OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,191
- 103,714
Richard Ndasa jana akichangia bajeti aliwananga wapinzani kwamba hawana nia nzuri na wananchi. Akizungumzia ''kufutwa'' kwa road license Ndasa alisema kwamba ongezeko la Sh.40 kwa lita halitakuwa na madhara yeyote kwenye nauli na bei kwa ujumla. Pasipo kufafanua zaidi Ndasa alisema kuwa ameongea na Shabib(Mbunge na mmiliki wa mabasi ya Shabib) amemwambia kuwa eti nauli haitaongezeka.
Wakati akihitimisha mchango wake, licha ya kuwa mbunge kwa miaka zaidi ya 15, ameshangazwa na ufisadi uliofanyika kwenye madini na amesisitiza mikataba iletwe bungeni.
Richard Ndasa ni mbunge wa Sumve kupitia CCM. Amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, akipitisha sheria za madini na ni mmoja kati ya walioazimia kumfukuza Zitto na Mnyika wakitaka mikataba ya madini ipitiwe bungeni
Wakati akihitimisha mchango wake, licha ya kuwa mbunge kwa miaka zaidi ya 15, ameshangazwa na ufisadi uliofanyika kwenye madini na amesisitiza mikataba iletwe bungeni.
Richard Ndasa ni mbunge wa Sumve kupitia CCM. Amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, akipitisha sheria za madini na ni mmoja kati ya walioazimia kumfukuza Zitto na Mnyika wakitaka mikataba ya madini ipitiwe bungeni