Mtu Kwao


Wana JF,

Hapa ndiyo unaona jinsi Nyang'au wanavyojua kujitangaza ingawa hawana kitu cha kuonyesha. Si mmeona viTembo na vijiFisi uchwara kwenye ardhi kame na udongo mwekundu!!!?

Hivi kwetu Bongo, hao wenye dhamana ya kutangaza maliasili na tamaduni zetu ni mpaka waende kwenye maonyesho na si kutengeneza audiovisial kama hizi?? Wajemeni hivi sisi tuna laana ya namna gani? Audiovisual kama hizi hazihitaji gharama kubwa. ni kiasi cha kutafuta wataalam wa shooting na kutengeneza kitu kama kwa gharama ndogo kabisa.

Ujinga wetu, utasikia wanaohusika wakilalama eti ooh hakuna tunataka pesa nyingi za kwenda ulaya kujitangaza. Kwa kutengeneza kitu kama hiki na kuweka kwenye internet mamilioni ya watu duniani watakuwa wamepata tangazo hili na kujionea tamaduni na vivutio vyetu.

Hivi kwa nini mungu asiwauwe wote wanaoi didimiza nchi yetu kwa kupenda ubinafsi?
 
Heshima yako Semazumba.

Mimi sikuona kama ni kitu cha utalii sana. Nimeona kama ni suala la economic aid pale alipoenda naye dampo. Halafu nimekapenda haka kabinti kwa kuweza kuongea lugha ya kimasai kifasaha, watoto wetu wengi hawawezi kuongea zaidi ya sentensi moja ya kilugha bila ya kuchanganya kiswahili au kiingereza.
Ila nafikiri hii kitu ilipangwa kwa sababu sidhani kama wanakijiji ( kule kijijini) na akina mama pale Nairobi wangeweza kujitayarisha kimapokezi bila ya kujua kilichokuwa kinaendelea.
Nimeipenda hii program na sijutii kupoteza dakika zangu ishirini na tano nilizotumia kuiangalia.
 
Hata mimi nimeipenda, sidhani kama ni sawa kusema eti jirani zetu waKenya wanatumia hii opportunity kutangaza utalii. Hiki ni kipindi tu, kama lilivyo jina lake, cha kuonesha watu wa mataifa tofauti sehemu zao za asili.

Nimependa huyo msichana ambavyo hajasahau alikotoka.

Ila sijaelewa ni wachumba au marafiki tu (not that it matters) - wanaonekana wana urafiki wa dhati
 
Kumbe Nairobi kuna watu wanaishi kwa taabu zaidi kuliko wale wa Dar? Nimekuwa naijua Nairobi upande mzuri tu, sikujua kuwa kuna sehemu watu wanaishi kwa kuchakura kwenye madampo ya uchafu.
 
Binafsi nimefurahishwa na huyo msichana kuwa mkweli namuwazi juu ya kabila lake na utamaduni wao pamoja na kuogea lugha ya wazazi wake ,bila kuona aibu ,ukingalia hapa ketu Tanzania tumekuwa tafauti unakuta mtu hataki kusikia kabila lake au kuongea lugha ya kabila lake,eti anaona aibu ,jamani chimbuko lake mtu ni muhimu haya yote ya Jiji ni hanasa za hapa na pale .
 
Kuhusu kama ni wapenzi au la, imenikumbusha enzi za kusoma kitabu cha Wakati Ukuta, wakati mhusika mmoja alisema hakuna urafiki kati ya mtoto wa kike na wa kiume. Kwenye mila zetu hasa katika mazingara ya vijijini, watu huwa wanachanganyikiwa ukimpeleka rafiki wa jinsia tofauti. Nilihisi kuchanganyikiwa huko kutokana na baadhi ya maswali ya babu.Kwa mfano, babu aliuliza swali kuwa je unafaidika na kuwa na binti yetu huko kwenu? ( kijana alijibu kwa njia ambayo mimi nilidhani amekwepa swali. Alisema kitu kama oh ni vizuri kuwa binti anasoma na anajitahidi. ( sijui hiyo lugha lakini binti ndiye aliyekuwa anatafsiri maswali ya babu yake.)

Na kuna mahali kijana anasema kuwa aliogopa babu asije akamuweka kwenye spot.
So in my opinion there is something cooking, I just don't know whether it is a cup of tea or sufuria la makande.
 
Back
Top Bottom