Mtu huyu akisimama na mgombea wa CCM mwaka 2025, ni lazima CCM tuangukie pua

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,860
12,291
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.

Ndugu wana JF wenzangu na watanzania wenzangu, ili chama cha CCM kiweze kushindwa katika uchaguzi mkuu wa 2025 au 2030, yanahitajika mambo matatu.

1) Kwanza: kinahitajika chama imara cha upinzani chenye sera nzuri, zinazoeleweka na kutekelezeka. Chama hicho kiwe na sura ya kitaifa, kiwe na viongozi wakweli, wenye maono na misimamo thabiti ya kuikomboa nchi. Kiwe na mifano hai ya utekelezaji wa sera zake kupitia chama husika ili kiweze kuaminika machoni mwa watanzania wengi.
a) Sio mtu useme chama chetu kina misingi ya demokrasia wakati mwenyekiti wa chama ambacho kingekuwa mfano wa demokrasia hiyo ana miaka 20 madarakani.​

b) Sio mtu useme chama chetu ni cha maendeleo, wakati wanaoendelea katika chama ni mwenyekiti wa chama taifa na genge lake, huku chama chenyewe kikiwa hakina hata ofisi ya kufanyika mkutano wa ndani.​

c) Sio mtu useme chama chetu kitasimamia utawala bora na haki, huku ndani ya chama chenyewe hakuna anaeweza kuongelea lolote mbele ya mwenyekiti wa chama au makamu wake.​

2) Pili: Anahitajika kuchaguliwa mgombea ambae hana makandokando ya uongo, uoga, unafiki na mwenye uwezo wa kweli wa kusimamia sera za chama chake bila kuyumbishwa na mtu yoyote iwe ndani ya chama au nje ya chama.

a) Sio kiongozi anakuwa na kauli za kilaghailaghai kwa maslahi yake binafsi ya kisiasa, na kiuongozi (kama tunavyoona hapo chini pichani) bila kujali madhara yatokanayo na ulaghai huo. Mtu wa aina hii ni ngumu kuchaguliwa maana watanzania wa sasa sio wale wa 2001, kule Zanzibar ambapo watu walikufa, kujeruhiwa na kufungwa, huku muhusika aliepiganiwa (aliekuwa katibu mkuu wa chama, na mgombea wa upinzani) akiwa Saudia Arabia kula tende na maswaiba zake. Mgombea akiwa hana msimamo thabiti wa kusimamia sera au hoja zake mwenye, basi hata Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Marekani ikija kusimamia uchaguzi bado ataangukia pua tu.​

3) Tatu: Tume huru isiyoegemea upande wowote wa kisiasa. Tume iwe na viongozi kutoka vyama mbali mbali vya kisiasa na kiraia ili kujenga sura ya utaifa katika tume hiyo.

Ni hayo tu ninayoyaona mimi, katika kuijenga Tanzania bora zaidi ya kesho.

Asanteni sana.

E5NpJDaWEAALjca.jpeg
Screenshot_20220605-165724.jpg
Screenshot_20220605-082514_1.jpg
images (1).jpeg
images (8).jpeg

 
Hata mletewe mtu mwema sana,tena malaika bado ni yaleyale tu.Ulaghai,ubabe,matumizi ya nguvu za majeshi,tume isiyo huru na utapeli ni mwingi.Halafu,siku vichwa-panzi wakiamua kutupa ujuha wao pembeni nchi itaondokana na jinamizi la CCM.
Nguvu ya umma ikiamua hata serikali ikitumia vyombo vya ndan na nje vya ulinzi itashindwa tu. Unakumbuka enzi ya CUF 2000 to 2005, pamoja na serikali kutumia vyombo vyote vya dola kudhibiti chama hicho, lkn bado vijana walisimama imara katika kukipigania chama hicho.

Unakumbuka CDM 2005 to 2015, pamoja na serikali kujaribu kukidhibiti chama na nguvu ya upinzani, lkn ilishindwa kutokana na misimamo thabiti ya wana CDM na upinzani kwa ujumla katika kupigania haki yao. Ila baada ya lile timbwili la Lowasa mwaka 2015, vijana wengi walivunjika moyo na kuamua kukaa mbali na mambo ya siasa baada ya kugundua kuwa 95% ya wapinzani wa Tanzania hawako serious na ajenda zao. Ndio maana kuanzia 2015 to 2020 serikali ilionekana kudhibiti upinzani vilivyo, kwani wale waliokuwa wanapigania upinzani huko nyuma kufa kupona wali give up kujihusisha na siasa uchwara again.
 
Unajitoa akili sio?

Kinachofanya ccm msiangukie pua ni kukosekana huyo mtu uliyemchora kichwani kwako au ni litume lenu mliloliweka la uchaguzi?

Si mjaribu kuwa na tume huru Kisha mpime.

Ila haki nawaambia mtachomwa moto jehanam nyinyi hamtaamini!
Tuchomwe moto kwa lipi mkuu? Ni nani mkamilifu hapa chini ya jua.
Usisahau Mungu ni wetu sote brother.
 
Nguvu ya umma ikiamua hata serikali ikitumia vyombo vya ndan na nje vya ulinzi itashindwa tu. Unakumbuka enzi ya CUF 2000 to 2005, pamoja na serikali kutumia vyombo vyote vya dola kudhibiti chama hicho, lkn bado vijana walisimama imara katika kukipigania chama hicho.

Unakumbuka CDM 2005 to 2015, pamoja na serikali kujaribu kukidhibiti chama na nguvu ya upinzani, lkn ilishindwa kutokana na misimamo thabiti ya wana CDM na upinzani kwa ujumla katika kupigania haki yao. Ila baada ya lile timbwili la Lowasa mwaka 2015, vijana wengi walivunjika moyo na kuamua kukaa mbali na mambo ya siasa baada ya kugundua kuwa 95% ya wapinzani wa Tanzania hawako serious na ajenda zao. Ndio maana kuanzia 2015 to 2020 serikali ilionekana kudhibiti upinzani vilivyo, kwani wale waliokuwa wanapigania upinzani huko nyuma kufa kupona wali give up kujihusisha na siasa again.
Subiri hali ya maisha iendelee kuwa ngumu zaidi na zaidi upinzani utakuwepo tu
 
Subiri hali ya maisha iendelee kuwa ngumu zaidi na zaidi upinzani utakuwepo tu !!
Inshaallah. Ki ukweli kuna watu wameshaichoka CCM, ila sasa hawaoni mbadala wa chama cha kuitoa CCM madarakani. Vyama vyote ukivichunguza havina tofauti na CCM mpaka inafikia kipindi watu wanahisi huenda huu upinzani ulitengenezwa maalum na CCM ili kuihadaa dunia kuhusu demokrasia nchini. Kwahiyo misaada inayoletwa na mabeberu kwa ajili ya kukuza na kuimarisha demokrasia inaliwa na wajanja wachache walio ndani ya serikali, CCM na upinzani butu.
 
Mbona hatuulizi juu Mzee Mrema kwani naye ana muda mrefu sana ktk harakati zake.
Kwanini iwe shida kwa huyu anayejenga Tasisi nakuonekana imara katka ushindani kwani tukumbuke ndo mshindani wa kweli na wa mfano wa kuigwa.
Tukumbuke sio mwepesi ndo maana hoja zinazomhusu haziishi kutoka kwetu.
Mfano ni madhila aliyoyapitia yy na wanaomzunguka.
Je ni nani mwingine aliyeyapitia aliyoyapitia?
Tuje na hoja dhabiti tutaeleweka vizuri sana.
 
Back
Top Bottom