Swadakta, ila sasa na sisi ndio tushajizoelea masikini ya Mungu. Tunashukuru Mkuu kwa kuanzisha hii
Jamani mwenzenu mbona nilikwisha jiandaa kuvumilia tu!
Kwasasa mtoto wangu ansome Shule ya Msingi Mburahati, anakaa kwa shangazi yake Kigogo. Akimaliza shule ya msingi atakwenda soma shule moja ya sekondari za kata Kule Ntwara inayofundishwa na walimu" Voda-fasta".
Kuhusu chuo sina uhakika kama atasoma,labda kama kama nafasi za ualimu zitakuwa bado hazijaisha aende angalau ule wa shule za msingi.
nachoomba ni kwamba asiumwe kipindi chote hicho.
Akiwa shuleni nimemwambia mi sina hela ya kumpa kila siku eti anunulie chipsi na maji ya chupa. Nimemwambia yeye hata shangazi yake kuwa mihogo mitano ya sh 50 na maji ya kiroba(cha kupuliza) yanatosha.
Waziri wa Elimu au Afya hatakuwa na uchungu wa kubadili hali ya shule au hospitali wakati hana mtoto wake anayesoma au kupata matibabu sehemu hizo, viongozi tuache unafiki