Serikal hii bhana,inakutumia,inakumwaga,ndo ashamwagwa huyo
Huyu jamaa ni wa kukatakata na kuwapa mamb wamle tu
Huyu jamaa ni wa kukatakata na kuwapa mamb wamle tu
jamaa kafanywa mbuzi wa kafala,sasa polis mjifunze wanawatuma nyie walala hoi wao wakubwa wamekaa tuu ikitokea la kutokea unatolewa kafala peke yako.kazi kwenu polis mjifunze sasa
Jamani hivi Chagonjwa atafanywaje kwa kuudanganya umma kuwa eti bomu lilirushwa tokea upande wa wafuasi wa CDM?
Ni mahakama gani? walisema mahakama ya kijeshi, is this true?
Kisheria huwa tunatowa na reference na reference nzuri ni kesi ya Zombe, Kamanda Zombe hakuwepo sehemu ya tukio la mauwaji lakini alikamatwa na kujumuishwa kwenye shtaka la mauwaji kwa sababu yeye alitoa amri ya mauwaji.
Sasa inashangaza huyu RPC Kamuhanda yeye pia alitowa amri ya mauwaji na alikuwepo eneo la mauwaji kushuhudia agizo lake linatekelezwa kisha ndio akatokomea, je ni kwa nini huyu asiwe mshitakiwa namba moja kwenye kesi hii ya mauwaji?
Hii haikubaliki na hatuwezi kuruhusu ujinga huu uendelee ndani ya Taifa letu.
, nawapa reference mkumbuke Zombe akushiriki wala hakuwepo kwenye tukio la mauwaji lakini alitiwa pingu kwa sababu yeye ndio alitowa amri ya Mauwaji, swala la Zombe kushinda kesi ni hadithi nyingine ya uzembe wa makusudi kutokuwa na madpp wenye viwango.
September 12, 2012
BREAKING NEWssssssssMTUHUMIWA WA MAUAJI YA MWANGOSI AFIKISHWAMAHAKAMANI LEO IRINGA
Askari anayetuhumiwa kumuua Daudi Mwangosi leo amefikishwa katika Mahakama ya wilaya ya mkoa wa Iringa na kusomewa mashitakata yake. Huku akiwa chini ya ulinzi mkali ambao ulifanya wanahabari waliofika mahakamani kujitahid kupata picha kwa ugumu.
Akisoma mashtaka mbele ya hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya wilaya Daines lymo mwendesha mashtaka ameeleza kuwa mtuhumiwa Pacificus Cleophase Simon (23
HABARI KAMILI ITAKUJIA HIVI PUNDE
Ni yakuangalia nani atasimamia vinywaji na ChakulaWalioko Iringa tunaomba picha kwa sababu picha za wauwaji wote tunazo, hatukubaliani na mazingaombwe haya, halafu naomba tu kuuliza sasa ile kamati ya harusi ya Nchimbi kazi yake ni nini sasa? changa la macho hili.
Akina Mwema na Chagonja hawa wanapaswa kuwajibika wenyewe,lasivyo Rais awatimue. Kwa kesi ya Iringa ni lazima Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya mauaji yamefanyika wajiuzulu,hawa ndiyo wakuu wa Kamati za Ulinzi na Usalama maeneo husika. Aidha wakuu wa Tiss wa mkoa na wilaya wawajibishwe. Walizembea!Achana na huyo chaugonjwa yeye na mke wake ni matapeli tu.
wasiwasi wangu ni umri uliotajwa!!!waliopo kwenye picha sioni kama kuna umri wa miaka23,au niwalewale akina Shigella?Sikubaliani kabisa na kesi hii ni batili, Wanaharakati wote wanapaswa kuipinga hii kesi maana ni kuwafanya Watanzania ni wapumbavu kuliko maelezo.
kelele zilizopigwa na hasa hapa jf kijitahidi kuweka picha za matukio zimesaidia sana kuizuia serikali isilete repoti ya uongo kwa watanzania kama ilivyozoeleka.
Kwa hiyo chamsingi sasa ni kuwa angalau katika hatua 100 za kwenda tumepunguza mbili basi iwe kama ndio tuaanza kuwasha moto.
Tuongeze msukumo na hasa kwa wale wanaoelewa masuala ya kisheria waweke wazi ufafanuzi ili na hao wengine weletwe mbele ya sheria ambapo itasaidia huko mbeleni hawa jamaa zetu wa polisi kupunguza au hata kuacha ukatili na manyanyaso yao.
tears in my eyes! i feel sorry for the young boy!