Mtumishi mwandamizi Ikulu adai kufukuzwa kama mbwa...

Mpitagwa

JF-Expert Member
Feb 10, 2012
2,339
1,119
Mtumishi mwandamizi wa serikali ya Tanzania, kwenye kitengo cha kurusha ndege za rais mzee Kileo, leo amefukuzwa kwenye nyumba aliyopewa na serikali kuanzia mwaka 1972.

Akiongea na Channel 10 kwa uchungu mzee Kileo amelalamika kuwa amekuwa rubani mwadilifu akirusha ndege za marais wote waliopita na sasa ni mshauri wa rais kwenye masuala ya anga amesikitishwa sana na kutolewa vifaa nje ya nyumba kunakofanywa na kampuni ya udalali kwa idhini ya mahakama. Amedai wenzake waliokimbia serikalini sasa ni matajiri wa kutupwa wengine wakimiliki meli na wengine ndege. Yeye aliyevumilia ndoo yanamkuta haya.

Dalali mwenye kazi hiyo amedai kuwa amepewa kazi ya kuvunja nyumba hiyo na benki ya TIB ambao wanataka kutumia eneo hili kwaajili ya ujenzi wa Benki ya Wakulima.

Changamoto, nani atakubali kuwa mtumishi mwaminifu ili baadaye yaje yamkute haya ya mzee Kileo? Kitendo kama hiki hakichangii tabia ya ufisadi na rushwa serikalini ili watu wachukue chao mapema?
 
Na aendelee kuimba ile nyimbo ya "KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI"

Sijui hata ni KIDUMU cha lita ngapi!!!!

ccm haiko kwa ajili ya kuwatetea wanyonge bali ile ni taasisi ya kulinda mali za viongozi mafisadi na kuwakingia kifua wafanyabiashara haramu.
 
Huenda kuna mzito anataka kupewa nyumba hiyo kama haikuuzwa wakati wa kuiba majumba ya umma. TIB ni ile benki ambayo mkuu wake ni Pita Noni aliyefanikisha wizi wa EPA siyo?
 
tungepata sababu ya kumtoa ingekuwa bora zaidi. Hiyo ni nyumba ya umma na tumekuwa tunalalamika nyumba hizo kuuzwa nadhani sasa inatosha zoezi la kuuza nyumba lisimame. Kama hakupata basi, je hana nyumba binafsi?
 
Pole mzee Kileo, uadilifu aliondoka nao Nyerere, waliokimbia serikalini waliona hayo mapema
 
Kama amekaa kwenye nyumba hiyo tangu 1972 bure anasitahiri kuwa na nyumba yake amekaa miaka 41 bado hakujenga.......

namsikitikia lakini ukweli lazima kusema, je wote waliostaafu bila nyumba serikalini tupitishe azimio la kuwapa nyumba hapa JF? Je wapewe nyumba? Ni sawa na kuhalalisha kuwa sera ya kuuza nyumba za umma iendelee.

je watumishi wa umma ambao wako nyumba za kupanga wapewe nini? Hii tabia ya kujimilikisha nyumba za umma ni wakati wake ifike kikomo.
 
Kama amekaa kwenye nyumba hiyo tangu 1972 bure anasitahiri kuwa na nyumba yake amekaa miaka 41 bado hakujenga.......

namsikitikia lakini ukweli lazima kusema, je wote waliostaafu bila nyumba serikali tupitishe azimio hapa JF wapewe nyumba? Ni sawa na kuhalalisha kuwa sera ya kuuza nyumba za umma iendelee

Swadakta!
Watu wanazeeka vibaya, 41 years hujajenga, kwa position yake hilo ni tatizo.
 
Tangu 1972 mpaka leo anakaa nyumba ya serikali tu?
Kuna watu mpaka leo lile neno Fainaly uzeeni wanadhani ni la utani, huyu mtu hata mke aliyeoa ni saa saba usiku anasubili kupanuwa mapaya tu, hivi kuwa na mke anayeshindwa kukushauri muwe na nyumba yenu ni wa kazi gani?

Kuna Zee moja nalo la hovyo kweli limeshika vyeo vikubwa Serikalini lakini mpaka leo linakaa Ilala Flat ambapo mimi zile Flat naziona ni kama bachela apartment tu kwa jinsi zilivyo na vyumba vidogo na sebule ndogo.
 
kuwa mtumishi mwadilifu hakumaanishi haki ya kujimilikisha mali ya serikali,
labda alalamike kuwa taratibu hazikufuatwa..
 
mhn, kazi kwelikweli, hatutafika , kwa michango ya watu inaonyesha tusivyo kuwa waadilifu, na ukiwa muadilifu unatukanwa! nilikuwa napita tu !
 
Kuna watu mpaka leo lile neno Fainaly uzeeni wanadhani ni la utani, huyu mtu hata mke aliyeoa ni saa saba usiku anasubili kupanuwa mapaya tu, hivi kuwa na mke anayeshindwa kukushauri muwe na nyumba yenu ni wa kazi gani?

Kuna Zee moja nalo la hovyo kweli limeshika vyeo vikubwa Serikalini lakini mpaka leo linakaa Ilala Flat ambapo mimi zile Flat naziona ni kama bachela apartment tu kwa jinsi zilivyo na vyumba vidogo na sebule ndogo.

Kwanini unadhani ni kosa la mwanamke?
 
Deadbeat serikali ya JK, kushindwa kulipa madeni, licha ya debt ceiling kuwa kubwa. Serikali inashindwa kulipa mishahara, mafao ya wastaafu, but JK kutwa angani kuomba vyandarua
 
mhn, kazi kwelikweli, hatutafika , kwa michango ya watu inaonyesha tusivyo kuwa waadilifu, na ukiwa muadilifu unatukanwa! nilikuwa napita tu !

No, hilo sio suala la kuwa muadilifu bali ni suala la kuishi kitoto na kutokuwa na malengo.



Hivi miaka yote hiyo akiwa kazini alishindwa ata kujenga kinyumba cha kuishi?ni uzembe na ujinga usiopaswa kuendekezwa.
 
Kuna watu mpaka leo lile
neno Fainaly uzeeni wanadhani ni la utani, huyu mtu hata mke aliyeoa ni
saa saba usiku anasubili kupanuwa mapaya tu, hivi kuwa na mke
anayeshindwa kukushauri muwe na nyumba yenu ni wa kazi gani?

Kuna Zee moja nalo la hovyo kweli limeshika vyeo vikubwa Serikalini
lakini mpaka leo linakaa Ilala Flat ambapo mimi zile Flat naziona ni
kama bachela apartment tu kwa jinsi zilivyo na vyumba vidogo na sebule
ndogo.

Mkuu Matola unazeeka vibaya mbona mkali hivyo
 
Sasa naye amekaa kwenye nyumba ya serikali miaka yote hiyo hata kujenga kakibanda tu cha kujihifadhi lol...dah! pole yake bwana atafanyaje sasa wenyewe ndo wameamua hivyo!
 
Back
Top Bottom