Sisi tuliosoma mchafukoge sec school tuna uwezo mkubwa Sana wa kukariri, swala la kuelewa utalikuta kazin
Hahaa...mtoto akiwa bright huhitaji kumpeleka mashule yenye majina makubwa sijui ada mil. 10. Mwache hapo hapo ila habari yake wataipata tu kwenye matokeo ya kitaifa. Mimi ilinigharimu niliposoma O-level private ambapo kila kipindi mwalimu anaingia, shida ikaja A-level mwalimu humwoni na material unajitafutia. Kwenye mazingira kama hayo ndo utamwona mwanafunzi ambaye ni kichwa.....Usinikumbushe mapito niliyo pitia.
Ile naanza na form five tu mwalimu wa kemia mzungu,mmarekani na Mjapani,hesabu ni mchina wa kimarekani na Mhindi,nageukia Fizikia nakutana na mzee Ngui sijui kabila gani masikini muda wote ni kufoka tu. Halelujaaa DS hii hapa na mzee Mwangoka anafundisha kwa kinyakyusa na stori zake za Tukuyu na kufukuzwa chuo kikuu kwa migomo...
Ikawa mwanzo mwisho ni kumeza tu....
ukiwa na pesa hutawaza hivyo mkuuNdo yale mambo ya junior junior, mpeleka huko changanyikeni akapambanie kombe.
Enyiwehi, umeongea ukweli mkuu
Nadhani serikali ijaribu kubuni mfumo mzuri utakaojengea wanafunzi ufahamu na uelewa wa kusoma na kuweza kutatua changamoto za mazingira yetu. Sio kusoma ma theory tu yaliyo solve nchi za ulaya na kusahau mazingira yetu na changamoto zake.Kuwa mjumbe wa Bodi wa Shule kumenisaidia kufahamu mengi juu ya hizi shule za serikali.Hizi shule za serikali siku hizi zimejaa siasa na mihemuko. Syllabus haifuatwi,kuna wataalamu wa elimu wanaojiita wakuu wa shule na maafsa elimu wa halmashauri kutwa kubuni vitu vya ajabu ajabu mara;
Wanafunzi wanakatazwa kusoma masomo mengine wasome Civics na Kiswahili eti wapate 'D' mbili za cheti.
Kuna baadhi wanaambiwa waache kabisa kusoma somo la hisabati. Wengine wanakatazwa walimu wasifundishe badala yake wawape wanafunzi mitihani na wasolve! Jumlisha mitihani ya inter- school, pre - mock,Mock,pre NECTA ,Terminal,Mid-term nk. Kunawafanya walimu wasifundishe kabisaa. Maagizo ya mara kwa mara toka kwa wabunifu wa wilayani na ubunifu wa mkuu wa Shule yasiyofuata na kuzingatia syllabus sio tu yanapunguza maana ya mtaala pia malengo yaliyokusudiwa.
Hivi inamaana hatuwezi kubadilisha mitaala ya hizi shule zetu ziwe kama za kimataifa. Najiuliza tu. Kwani hatuwezi au ni nini shida
... kwa upande wa HR unahitaji kuondoa, kujengea uwezo, na kuajiri walimu zaidi ya 100,000 sio mchezo. Hao utakaowaondoa inamaanisha lazima "redundancy" ipite sasa malipo yake ndio balaa; piga hesabu hapo kila mmoja alipwe average 100,000,000 unazungumzia more than 10tr/- redundancy ya walimu halafu uanzishe ajira mpya ku-replace hao walioondolewa. Hiyo ni HR peke yake; njoo kwenye miundombinu; vitabu; n.k. Si mnataka ISO-certification?Hivi inamaana hatuwezi kubadilisha mitaala ya hizi shule zetu ziwe kama za kimataifa. Najiuliza tu. Kwani hatuwezi au ni nini shida
Mbona wengine tumesoma hizi hizi shule za sirikali, tena shule ya msingi kijijini kwa babu kuongea kilugha mwanzo mwisho lakini tumefanikiwa kupata scholorship kusoma Masters na PhD kwenye international universities ambazo zipo kwenye world ranking ya 10 bora, what happened?
Umenena mkuu. Siku hizi kila mwenye nafasi anapanga lake analodhani litamsaidia kulinda cheo chake au kupanda zaidi.Kuwa mjumbe wa Bodi wa Shule kumenisaidia kufahamu mengi juu ya hizi shule za serikali.Hizi shule za serikali siku hizi zimejaa siasa na mihemuko. Syllabus haifuatwi,kuna wataalamu wa elimu wanaojiita wakuu wa shule na maafsa elimu wa halmashauri kutwa kubuni vitu vya ajabu ajabu mara;
Wanafunzi wanakatazwa kusoma masomo mengine wasome Civics na Kiswahili eti wapate 'D' mbili za cheti.
Kuna baadhi wanaambiwa waache kabisa kusoma somo la hisabati. Wengine wanakatazwa walimu wasifundishe badala yake wawape wanafunzi mitihani na wasolve! Jumlisha mitihani ya inter- school, pre - mock,Mock,pre NECTA ,Terminal,Mid-term nk. Kunawafanya walimu wasifundishe kabisaa. Maagizo ya mara kwa mara toka kwa wabunifu wa wilayani na ubunifu wa mkuu wa Shule yasiyofuata na kuzingatia syllabus sio tu yanapunguza maana ya mtaala pia malengo yaliyokusudiwa.
Wazo zuri aisee ,wangeanza hata na shule zao zile special (mzumbe,kibaha,ilboru,Tabora b&g,kilakala na msalato)
Hapo hata Mimi kanishinda aseeDaah nilikutana na mtoto wa shule hizi nikamuuliza una ndoto ipi akaniambia I want to be a UN SECRETARY.
Nikasema hawa kweli wanawaza international level.
Mkuu kuna world scholars kibao ambao hawajakanyaga hizo international schools na wanaheshimika kwenye field zao. Nafikiri hizo shule zimeanzishwa purposely kwa ajili ya watoto wa mabalozi kwenye nchi husika, hakuna jipya...
Lakini mbona kibongo talent nyingi zinatoka kwa watu ambao ni masikini na wasio na elimu kubwa
Mbona hatuoni hao international wakiongoza kwenye fani nyingi zinazotumia vipaji sana
Niache kula vizuri, niache starehe eti mtoto asome shule nzuri?
Atasoma hizo za baba ake
Mimi mwenyewe napenda mtoto wangu asome international school eeh mola nijalie, hizi shule zetu st kayumba mtoto GPA kubwa Ila exposure zero hata ufahamu
Lione hili nalo bichwa kama Lisu.
Kujieleza kwa kiingereza siyo kigezo cha kuelimika .
Kiingereza ni lugha tu kama kisukuma