Mtoto wa ujanani!

CONSHUMA

New Member
Sep 15, 2011
2
0
wandugu, nilipata mtoto na binti mmoja miaka kadhaa iliyopita, hatukuoana wala kuwahi kuishi pamoja, nilimchukua mtoto akiwa na miaka miwili (pls dont ask why)na nilimlea mwenyewe hadi nilipooa, hii ikiwa ni miaka miwili na nusu baadae, mke wangu alimkubali na kumlea mtoto kwa mapenzi yote kiasi kwamba ni wachache mno ambao wanafahamu kuwa yeye sie mama yake mzazi, hata mtoto na wadogo zake hawalifahamu hilo na baadhi ya ndugu zangu pia. mama mzazi wa mtoto alishaolewa na ana maisha yake kwa mumewe na watoto wao na tuna mawasiliano ya msimu kuhusu mtoto, hajawahi kumuona mwanae kwa zaidi ya miaka nane sasa! tatizo linakuja ni kwamba mtoto amekua na ana shughuli mbeleni ambayo sidhani kama itakuwa jambo la busara mama yake kutohudhuria au kutopata taarifa, je mtoto, wadogo zake, na mama yake(mke wangu) watalipokeaje?!nachelea kufanya lolote litakaloikosesha familia yangu amani, i love my family na siko tayari kuona hili litokee,je nimpotezee tu mama yake bila kumfahamisha? but in otherside ana haki kwani ni mwanae! ni wakati gani muafaka wa kumuweka wazi mtoto kuhusu hili au nalo nilipotezee hadi atakapokuja gundua mwenyewe mbele ya safari??seriosly hili linanitatiza na noamba ushauri wako..tafadhali usinihikumu kwa makosa ya nyuma, nakaribisha ushauri wako..
 
Kwa kweli mwambie tu mama yake, sababu badae huyo mtoto anaweza kuja uliza, na pia kila mtoto ana haki kwa wazazi wake wote, naona ni jambo la busara mama yake akiambiwa, pia kabla hujamwambia mwambie mwenzako uone atalichukuliaje hili ukiona limeleta makashehe makubwa basi tupilia mbali wazo la kumleta huyo mama
 
Usimwalike kabisa, alikuwa wapi siku zote atokee kwenye sherehe tu, ulimwalika kumpeleka mtoto siku ya kwanza shuleni? ulimwalika nakumuita wakati mtoto analia usiku mnambembeleza, wakati nyie mmebanwa na shughuli mtoto hana wa kubaki nae mlimuita, kwa kweli usimkwaze binti wa watu huyo ndio mama yake
 
wandugu, nilipata mtoto na binti mmoja miaka kadhaa iliyopita, hatukuoana wala kuwahi kuishi pamoja, nilimchukua mtoto akiwa na miaka miwili (pls dont ask why)na nilimlea mwenyewe hadi nilipooa, hii ikiwa ni miaka miwili na nusu baadae, mke wangu alimkubali na kumlea mtoto kwa mapenzi yote kiasi kwamba ni wachache mno ambao wanafahamu kuwa yeye sie mama yake mzazi, hata mtoto na wadogo zake hawalifahamu hilo na baadhi ya ndugu zangu pia. mama mzazi wa mtoto alishaolewa na ana maisha yake kwa mumewe na watoto wao na tuna mawasiliano ya msimu kuhusu mtoto, hajawahi kumuona mwanae kwa zaidi ya miaka nane sasa! tatizo linakuja ni kwamba mtoto amekua na ana shughuli mbeleni ambayo sidhani kama itakuwa jambo la busara mama yake kutohudhuria au kutopata taarifa, je mtoto, wadogo zake, na mama yake(mke wangu) watalipokeaje?!nachelea kufanya lolote litakaloikosesha familia yangu amani, i love my family na siko tayari kuona hili litokee,je nimpotezee tu mama yake bila kumfahamisha? but in otherside ana haki kwani ni mwanae! ni wakati gani muafaka wa kumuweka wazi mtoto kuhusu hili au nalo nilipotezee hadi atakapokuja gundua mwenyewe mbele ya safari??seriosly hili linanitatiza na noamba ushauri wako..tafadhali usinihikumu kwa makosa ya nyuma, nakaribisha ushauri wako..

mna mawasiliano ya msimu lakini hajawahi kuona mtoto wake kwa zaidi ya miaka 8?????
 
We mkaushie huyo mama asije coz kwenye hiyo sherehe kunaweza kukawa na majonz na sio furaha tena.Na utafute siku nyingne uliweke wazi kwa familia yako coz ukiifuga hiyo siri utajikuta mwanao atafikili wewe ni mbaya na ulimterekeza mama yake na akimfuata mama yake yeye atajitetea kwa jibu rahis tu BABA YAKO HAKUTA NIWE KARIBU NAWE na chuki zitaflow kuja kwako.POLE SANA KWA WAKATI MGuMU
 
Pole sana ndugu, mkeo amesemaje kuhusu hilo au bado hujaongea nae?
Naomba umpe mkeo nafasi ya kuwa mwamuzi katika hili.
 
Kwa mimi nashauri anza na mkeo kwanza then mkimaliza muongee na mtoto kwa pamoja then feedback ya hapo itakupa go ahead ya either umuite huyo mama au la though kwa busara ni vizuri mama akawepo ashuhudie mwanae akipokea hiyo baraka!
 
mna mawasiliano ya msimu lakini hajawahi kuona mtoto wake kwa zaidi ya miaka 8?????
Hapo ndipo na mie nimejiuliza, hayo mawasiliano ni ya juu ya nini, kuna wanawake wana roho ngumu sana, mtoto umeingia leba mwenyewe usimuone miaka nane? halafu unataka kwenda kwenye sherehe, huyu mama ni mjinga wala hastahili kwenda kwenye hiyo sherehe ata mconfuse tu mtoto keshazoea maisha yake
 
wandugu, nilipata mtoto na binti mmoja miaka kadhaa iliyopita, hatukuoana wala kuwahi kuishi pamoja, nilimchukua mtoto akiwa na miaka miwili (pls dont ask why)na nilimlea mwenyewe hadi nilipooa, hii ikiwa ni miaka miwili na nusu baadae, mke wangu alimkubali na kumlea mtoto kwa mapenzi yote kiasi kwamba ni wachache mno ambao wanafahamu kuwa yeye sie mama yake mzazi, hata mtoto na wadogo zake hawalifahamu hilo na baadhi ya ndugu zangu pia. mama mzazi wa mtoto alishaolewa na ana maisha yake kwa mumewe na watoto wao na tuna mawasiliano ya msimu kuhusu mtoto, hajawahi kumuona mwanae kwa zaidi ya miaka nane sasa! tatizo linakuja ni kwamba mtoto amekua na ana shughuli mbeleni ambayo sidhani kama itakuwa jambo la busara mama yake kutohudhuria au kutopata taarifa, je mtoto, wadogo zake, na mama yake(mke wangu) watalipokeaje?!nachelea kufanya lolote litakaloikosesha familia yangu amani, i love my family na siko tayari kuona hili litokee,je nimpotezee tu mama yake bila kumfahamisha? but in otherside ana haki kwani ni mwanae! ni wakati gani muafaka wa kumuweka wazi mtoto kuhusu hili au nalo nilipotezee hadi atakapokuja gundua mwenyewe mbele ya safari??seriosly hili linanitatiza na noamba ushauri wako..tafadhali usinihikumu kwa makosa ya nyuma, nakaribisha ushauri wako..

mkuu unatakiwa kufanya kama kwenye harusi ya tabata bi harusi kumtambulisha kidume wake wa kwanza..
 
Nakumbuka maneno ya Marehemu Bakari Abedi aliyekuwa bingwa wa lugha ya Kiswahili. Siku moja kulikuwa na mjadala kuhusu mama wa kambo na yeye akasema "mama wa kambo siku zote hutokea mtoto akifikia kwenye umri wa kuanzia miaka 14 na kuendelea. Hapo ndiyo utamkuta mama mzazi analeta maneno na kumwambia yule mtoto kwamba huyo ni mama wa kambo, hakupendi na mengine tele. Lakini alipokuwa mdogo na akihitaji kuhudumiwa mama mzazi huwa kimya"

Sasa fikiria na uwaze kwa makini kabla hujamleta mama hapo akaja na sera zake za mama wa kambo.
 
Achana nae, ale starehe zake huko na mumewe halafu nyie mbaki mnagombana na mkeo,mwache kabisa baada ya sherehe ndio umwambie, kwamba jana tulimfanyia mtoto sherehe
 
Achana nae, ale starehe zake huko na mumewe halafu nyie mbaki mnagombana na mkeo,mwache kabisa baada ya sherehe ndio umwambie, kwamba jana tulimfanyia mtoto sherehe

Hebu vaa viatu vya huyu mama na useme kama wewe ungeweza kuishi bila kumuona/kufahamiana na damu yako.
 
Kama hiyo shughuli bado iko mbali its better mkamwambia tu bado mapema sio siku yenyewe inafika au bado siku mbili ndo mnajifanya kumwambia!
 
utamuumiza mtoto wako,bora usimwambie kitu huyo mama.kipindi chote unachowasiliana nae,kwa nini hakumuona mtoto wake?au anaishi nje ya nchi?maana kama anaishi bongo,sioni sababu kwa huyo mama kutokumuona mtoto wake.subiri huyo mtoto akue,afike kwenye 18 ndio umuambie ukweli.na umpe sababu ambazo zitafaa kwa huyo mtoto ili asije akamchukia mama yake aliemzaa
 
Hapo ndipo na mie nimejiuliza, hayo mawasiliano ni ya juu ya nini, kuna wanawake wana roho ngumu sana, mtoto umeingia leba mwenyewe usimuone miaka nane? halafu unataka kwenda kwenye sherehe, huyu mama ni mjinga wala hastahili kwenda kwenye hiyo sherehe ata mconfuse tu mtoto keshazoea maisha yake

dah! For sure hii comment imeniumiza to the extent nimeshindwa hata niseme nini coz naona ka unamsemea my mum ambae najua kabisa sio ujinga ulomfanya asinione mwanae kwa miaka mingi!
 
Sababu hasa ya kutomuona mwanae kwa miaka 8 ni ipi? Ulimkataza asimwone? Mama hakuwa interested kukutana na mwanae baada ya kupata familia mpya? Umbali? Ni nini hasa! Mtoto wako wa kumzaa kabisa umwache tangu akiwa na miaka 2 uje kujali sasa baada ya miaka yote hiyo kweli?! Mmh.. Think again usije ipa mtihani familia yako!
 
Usimwalike kabisa, alikuwa wapi siku zote atokee kwenye sherehe tu, ulimwalika kumpeleka mtoto siku ya kwanza shuleni? ulimwalika nakumuita wakati mtoto analia usiku mnambembeleza, wakati nyie mmebanwa na shughuli mtoto hana wa kubaki nae mlimuita, kwa kweli usimkwaze binti wa watu huyo ndio mama yake

kwa hiyo unataka kusema kuwa kulikuwa na option moja tu ya mpaka mama aende? Huyo baba angempeleka huyo binti kumsalimia mama yake ingekuwa kosa? Assume kuwa we ndo huyo binti!
 
Ni kweli kabisa Kipipi. Hapa tumesikia one side of the story na tuna conclude. Mtoa mada amekuwa makini kuomba tusimseme kuhusu makosa ya nyuma ambayo hajatuambia ni yepi. Kweli tutachuma dhambi kumsema huyu mama.

Kama unampenda mwanao nadhani ilikuwa si busara ku mseparate na mama yake no matter what? Hata mama yake angesema simtaki huyu mtoto; kitu ambacho najua hakuna mama wa hivyo wewe ungekuwa unampeleka amuone tu si kumlea ili amjue.

Kama mtoto bado ni mdogo nakushauri ufanye haraka amjue mama yake akikua hatakaa akusamee wewe na huyo mama wa kambo hata mumpe maelezo gani. Kwa umri wa sasa hatakuwa na akili ya kuwahoji lakini akikua mtajuta.

Huyo mkeo atachukia kisa umemualika mama wa mtoto kuja kwenye sherehe ya mtoto wake? What made you think so?? Any way wewe wamjua mkeo vizuri; ila mke mwenye busara hawezi chukia tena ukizingatia huyo mama wa mtoto keshaolewa kwa hiyo there is no way mnaweza kurudiana. Kama mkeo alikuwa na roho nzuri ya kumlea mtoto asiye wake leo hii kipi kitamfanye aone vibaya mwenye mtoto kumuoana mwanae? Ataona wivu kuwa mtoto anamuona si real mother? Why na ana watoto wake? Yeye si ana watoto wake? Angefurahi mtu afanye hicho mlichofanya kwa watoto wake?

Kuna family friend wetu aliolewa na jamaa afu waka divorce. jamaa watoto kapeleka kusoma UK ili mama asiwaone. Na huyu dada akijiiba watoto wakiwa likizo kwenda kuwaona mama yao wa kambo anamtimua na kuwaambia watoto this is not your mother am your mother; imagine.
Na watoto wanamwangalia kama hawamjuhi maana huyo mdada hana uwezo kipesa ila alikuwa ni mzuri saaana ndiyo maana huyo jamaa akamzimikia na kumuoa ndoa ambayo haikudumu. Sasa watoto wakimwangalia mama alivyo arosto wanaona kuwa ni kweli this cannot be our mother. Kwa hiyo kama hatujapata full story tusi judge.

kwa hiyo unataka kusema kuwa kulikuwa na option moja tu ya mpaka mama aende? Huyo baba angempeleka huyo binti kumsalimia mama yake ingekuwa kosa? Assume kuwa we ndo huyo binti!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom