Mtumishi wa umma atakuwa na furaha pindi tu Serikali itakapoamua kumkopesha bila riba

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,646
35,981
Binafsi ni mtumishi wa umma. Nimewahi kukopa mara 1 na kufanya top up mara 2. Kwa lugha nyepesi ni kwamba nimekopa mara 3.

Kwakweli hali ni mbaya, topup ni wizi wa wazi kabisa. Hata hii mikopo ni unyonyaji ila tu watumishi hukopa kwa aidha shida ya haraka au kukosa maarifa. Muda mwingine hukopa ili tu mtu ajikwamue aweze kununua usafiri, kujenga au kulipa ada yake au ya mtoto.

Ashukuriwe Mungu sasa nina miaka 3 sijakopa wala kufanya topup. Nasubiri deni liishe nikope parefu kidogo niache kazi. Maana siku hizi ukiacha kazi ili ukajiajiri hupati kirahis ile fedha yako kutoka mfuko uliochangia.

Kwakweli watumishi wa umma ukiondoa wezi na mafisadi siku zao za furaha zinahesabika.

Katika mwezi wa siku 28-31 mtumishi wa umma hupata furaha siku 5- 10 tu.

Serikali iwakopeshe watumishi wake mikopo isiyo na riba ili kuwaondolea ufukara na umaskini.

Kwakweli watumishi wengi ni mafukara, kadi zao za benki zimewekwa rehani jambo ambalo ni aibu.

Hizi microfinance institutions zimewarubuni watumishi. Wengi huziendea ili kupata mkopo wa chap wasolve shiida zao baadaye zinageuka kuwa mwiba.

Hata hizi benki kubwa bado zinawaumiza watumishi wa umma ingawa kupata mkopo wenyewe mpaka muzungushane.
 
Subiri majibu ya 'billionaires of tomorrow'
Ulichoongea ni uhalisia.
Watumishi wengi wanaishi katika hali ngumu. Matumaini yao yamekuwa kwenye kusubiria pesa za mafao ili wajenge, wafanye biashara(ambazo hawana hata uzoefu) pamoja na kusomesha watoto wa mwisho.
Bahati mbaya stress za kuchelewa kwa mafao na nyumba ndogo zinachukua uhai wao.
 
Subiri majibu ya 'billionaires of tomorrow'
Ulichoongea ni uhalisia.
Watumishi wengi wanaishi katika hali ngumu. Matumaini yao yamekuwa kwenye kusubiria pesa za mafao ili wajenge, wafanye biashara(ambazo hawana hata uzoefu) pamoja na kusomesha watoto wa mwisho.
Bahati mbaya stress za kuchelewa kwa mafao na nyumba ndogo zinachukua uhai wao.
Tunayashuhudia haya uliyoyaandika kila leo
 
Baadhi ya taasisi zinakopesha watumishi wake bila riba, benki kuu, mifuko ya hifadhi ya jamii wana mikopo kwenye revolving credit facility ambapo mtumishi anaweza kukopa hadi 100M bila riba kwa kipindi flani ama riba kidogo sana.

Mikopo Tanzania kutoka hizi taasisi za fedha iko juu sana.

Sio rahisi serikali iweke revolving fund kwa watumishi wake wote. Hiyo ni arrangement ambayo inaweza kufanywa na taasisi husika. Nategemea CWT iwe na revolving fund kusaidia waalimu.
 
Sandali Ali mbona mkuu karibia nyuzi zako zote zimeongelea zaidi kuhusu watumishi?
Jf kila Mtu ni mtumishi wa umma, lakini pia hoahao ndio kwenye nyuzi nyingine utaona wanalalamika wamemaliza vyuo na hawana ajiraa.
Ukuwa humu jua kuwa wewe ni mtumishi, una gari, una nyumba nzuri na unajua kila kitu
Kuishi humu kunahitaj ujiongeze shekheee
 
Jf kila Mtu ni mtumishi wa umma, lakini pia hoahao ndio kwenye nyuzi nyingine utaona wanalalamika wamemaliza vyuo na hawana ajiraa.
Ukuwa humu jua kuwa wewe ni mtumishi, una gari, una nyumba nzuri na unajua kila kitu
Kuishi humu kunahitaj ujiongeze shekheee
Mimi pia ni mtumishi wa Umma, ni baba wa familia, ni mjasiriamali, ni mpenda mabadiliko a.k.a UKAWA, nk.

Nongwa iko wapi mkuu!!! Relax!!!!
 
Mbona Watumishi wa Umma wanapewa mikopo isiyo na Riba ipo tangu miaka ya 1990 inatolewa na Wizara ya Fedha kupitia Kitengo cha Advance. Labda kwa miaka ya sasa sasa sijui lkn kwa Historia hizi fedha zinatolewa kwa kila Ofisi watumishi wakopeshwe bila riba yoyote na inaanzia 15 hadi Mil.55.
 
Baadhi ya taasisi zinakopesha watumishi wake bila riba, benki kuu, mifuko ya hifadhi ya jamii wana mikopo kwenye revolving credit facility ambapo mtumishi anaweza kukopa hadi 100M bila riba kwa kipindi flani ama riba kidogo sana.

Mikopo Tanzania kutoka hizi taasisi za fedha iko juu sana.

Sio rahisi serikali iweke revolving fund kwa watumishi wake wote. Hiyo ni arrangement ambayo inaweza kufanywa na taasisi husika. Nategemea CWT iwe na revolving fund kusaidia waalimu.
Hivi kwa hadi sasa ile mifuko kama LAPF, PSPF na mingineyo bado inatoa huduma hizo za mikopo na mafao mengine au ni jukumu la mfuko mpya ulioanzishwa?
Mwenye kujua hili asaidie.
 
Hivi kwa hadi sasa ile mifuko kama LAPF, PSPF na mingineyo bado inatoa huduma hizo za mikopo na mafao mengine au ni jukumu la mfuko mpya ulioanzishwa?
Mwenye kujua hili asaidie.
Hiyo mifuko ishamezwa na huduma hizo hazipo sasa
 
Naona lengo la kuunganisha mifuko kwao limetimia.
Ni kukusanya bila kuboresha huduma.
Ushindani una ladha yake kwa kila kitu. Hufanya ubunifu na ujuzi/taaluma kufanya kazi kwa kiwango chake halisi
Ile mifuko ilikuwa na bakshishi nyingi. Sasa hakuna fao wala mkopo wowote kutoka lifuko hili la kishetitwani
 
Back
Top Bottom