Mtu mweusi alitoka wapi?

Easymutant

R I P
Jun 3, 2010
2,564
1,129
naomba kueleweshwa kwa mwenye ufahamu na hili ni katika kueleweshana
Naomba lisiwe na chembe za udini japo source yake imetoka kwenye bible bible hivi..
Nikiwa nimekulia na kulelewa katika mazingira ya dini ya kikiristo tulikuwa tukionyeswa vitabu
Na vitabu amabayo tulikuwa tunafundishiwa ni vile vyenye picha za adam na hawa na wengine wote ambao inaonyesha kwamba

Walikuwa ni watu weupe ambao niliamini niwazungu. Sasa najiuliza kama original ya adam na hawa walikuwa ni wazungu na ndio tunaaminishwa kwamba walikuwa ni wanadamu wa kwanza
Kabisa kuishi duniani je mie mtu mweusi nilitoka wapi? Maana siamini mzungu na mzungu wanaweza kuzaa mtu full black kabisa.

Kingine kinachonichanganya je zamani waliruhusiwa kaka na dada kuoana? Maana kama adamu na hawa ndo wakwanza it means waliozaliwa ni watoto je walijijenerate namna gani
Na isitoshe waliozaliwa tunaambiwa walikuwa wa jinsia moja wanaume tupu sasa hapo ndo sielewi kabisa msaada jamani!!!
 
Jibu la mtu mweusi ametoka wapi rahisi
..lakini hayo maswali yaliofutia..am waiting to see the answers!!
 
nadhani mwanadamu alianza kusambaratika pale mnara wa babel ulivyosambaratika.......watu walitawanyika kila mahali na kuongea lugha mbalimbali.....kwa maana hiyo kila sehemu walipokwenda ndivyo walivyozidi kubadilika kutokana na hali ya hewa...ila sina uhakika original alikuwa ni nani......kuhusu kuzaliana ni kweli walizaliana wao kwa wao kutokana na kuwa walikuwa wapo wenyewe na uzazi ulikuwa lazima ufanyike....kadri watu walivyoongezeka ndivyo wigo ulivyozidi kupanuka na sio kweli kuwa waliokuwa wanazaliwa walikuwa wanaume tu...hapana.....wanawake walikuwepo mfano kina sara, rebecca, esta, n.k, ila wanaume ndio waliokuwa wanahesabiwa kama kizazi kamili....nafikiri nimejaribu kukuelewesha
 
Sasa Easymutant we umeona mtu mweusi(Mwafrica) tu ndo ajabu? Vipi watu wa rangi nyingine kama wahindi wachina na waarabu? Au unadhani mzungu kwa mzungu wanaweza kuzaa mchina? Au kwako wachina na wahindi na wengineo ni wazungu? That issue is more than "mtu mweusi"
 
nadhani mwanadamu alianza kusambaratika pale mnara wa babel ulivyosambaratika.......watu walitawanyika kila mahali na kuongea lugha mbalimbali.....kwa maana hiyo kila sehemu walipokwenda ndivyo walivyozidi kubadilika kutokana na hali ya hewa...ila sina uhakika original alikuwa ni nani......kuhusu kuzaliana ni kweli walizaliana wao kwa wao kutokana na kuwa walikuwa wapo wenyewe na uzazi ulikuwa lazima ufanyike....kadri watu walivyoongezeka ndivyo wigo ulivyozidi kupanuka na sio kweli kuwa waliokuwa wanazaliwa walikuwa wanaume tu...hapana.....wanawake walikuwepo mfano kina sara, rebecca, esta, n.k, ila wanaume ndio waliokuwa wanahesabiwa kama kizazi kamili....nafikiri nimejaribu kukuelewesha

Dah! Preta kiukweli umeenda mbali mmo ngoja nisubiri bado hujanijibu kabisa
 
Sasa Easymutant we umeona mtu mweusi(Mwafrica) tu ndo ajabu? Vipi watu wa rangi nyingine kama wahindi wachina na waarabu? Au unadhani mzungu kwa mzungu wanaweza kuzaa mchina? Au kwako wachina na wahindi na wengineo ni wazungu? That issue is more than "mtu mweusi"

Mgalanjuka sina maana hiyo nadhani nikijibiwa hilo nililouliza linaweza kujibu baadhi ya maswali mengine endelea tu kunisaidia maana nafikia sehemu nagota
 
naomba kueleweshwa kwa mwenye ufahamu na hili ni katika kueleweshana
Na vitabu amabayo tulikuwa tunafundishiwa ni vile vyenye picha za adam na hawa na wengine wote ambao inaonyesha kwamba
Walikuwa ni watu weupe ambao niliamini niwazungu. Sasa najiuliza kama original ya adam na hawa walikuwa ni wazungu na ndio tunaaminishwa kwamba walikuwa ni wanadamu wa kwanza

Swali lako zuri sana na pia maswali ni mengi sana mno kujua mtu mweusi alitoka wapi? Jiulize pia kwenye vitabu vya dini tunaona watakatifu wote ni weupe (wazungu) hata pia Malaika ni weupe (wazungu) lakini ukiangalia picha ya Shetani ni Mweusi kama Mkaa kwahiyo uliza pia swali hili je mtu mweusi naye ni kizazi cha SHETANI????
 
@ Easymutant itakua biblia inadanganya maana. Wakati wa adam na hawa hapakua na camera sasa walipatikanaje kupigwa picha? Hizo ni propaganda za wazungu kutaka kuwatawala watu kimawazo na waafrika wameshatawaliwa.

Ktk lugha ya kiarabu neno "adam" maana yake ni kitu cheusi. Kwa hiyo yule aliitwa adam kwakua alikua mweusi.

Ukitaka kuelewa kila jambo. Nakushauri ingia ktk uislam au soma qur-an kwa undani utapata mpaka historia ya kweli sio ile iliyochafuliwa kwa maslah ya wazungu.
 
naomba kueleweshwa kwa mwenye ufahamu na hili ni katika kueleweshana
Naomba lisiwe na chembe za udini japo source yake imetoka kwenye bible bible hivi..
Nikiwa nimekulia na kulelewa katika mazingira ya dini ya kikiristo tulikuwa tukionyeswa vitabu
Na vitabu amabayo tulikuwa tunafundishiwa ni vile vyenye picha za adam na hawa na wengine wote ambao inaonyesha kwamba
Walikuwa ni watu weupe ambao niliamini niwazungu. Sasa najiuliza kama original ya adam na hawa walikuwa ni wazungu na ndio tunaaminishwa kwamba walikuwa ni wanadamu wa kwanza
Kabisa kuishi duniani je mie mtu mweusi nilitoka wapi? Maana siamini mzungu na mzungu wanaweza kuzaa mtu full black kabisa.
Kingine kinachonichanganya je zamani waliruhusiwa kaka na dada kuoana? Maana kama adamu na hawa ndo wakwanza it means waliozaliwa ni watoto je walijijenerate namna gani
Na isitoshe waliozaliwa tunaambiwa walikuwa wa jinsia moja wanaume tupu sasa hapo ndo sielewi kabisa msaada jamani!!!

Kama unaamini Bible wacha nikujibu kwa Bible.

Ni kweli labda ulipokuwa mtoto ulioneshwa picha za Adam na Hawa wakiwa weupe...lakini kwa sasa mambo yamebadilika na si ajabu ukipitia tena vitabu vya aina hiyo hiyo wakati huo uliyooneshwa utaona baadhi yake ambavyo vina picha ya Adam na Hawa weusi tu kama wewe au wakionekana kama Wahindi, Wa-aborigines,Wakorea,Amerindians,Wa-siberians n.k. Kwa kifupi hayo yalikuwa mambo ya kupita tu. Wala sidhani kama kuna mwenye udhibitisho wa rangi haswa ya Adam na Hawa ilikuwaje kwani ukirudi kwenye evolution theory utaambiwa mwanadamu wa kwanza aliishi Africa na hilo litakupa uwezekano mkubwa kuwa alikuwa mweusi au light skin kama baadhi ya Wahabeshi au Wasomali.

Kuhusu kama walioana dada na kaka ni kweli kabisa ndivyo ilivyo kuwa kwani hata baadhi ya wazee wa imani kama Abraham mke wake alikuwa ni dada yake waki-share baba na mama tofauti; soma Gen:20:1-13 utaelewa kidogo kuhusu hilo. Sheria za kukataza ndugu koana zimekuja baada ya Wayahudi kutoka Egypt rejea Lev: 18:1-30 utaona huu ufafanuzi.
Kuhusu kwamba hakukuwa na wasichana na tunaambiwa kuwa walikuwa wanaume tu nadhani hapo umeteleza kidogo.

Biblia walipewa Wayahudi na kwa Wayahudi mara nyingi watoto wa kile hawapewi uzito sana kama wanaume wanavyopewa lakini hilo haliwezi kuwa sababu ya kwamba hakukuwa na watoto wa kike enzi hizo. Hao walikuwepo tena tele. Kwa mfano tunajua Yakobo alikuwa na watoto 12 tena wote wavulana lakini ukumbuke alikuwa nao na wa kike wengi tu mfano wa mtoto wake wa kike ni Dina rejea Gen: 30: 21(lakini ukipenda soma Chapter 30 yote ili uelewe zaidi.)
 
@ Easymutant itakua biblia inadanganya maana. Wakati wa adam na hawa hapakua na camera sasa walipatikanaje kupigwa picha? Hizo ni propaganda za wazungu kutaka kuwatawala watu kimawazo na waafrika wameshatawaliwa.

Ktk lugha ya kiarabu neno "adam" maana yake ni kitu cheusi. Kwa hiyo yule aliitwa adam kwakua alikua mweusi.

Ukitaka kuelewa kila jambo. Nakushauri ingia ktk uislam au soma qur-an kwa undani utapata mpaka historia ya kweli sio ile iliyochafuliwa kwa maslah ya wazungu.

Kama Adam ni kitu cheusi na Koran inasema hivyo hao weupe walitoka wapi? Au unataka tukatae utawala wa wazungu tufuate wa Waarabu? Na kama Bible inadanganya basi Koran ndio funga kazi kwa uongo!

Halafu jaribu kuja na facts na sio ujanja ujanja wa oooh sijiu Koran nini lete vitu detailed ili kama tutakubaliana na wewe tufuate huo Uislam . Siyo una-generelalize tu Biblia inadanganya.
 
VT-05701-491524f5-1.jpg
 
...
Ukitaka kuelewa kila jambo. Nakushauri ingia ktk uislam au soma qur-an kwa undani utapata mpaka historia ya kweli sio ile iliyochafuliwa kwa maslah ya wazungu.
Anahitaji jibu hapa, sasa hadi aingie uisilamu, ajifunze quran halafu aijue kwa undani ndiyo apate jibu, kwa nini usiweke hapa yale uyajuayo kutoka kwenye uisilamu ili ajue jibu la swali lake? Waisilamu bwana, watata kama kilivyo kitabu chao !
 
Ili suhala kulijadili nje ya imani zetu, inaweza kuwia ugumu kidogo, maana karibia sisi sote tumeathirika na hizi imani za dini...!

Kuna maelezo mengi kuhusiana na binadam wa kwanza, karibia imani za dini zote zina amini huwepo wa binadam wa kwanza hapa ulimwenguni...!

Kwa vile tunajuwa kuwa Adam aliumbwa kwa udongo na wasomi wengine wanatuambia kuwa udongo alio umbiwa Adam ni Mweusi, na wengine wanasema kuwa ni wenye rangi tofauti tofauti ndio maana kila mtu anayezalikana naye amekuwa na rangi tofauti tofauti. Hivyo, ndivyo tulivyo pata rangi zetu kutoka kwa baba yetu kwa kurithi.

Wengine wanasema Rangi ya asili ni nyeusi, ndio maana ni rahisi kwa mtu mwenye rangi nyeusi kuwa mweupe, lakini haiwezekana kwa mtu mweupe kubadilika kuwa mweusi... kwa sababu weupe ni photocopy ya weusi...(Joke?).

Wayahudi wa kale walikuwa wanaamini kuwa Mungu aliwauumba watu wa kwanza Adam (mwanamme) na Lilith (mwanamke ila Si Eve) kwa udongo na kwa wakati mmoja, ila Lilith alikataa kuwa chini ya Adam na akaamua kuondoka, baadae alikuja kufanya mapenzi na Malaika mkuu Samael (soma kitabu kinachoitwa: Tree of souls: the mythology of Judaism, By Howard Schwartz, page 218). Baadae tena ndipo Mungu akamuumba Eve (Hawa) kutoka kwenye ubavu wa Adam, na kujaaliwa kupata watoto watatu, Cain, Abel na badae Seth...!

Wasomaji wengi wanajua kisa cha Cain na Abel, Cain alikuja gombana na nduguye kwa wivu na akamuua mdogo wake Abel... Kisa kinaendelea mpaka kufukuzwa kwa Cain na kuamia mji wa Nod, mji ambao unaonekana ulikuwa na watu wakiishi kwani uko Nod, Cain alioa na kupata watoto (Genesis 4), Ukisoma iki kisa kitakuonyesha kuwa Adam inawezekana si binadam wa kwanza kuumbwa... ila ili suhala lina utata mwingi sana...!
 
Anahitaji jibu hapa, sasa hadi aingie uisilamu, ajifunze quran halafu aijue kwa undani ndiyo apate jibu, kwa nini usiweke hapa yale uyajuayo kutoka kwenye uisilamu ili ajue jibu la swali lake? Waisilamu bwana, watata kama kilivyo kitabu chao !

Mpe zake huyo mkuu. Yaani anatudanganya kuwa kitabu chake ndo kinasema kweli wakati hata kukielewa kwenyewe hawakielewi! Wanakaririshwa Kiarabu wala hawaelewi kilichomo! S....ic Verses
 
Kama Adam ni kitu cheusi na Koran inasema hivyo hao weupe walitoka wapi? Au unataka tukatae utawala wa wazungu tufuate wa Waarabu? Na kama Bible inadanganya basi Koran ndio funga kazi kwa uongo!

Halafu jaribu kuja na facts na sio ujanja ujanja wa oooh sijiu Koran nini lete vitu detailed ili kama tutakubaliana na wewe tufuate huo Uislam . Siyo una-generelalize tu Biblia inadanganya.

Point taken mkuu,wakati islam wanadai koran ilishushwa na Mungu,Biblia ilikuwa imeshaandikwa na koran its a copy of bible in arabic.
 
naomba kueleweshwa kwa mwenye ufahamu na hili ni katika kueleweshana
Naomba lisiwe na chembe za udini japo source yake imetoka kwenye bible bible hivi..
Nikiwa nimekulia na kulelewa katika mazingira ya dini ya kikiristo tulikuwa tukionyeswa vitabu
Na vitabu amabayo tulikuwa tunafundishiwa ni vile vyenye picha za adam na hawa na wengine wote ambao inaonyesha kwamba
Walikuwa ni watu weupe ambao niliamini niwazungu. Sasa najiuliza kama original ya adam na hawa walikuwa ni wazungu na ndio tunaaminishwa kwamba walikuwa ni wanadamu wa kwanza
Kabisa kuishi duniani je mie mtu mweusi nilitoka wapi? Maana siamini mzungu na mzungu wanaweza kuzaa mtu full black kabisa.
Kingine kinachonichanganya je zamani waliruhusiwa kaka na dada kuoana? Maana kama adamu na hawa ndo wakwanza it means waliozaliwa ni watoto je walijijenerate namna gani
Na isitoshe waliozaliwa tunaambiwa walikuwa wa jinsia moja wanaume tupu sasa hapo ndo sielewi kabisa msaada jamani!!!
Huwezi kupata ukweli isipokuwa kutoka kwenye Biblia na true science combined.Kukataa ukweli huu ni kwamba you prefer lies.Link ninayokupa itakupa ukweli wa biblia and true science.
Nenda www.bible-truth.org/race.htm. Kuwa mwangalifu na ushauri unaopata kutoka JF hasa kwa mambo kama haya some people in JF ni Freemasons,wanapindisha ukweli ili kumtukuza mungu wao.ambaye ni shetani.It's only the bible and true science which can give you the truth.Ninasema true science makusudi kwasababu kuna ujinga kama evolution ambao uliletwa makusudi ili ku-downgrade kazi ya Mungu ya umbaji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom