Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,240
- 9,527
Zoezi la kutaka kuonyesha kama siasa ni vita na upinzani ni uadui limeshika kasi hapa nchini!
Uwekezaji mkubwa umefanyika kwenye hili zoezi na wananchi na viongozi kwa ujumla wamejikuta wakiingia katika huu mtego bila kujua lengo la muasisi wa zoezi.
Watanzania wamefungamana sana;
1. Kifamilia.
2. Kidini
3. Kikabila
4. Kibiashara
5. Shuhuli za kijamii kama vile sherehe na misiba.
Ukitaka kuwagawa kwa kutumia siasa, utafanyaje kwenye mahusiano ya kifamilia, kidini, kikabila, kibiashara na shughuli za kijamii?
Leo chakula alichokua anakula Lema kimehamishiwa kwa Gambo kwa kutumia nguvu. Gambo mtaani ni jirani yangu na tunashirikiana nae pamoja na familia yake kwenye shughuli za kijamii. Lema ni shemeji yangu maana nimeoa kwao.
Sasa ukitaka kuonyesha Lema ni mtu mbaya sana na Gambo ni mtu mzuri sana, mimi nitasimamia upande gani? Makwazo ni budi kuwapo ila ole wake anayeyaleta. Yampasa kufungwa jiwe la kusagia shingoni mwake na atumbukizwe kwenye kina kirefu cha maji!
Ni muda sasa wa kutafakari lengo la muasisi huyu wa siasa za kibaguzi. Ilikuwaje tukaishi pamoja na kwa umoja na upendo chini ya Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete?
Nini kimeenda vibaya?
Tumefikaje hapa?
Uwekezaji mkubwa umefanyika kwenye hili zoezi na wananchi na viongozi kwa ujumla wamejikuta wakiingia katika huu mtego bila kujua lengo la muasisi wa zoezi.
Watanzania wamefungamana sana;
1. Kifamilia.
2. Kidini
3. Kikabila
4. Kibiashara
5. Shuhuli za kijamii kama vile sherehe na misiba.
Ukitaka kuwagawa kwa kutumia siasa, utafanyaje kwenye mahusiano ya kifamilia, kidini, kikabila, kibiashara na shughuli za kijamii?
Leo chakula alichokua anakula Lema kimehamishiwa kwa Gambo kwa kutumia nguvu. Gambo mtaani ni jirani yangu na tunashirikiana nae pamoja na familia yake kwenye shughuli za kijamii. Lema ni shemeji yangu maana nimeoa kwao.
Sasa ukitaka kuonyesha Lema ni mtu mbaya sana na Gambo ni mtu mzuri sana, mimi nitasimamia upande gani? Makwazo ni budi kuwapo ila ole wake anayeyaleta. Yampasa kufungwa jiwe la kusagia shingoni mwake na atumbukizwe kwenye kina kirefu cha maji!
Ni muda sasa wa kutafakari lengo la muasisi huyu wa siasa za kibaguzi. Ilikuwaje tukaishi pamoja na kwa umoja na upendo chini ya Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete?
Nini kimeenda vibaya?
Tumefikaje hapa?