Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,395
Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara linawashikilia wanafunzi 9 wa Chuo Kikuu cha Stella Maris na Daktari wa Hospitali ya Mission Nanyamba, wakituhumiwa kutumia mitandao ya kijamii ikiwamo WhatsApp na Telegram kuhamasisha maandamano.
IKUMBUKWE KUWA: Mnamo mwezi Machi mwaka huu, Rais Dkt. John Magufuli aliwaonya vikali watu wanaopanga kufanya maandamano nchini akisema kwamba hawataruhusiwa.
"Wapo watu wangependa nchi hii kila siku tuwe na migogoro," alisema Dkt Magufuli.
"Wapo watu ambao wameshindwa kufanya siasa za kweli, wangependa kila siku tuko barabarani tunaandamana. Watu wao wanahamia huku, wao wanataka wabaki wanaandamana kule.
Nitasema ngoja waandamane wataniona. Kama kuna baba zao wanawatuma, watakwenda kuwasimulia vizuri."
"Niliapa kwa katiba kwamba nchi hii lazima iwe ya amani."
IKUMBUKWE KUWA: Mnamo mwezi Machi mwaka huu, Rais Dkt. John Magufuli aliwaonya vikali watu wanaopanga kufanya maandamano nchini akisema kwamba hawataruhusiwa.
"Wapo watu wangependa nchi hii kila siku tuwe na migogoro," alisema Dkt Magufuli.
"Wapo watu ambao wameshindwa kufanya siasa za kweli, wangependa kila siku tuko barabarani tunaandamana. Watu wao wanahamia huku, wao wanataka wabaki wanaandamana kule.
Nitasema ngoja waandamane wataniona. Kama kuna baba zao wanawatuma, watakwenda kuwasimulia vizuri."
"Niliapa kwa katiba kwamba nchi hii lazima iwe ya amani."