Mtumeee,Richard Ndasa(Mb) asema Sh.40 ya road license haitaongeza nauli

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,191
103,714
Richard Ndasa jana akichangia bajeti aliwananga wapinzani kwamba hawana nia nzuri na wananchi. Akizungumzia ''kufutwa'' kwa road license Ndasa alisema kwamba ongezeko la Sh.40 kwa lita halitakuwa na madhara yeyote kwenye nauli na bei kwa ujumla. Pasipo kufafanua zaidi Ndasa alisema kuwa ameongea na Shabib(Mbunge na mmiliki wa mabasi ya Shabib) amemwambia kuwa eti nauli haitaongezeka.

Wakati akihitimisha mchango wake, licha ya kuwa mbunge kwa miaka zaidi ya 15, ameshangazwa na ufisadi uliofanyika kwenye madini na amesisitiza mikataba iletwe bungeni.

Richard Ndasa ni mbunge wa Sumve kupitia CCM. Amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, akipitisha sheria za madini na ni mmoja kati ya walioazimia kumfukuza Zitto na Mnyika wakitaka mikataba ya madini ipitiwe bungeni
 
Ongezeko la sh 40 tu ndio lipandishe nauli? Huyo mbunge yupo sahihi
 
Hawa si ndio wa ndioooooooooooo ndioooooooo papapapapapapapapapapapapapap ...shit
 
Huwa ndo mlivyooo...wazee wa ndiyoo
Sio lazima tufanane mawazo. Mtu umeondolewa road licence ukaongezewa 40 kwenye mafuta unapiga kelele za nini. Road licence ilikuwa ni mzigo mkubwa kuliko hiyo 40 iliyoongezeka hapo. Mmezidi kulalamika kila kitu. Hebu eleza hiyo 40 inaongeza vipi nauli. Labda naweza kukuelewa.
 
Back
Top Bottom