara zimekosa nishati ya umeme kwa takribani saa ishirini na nne na kupelekea baadhi ya shughuli za kiuchumi kusimama, baada wanafunzi wa kidato cha tatu na cha pili wa shule ya sekondari Mnyawi kuchezea laini kubwa ya umeme kwa kurusha miti na kufurahia mwanga pale nyaya zinapogusana.
Meneja wa TANESCO wilaya ya Tandahimba Edward Namoto amesema michezo hiyo ni hatari lakini pia inaumiza wananchi wanaotegemea nishati hiyo kujipatia kipato.
Aidha, Wanafunzi hao wa kidato cha tatu ambao wamepanga katika kijiji hicho kwa ajili ya ukaribu wa shule wamekiri hilo.
Chanzo: ITV