Mtu wa Kanda ya Ziwa kutokujua kuogelea ni ujinga wa hali ya juu

Kufa ni lazima kwa kiumbe CHOCHOTE kilichozaliwa vingine vinaepukika mfano kujaza abiria kwenye vyombo vya usafiri ni kosa lakini mamlaka huwa zimelala hazichukui hatua. Sasa huku Africa vtu vinatokea kizembe unasema ni mtego tena ndo mana huwa tunashindwa kuondoa matatizo
Unaongela hbr za mamlaka utadhani u mgeni......mnakera na post zenu za kijinga, eti wangeogelea....
 
Sio kosa la marehemu vitu vingi ni uzembe jamani kuanzia kushindilia watu kupita kiasi, no life jackets na haya majanga hujirudia Mara kwa Mara, pia na sisi RAIA tujihurumie kwanza sisi wenyewe tukisubiri wanasiasa tutateketea tu
Kweli mkuu mi nakuelewa vizuri sana,madhara ya kubana matumizi Hadi kwenye masuala ya msingi haya ndio madhara yake
 
Hata mimi nimeshangaa sana,nimekulia kanda ya ziwa pembezoni mwa ziwa,nimeanza kuogelea nikiwa sijafika miaka 10 ,nimeshangaa sana kuona picha za vijana wa kiume tena vijana wadogo sana wamekufa maji,tena umezaliwa kisiwani hujui kuogelea,muogeleaji hata kama ingezama katikati ya ziwa huwezi kuzama mpaka unaokoka khofu ni samaki wakali tu
Wewe umeandika point bila unafiki mi mwenyewe nimeshangaa sana kwa kweli
 
Yap ni rahisi kujifunza hayo ila sio kila kitu chakujifunza au kila kitu ni chakuiga

Kuogelea yahitaji moyo mtu anaishi mwanza ila mwoga wa maji ya ziwan huwez jifunza kuogelea kwa kuiga kuogelea kujifunza vp wale walio kuwa wanaiga kuogelea kwenye mabwawa wakanywa vibba kama vyote
 
Hata kama ingepinduka kama gari kama unajua kuogelea lazima utajiokoa tu,mtu anaejua kuogelea ndani ya maji ni kama boya tu anaelea,kama hujui ndio unakuwa kama shilingi lazima uende chini tu
Wewe hujui kuogelea Kivuko kikipinduka na kukulalia huna jinsi. Ujue ukubwa wa Kivuko pia kuna miziko na abiria pia vyote hivyo ni vikwazo katika kuogelea ndiyo maana wengi waliopona ni wale waliopata kuruka mapema kabla hajapinduka na Kivuko hakikupinduka uelekeo wao!
 
Kuogelea yahitaji moyo mtu anaishi mwanza ila mwoga wa maji ya ziwan huwez jifunza kuogelea kwa kuiga kuogelea kujifunza vp wale walio kuwa wanaiga kuogelea kwenye mabwawa wakanywa vibba kama vyote
Unachosema ni kweli mkuu ila ukikaa mazingira kama hayo inabidi usiwe muoga wa maji maana utakufa kizembe sana angalau usubiri muokoaji
 
Back
Top Bottom