JosM
JF-Expert Member
- Oct 11, 2008
- 679
- 17
huyu jamaa ni mkazi mwa Mbezi Beach eneo la Makonde Juu /Kipongoso anajulikana kwa jina la ALLuh
na Exuper Kachenje
WAKAZI wa maeneo ya Mwananyamala wilayani Kinondoni jana walimiminika katika hospitali ya Mwananyamala, kutaka kumuona mgonjwa aliyelazwa ambaye anadaiwa kuwa alibadili jinsia yake na kuwa mwanamke.
Imeelezwa kuwa mgonjwa huyo aliokotwa na polisi kwenye ufukwe wa Bahari ya Hindi, Mbezi jijini Dar es Salaam. Alikuwa hajitambui na habari zaidi zinasema kuwa alikuwa amebakwa.
Habari za kuwepo katika hospitali hiyo mtu wa aina hiyo aliyewekewa viungo vya kike, zilianza kusambaa katika maeneo ya Mwananyamala na vitongoji vingine vya Jiji la Dar es salaam majira ya saa 4:00 asubuhi jana.
Mwananchi ilifika hospitalini hapo saa 6:05 na kukuta watu wakisimuliana kuhusu mtu huyo huku wakionyesha kustaajabishwa na kushtushwa na habari hizo.
Loh, dunia kweli imekwisha, wanasema ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni, tumesikia yupo mgonjwa wa aina hiyo amelazwa hapo wodi namba tatu, lakini tunazuiwa kumuona kazungushiwa pazia, alisema mmoja wa wakazi hao akimsimulia mwenzake.
Ndani ya wodi namba tatu ambayo inashughulikia upasuaji na matatizo ya jinsia (Ward III Gyne and Surgical), kulikuwa na watu wengi ambao walikuwa wakionekana kuwa na hamasa ya kumuona mtu huyo, ambaye Mwananchi ilidokezwa kuwa anaitwa Victoria.
Alikuwa amelala kwenye kitanda ambacho kilizungushiwa pazia na kubandikwa tangazo linalozuia mtu kuingia ndani na kumwona.
"Si ruhusa mtu yoyote kuinga katika chumba hiki, lilisomeka tangazo lililobandikwa katika pazia.
Mwananchi ilifanikiwa kumuona Victoria ambaye utaifa wake haukutambulika mara moja, lakini ni mtu mweupe na ambaye ametoboa masikio na nywele zikiwa za asili ya Kiasia.
Habari za ndani kutoka hospitali hiyo zinasema kifuani Victoria ana matiti makubwa ambayo muuguzi mmoja alidokeza kuwa yanaonekana kuwa ya kutengeneza kwa sindano.
Alisema nia ya kuzungushia pazia kitanda chake ni kuzuia watu wasiendelee kumshangaa na pia kuwaondolea hofu wagonjwa wengine ambao ni wanawake waliolazwa wodi hiyo.
Habari zaidi zinasema kuwa ingawa Victoria hajaweza kuzungumza, hali yake imeanza kuwa nzuri na ameanza kupata fahamu kwa kufumbua macho na awaonapo wanaume huwafurahia zaidi kuliko wanawake.
Habari zaidi zinaeleza kuwa Victoria alifikishwa hospitalini hapo saa 11:00 alfajiri jana na polisi baada ya kuokotwa katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, Mbezi akiwa hajitambui na inahisiwa alibakwa na watu wasiojulikana.
Hii ni Police case (suala la kipolisi), aliletwa na polisi sikumbuki wa kituo gani kilisema chanzo cha habari hospitalini hapo.
Inavyoonekana Victoria alifanyiwa uhuni, watu walimbaka na kumtelekeza ufukweni. Nadhani maeneo ya Mbezi Beach kuna matatizo... waandishi fuatilieni, hii ni mara ya pili. Kuna wakati aliokotwa mtu katika kali hiyo maeneo hayo akaletwa hapa na alikufa hakuwa na ndugu.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, mganga mkuu wa hospitali ya Mwananyamala, Dk Suleiman Mtani alisema anachojua yeye aliyepokelewa ni mgonjwa kama wengine na wajibu wao ni kumpatia huduma inayostahili.
Ni kweli kuna mgonjwa amepokelewa leo alfajiri, akiwa hajitambui, mpaka muda huu hajaweza kuzungumza. Lakini ninachoweza kuwaambia ni kuwa amepokelewa kama wagonjwa wengine na jukumu letu ni kumsaidia kwa kumpatia matibabu si kutoa taarifa zake, alisema Dk. Mtani.
Maadili ya kazi yetu, ni kulinda utu na heshima ya mgonjwa, madaktari hawatoi taarifa za mgonjwa kwa mtu asiyehusika. Tafadhali naomba tuzingatie hilo, ni kiapo cha kazi yetu.
Hata hivyo alisema kama ni kupata taarifa kamili za mgonjwa huyo polisi ndiyo inaweza kuwa nazo kwani ndiyo iliyomfikisha hospitalini hapo na kuwa hakuna taarifa zake zaidi kwa sababu hawezi kuongea pia hadi jana mchana ndugu zake hawajajitokeza.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye alisema: Nipo nje ya Dar es Salaam, mtafute kaimu wangu afande Damas Masinde.
Alipotafutwa, Masinde alithibitisha kuokotwa kwa mtu huyo, lakini akasema uchunguzi unaendelea kujua nini kilimpata.
Askari wetu wa kituo cha Kawe walimwokota mtu huyo na kumpeleka Hospitali ya Mwanayamala. Ngoja nikwambie ukweli ndugu yangu, mchana nimemtuma mkuu wa upelelezi kwenda pale kujua zaidi habari za mtu huyo, lakini kwa kuwa bado hajapata fahamu madaktari na manesi hawakumruhusu kumuona, alisema Masinde.
Alifafanua kwamba askari wake wanaendelea kufuatilia na atakapopata nafuu atafanyiwa uchunguzi na taarifa itatolewa.
Hatuna uhakika amepatwa na nini. Tunaendelea kufuatilia tukipata ukweli tutatoa taarifa. Kwa sasa siwezi kusema lolote, alisema afande Masinde.
na Exuper Kachenje
WAKAZI wa maeneo ya Mwananyamala wilayani Kinondoni jana walimiminika katika hospitali ya Mwananyamala, kutaka kumuona mgonjwa aliyelazwa ambaye anadaiwa kuwa alibadili jinsia yake na kuwa mwanamke.
Imeelezwa kuwa mgonjwa huyo aliokotwa na polisi kwenye ufukwe wa Bahari ya Hindi, Mbezi jijini Dar es Salaam. Alikuwa hajitambui na habari zaidi zinasema kuwa alikuwa amebakwa.
Habari za kuwepo katika hospitali hiyo mtu wa aina hiyo aliyewekewa viungo vya kike, zilianza kusambaa katika maeneo ya Mwananyamala na vitongoji vingine vya Jiji la Dar es salaam majira ya saa 4:00 asubuhi jana.
Mwananchi ilifika hospitalini hapo saa 6:05 na kukuta watu wakisimuliana kuhusu mtu huyo huku wakionyesha kustaajabishwa na kushtushwa na habari hizo.
Loh, dunia kweli imekwisha, wanasema ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni, tumesikia yupo mgonjwa wa aina hiyo amelazwa hapo wodi namba tatu, lakini tunazuiwa kumuona kazungushiwa pazia, alisema mmoja wa wakazi hao akimsimulia mwenzake.
Ndani ya wodi namba tatu ambayo inashughulikia upasuaji na matatizo ya jinsia (Ward III Gyne and Surgical), kulikuwa na watu wengi ambao walikuwa wakionekana kuwa na hamasa ya kumuona mtu huyo, ambaye Mwananchi ilidokezwa kuwa anaitwa Victoria.
Alikuwa amelala kwenye kitanda ambacho kilizungushiwa pazia na kubandikwa tangazo linalozuia mtu kuingia ndani na kumwona.
"Si ruhusa mtu yoyote kuinga katika chumba hiki, lilisomeka tangazo lililobandikwa katika pazia.
Mwananchi ilifanikiwa kumuona Victoria ambaye utaifa wake haukutambulika mara moja, lakini ni mtu mweupe na ambaye ametoboa masikio na nywele zikiwa za asili ya Kiasia.
Habari za ndani kutoka hospitali hiyo zinasema kifuani Victoria ana matiti makubwa ambayo muuguzi mmoja alidokeza kuwa yanaonekana kuwa ya kutengeneza kwa sindano.
Alisema nia ya kuzungushia pazia kitanda chake ni kuzuia watu wasiendelee kumshangaa na pia kuwaondolea hofu wagonjwa wengine ambao ni wanawake waliolazwa wodi hiyo.
Habari zaidi zinasema kuwa ingawa Victoria hajaweza kuzungumza, hali yake imeanza kuwa nzuri na ameanza kupata fahamu kwa kufumbua macho na awaonapo wanaume huwafurahia zaidi kuliko wanawake.
Habari zaidi zinaeleza kuwa Victoria alifikishwa hospitalini hapo saa 11:00 alfajiri jana na polisi baada ya kuokotwa katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, Mbezi akiwa hajitambui na inahisiwa alibakwa na watu wasiojulikana.
Hii ni Police case (suala la kipolisi), aliletwa na polisi sikumbuki wa kituo gani kilisema chanzo cha habari hospitalini hapo.
Inavyoonekana Victoria alifanyiwa uhuni, watu walimbaka na kumtelekeza ufukweni. Nadhani maeneo ya Mbezi Beach kuna matatizo... waandishi fuatilieni, hii ni mara ya pili. Kuna wakati aliokotwa mtu katika kali hiyo maeneo hayo akaletwa hapa na alikufa hakuwa na ndugu.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, mganga mkuu wa hospitali ya Mwananyamala, Dk Suleiman Mtani alisema anachojua yeye aliyepokelewa ni mgonjwa kama wengine na wajibu wao ni kumpatia huduma inayostahili.
Ni kweli kuna mgonjwa amepokelewa leo alfajiri, akiwa hajitambui, mpaka muda huu hajaweza kuzungumza. Lakini ninachoweza kuwaambia ni kuwa amepokelewa kama wagonjwa wengine na jukumu letu ni kumsaidia kwa kumpatia matibabu si kutoa taarifa zake, alisema Dk. Mtani.
Maadili ya kazi yetu, ni kulinda utu na heshima ya mgonjwa, madaktari hawatoi taarifa za mgonjwa kwa mtu asiyehusika. Tafadhali naomba tuzingatie hilo, ni kiapo cha kazi yetu.
Hata hivyo alisema kama ni kupata taarifa kamili za mgonjwa huyo polisi ndiyo inaweza kuwa nazo kwani ndiyo iliyomfikisha hospitalini hapo na kuwa hakuna taarifa zake zaidi kwa sababu hawezi kuongea pia hadi jana mchana ndugu zake hawajajitokeza.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye alisema: Nipo nje ya Dar es Salaam, mtafute kaimu wangu afande Damas Masinde.
Alipotafutwa, Masinde alithibitisha kuokotwa kwa mtu huyo, lakini akasema uchunguzi unaendelea kujua nini kilimpata.
Askari wetu wa kituo cha Kawe walimwokota mtu huyo na kumpeleka Hospitali ya Mwanayamala. Ngoja nikwambie ukweli ndugu yangu, mchana nimemtuma mkuu wa upelelezi kwenda pale kujua zaidi habari za mtu huyo, lakini kwa kuwa bado hajapata fahamu madaktari na manesi hawakumruhusu kumuona, alisema Masinde.
Alifafanua kwamba askari wake wanaendelea kufuatilia na atakapopata nafuu atafanyiwa uchunguzi na taarifa itatolewa.
Hatuna uhakika amepatwa na nini. Tunaendelea kufuatilia tukipata ukweli tutatoa taarifa. Kwa sasa siwezi kusema lolote, alisema afande Masinde.