Mtoto wa shangazi ana kiburi kwenye kufata sheria zangu nyumbani kwangu, nitatue vipi?

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,032
Nyumbani kwangu ikifika wakati wa chakula cha usiku (dinner) ni lazima tule pamoja kwenye chumba kimoja,

Sasa kuna mtoto wa shangazi ni kama miaka 20 hivi hapendi kufata sheria ya mda wa dinner. Sheria ya muda wa mlo wa usiku ni kwamba simu hazitakiwi kutumika, simu inabidi ziachww vyumbani.

Lengo ni kupata chakula cha usiku kama familia, ni muda ambao watu wote ndani ya nyumba tunajumuika, kila mtu anaelezea siku yake imeendaje, maendeleo ama changamoto kwenye shughuli zake, ushauri, kukumbushana umoja ni nguvu, n.k.

Sasa huyu dogo ni kama haheshimu huu utaratibu, yeye akija bado yupo busy na simu kwa kuibia ibia. Shangazi yangu ni mtu ambae tumezoeana sana tangu nikiwa mtoto, naogopa nikimminya sana dogo ataenda kulalamika halafu ikala kwangu.

Nimemwambia kama mara 3 anaacha ila anarudia.

Suluhisho ni nini??
 
Heading: Mtoto wa shangazi
Main body: Mtoto wa mamdogo
Conclusion: Chai jaba.
Mkuu haya mambo ya binamu, shangazi, mamdogo, shemeji mpaka leo huwezi amini yananipiga chenga.

Nje ya maada lakini nielimishe utofauti mkubwa wa shangazi na mamdogo na ndugu zake wa kike wa mama.
 
Kama mengn yote anaendana nayo hakun tatzo sana

Zaidi ikifik saa 1:45 chukua simu yake kaweke chumbn kwako then mrudishie kesho asubuh hadi atapobadlk yeye binafs
 
Tumia sheria hii itakusaidia:

Chini ya dari langu ni sheria zangu, au kwa kimakonde under my roof my rule.

Kama ulishamkanya subiri siku kukiwa kuna msosi aupendao sana, siku hiyo akigusa simu mwambie aile hiyo simu yake na umfukuze mezani aende kuchat vizuri, usimuonee huruma wala haya. Halafu tupe mrejesho kama amebadilika au la
 
Nyumbani kwangu ikifika wakati wa chakula cha usiku (dinner) ni lazima tule pamoja kwenye chumba kimoja,

sasa kuna mtoto wa shangazi ni kama miaka 20 hivi hapendi kufata sheria ya mda wa dinner.

sheria ya muda wa dinner ni kwamba simu zisifike eneo la chumba hicho.

lengo ni kupata chakula cha usiku kama familia, ni muda ambao watu wote ndani ya nyumba tunajumuika

sasa huyu dogo ni kama haheshimu huu utaratibu, yeye akija bado yupo busy na simu kwa kuibia ibia.

nimemwambia kama mara 3 anaacha ila anarudia.

suluhisho ni nini??
Usiseme sheria sema kanuni... Sema mzee baba insonyesha wewe ni mzee wa itikadi sana mzee wakunyosha palipo pinda kwa masharti
 
Tumia sheria hii itakusaidia:

Chini ya dari langu ni sheria zangu, au kwa kimakonde under my roof my rule.

Kama ulishamkanya subiri siku kukiwa kuna msosi aupendao sana, siku hiyo akigusa simu mwambie aile hiyo simu yake na umfukuze mezani aende kuchat vizuri, usimuonee huruma wala haya. Halafu tupe mrejesho kama amebadilika au la
Kumbe wakoloni mpo wengi.... Sasa si mumuachie kijana achezee simu wewe pia umeona sawa akaze
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom