Elice Elly
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 1,268
- 1,593
Hivi karibuni kuna Mtu mweusi ametendwa vibaya huko Marekani kitendo kilichozusha fujo Kubwa, huku watu wakikemea kitendo hicho. Lakini cha ajabu ndani ya Afrika Waafrika wenyewe wakinyanyasana kwa kiasi kikubwa sana.
Vitendo Vya kunyanyasani ndani ya Afrika ni jambo la kawaida lakini cha hakuna nguvu ya pekee ya kukemea vitendo hivi. Tumeshuhudia mambo mengi ya kikatili wanayo fanyiwa watu tena matendo haya yanatendwa na watu wenye mamlaka. Kuna watu wanauawa wengine wanatekwa, wengine wananyanyaswa kwa namna mbali mbali, lakini hakuna nguvu ya pekee ya kukemea matendo hayo.
Huko Afrika ya kusini serikali ya makaburu iliwanyanyasa sana Waafrika, kiasi kwamba Waafrika wote tuliungana kukemea vitendo hivyo, cha ajabu matendo Yale Yale yaliyotendwa na makaburu leo Waafrika wanayatenda tena kwa hali ya juu,kiasi kwamba tumewazidi wale tuliokuwa tunawakeme.
Muda Fulani najiuliza inamaana tunachukia kutendewa vibaya na wazungu huku tukifurahia kutendeana vibaya sisi kwa sisi?
Vitendo Vya kunyanyasani ndani ya Afrika ni jambo la kawaida lakini cha hakuna nguvu ya pekee ya kukemea vitendo hivi. Tumeshuhudia mambo mengi ya kikatili wanayo fanyiwa watu tena matendo haya yanatendwa na watu wenye mamlaka. Kuna watu wanauawa wengine wanatekwa, wengine wananyanyaswa kwa namna mbali mbali, lakini hakuna nguvu ya pekee ya kukemea matendo hayo.
Huko Afrika ya kusini serikali ya makaburu iliwanyanyasa sana Waafrika, kiasi kwamba Waafrika wote tuliungana kukemea vitendo hivyo, cha ajabu matendo Yale Yale yaliyotendwa na makaburu leo Waafrika wanayatenda tena kwa hali ya juu,kiasi kwamba tumewazidi wale tuliokuwa tunawakeme.
Muda Fulani najiuliza inamaana tunachukia kutendewa vibaya na wazungu huku tukifurahia kutendeana vibaya sisi kwa sisi?