Mtoto wa nje ya ndoa

Maindainda

Member
Jun 1, 2008
40
6
Ndugu na rafiki zangu wa Jamii Forums,

Naomba msaada katika jambo hili.

Nina ndoa ya kama miaka kumi. Nina mume wangu ambae najua ananipenda, nami pia ninampenda. Miaka kadhaa iliyopita nilikutana na jambo ambalo limenitia simanzi sana na sijui hata nifanyeje, kuna wakati siamini kama ni jambo lililonitokea mimi maishani.

Kwa kifupi ni kwamba nina mtoto ambae najua si wa mume wangu! Amelelewa na huyu baba bila kujua kwa upendo mkubwa, kulipa ada za shule na mahitaji yote. Kusema kweli haijakuwa jambo rahisi maana kila anapomuita baba mimi moyo wangu hujaa simanzi. It happenned that I was at a wrong place with a wrong guy and it happenned. Si tabia yangu na wala sikujidhania kwamba siku moja naweza kuisaliti ndoa yangu.

Huyo baba mwenye mtoto ana mke, simpendi kimapenzi na wala hatuhusiani tena, ikiwa ni pamoja na kuwa hajawahi kumtunza mtoto huyu ingawa anaweza. Sikutaka afanye hivyo. Tatizo ni kuna wakati fulani aliwahi kusema kuwa atakuja kumchukua mtoto wake siku moja, kivipi sijui. Naona ana fujo maana sioni uwezekano wa jambo hili labda avunje ndoa yangu kwanza.

Sio kutokana na sababu hii ila kwa muda mrefu tangu nikiwa na mimba ile nimetaka kumwambia mume wangu ukweli lakini nimeshindwa. Maisha ya masikitiko na kuwaza jamani naona nashindwa na nataka nimwambie ukweli na atoe hukumu yake.

Naomba mnishauri hasa wanaume- ingekuwa wewe ungefanyaje? Nimwambie au niache?

Hili ni tukio la kweli, naomba ushauri usiwe katika yafuatayo:
1. Kusema kwamba mimi msaliti na mke mbaya-hilo nalijua na wengi wenu mnayajua haya na haitanisaidia sana.
2. Kusema nimefanya ngono zembe nikapime ukimwi - nimepima na sina

Naomba msaada.
 
Mama,

Ungeyasema haya mapemaaaaa, kadiri unavyochelewa ndiyo tatizo linavyokuwa kubwa.Muangukie mume wako umuambie, muombe msamaha.Na huyo baba yake mtoto wa kibaiolojia kama hakuandikwa kwenye title deed (birth certificate) anasema mtoto wake kwa kigezo na ushahidi gani? Kwa kukaa kimya sana sana amejifanya "sperm donor" tu.

Mwambie atafute rekodi ya Shaquille O'Neal "Biological didn't bother" ingawa mazingira kidogo ni tofauti lakini Shaquille anaelezea anavyomthamini baba wa kumlea kuliko baba yake wa kibaiolojia, kwa sababu baba wa kibaiolojia ni kama mgeni, ndiyo nini kusubiri siku zote hziz na kutaka mtoto sasa?

Haki ya mungu huu wimbo unatoa machozi, hasa ukilifikiria lile Shaquille Man of Steel linavyokuwa sentimental hapo hamna cha Shaq Diesel wala nini!

GT,

Are you keeping score of the many reasons not to get married?


Two so far.

Yo, Yo
I want to dedicated this song to Philip Arthur Harrison
Word up
cause he was the one who took me from a boy to a man
So as far as I'm concerned, he's my father cause my biological didn't bother

[Verse 1]
Biological father, left me in the cold, when a few months old
Aa father's child was greater than gold but I guess not
You brought me into the world but your not my dad
Mess around with those drugs makes my moms mad
So we left you with no remorsal pity
Took the first bus from York to Jersey City
Women and child alone now thats pressure
Moms got to go to work, drop me off by Obesa
Momma, Aunt DeDe, whoever
Aunt Falma, Uncle Roy we stuck together
A year went by and I could walk y'all
Moms got that good ol job at city hall
She probably didn't trust men anymore
Until Philip Harrison walk though the door
Went out a few times but what about Shaquille
Moms offered him a million dollar package deal
She said you want me you gotta take my son
or else its like a hot dog but without the bun
Guess what he accepted, responsibility he never left it
He kept it, he kept it
He took me from a boy to a man so Phil is my father
cause my biological didn't bother

[chorus] He took me from a boy to a man so Phil is my father
cause my biological didn't bother. (4x)

[Verse 2]
January 5th Phil made a promise (what's that)
He joined the army we moved to fort mamth
He disciplined me right from the get go
Age 2 bottle and my Mom shaquille let go
Actin spoiled, rotten, trippin
Got a butt whippin because I didn't listen
Back then you see privates made no bucks
Had to get another job driven trucks
Workin hard as hell didn't satisfy him
Had to another job working at the gym
He wasn't "Gone with the Wind" like Clark Gable
Work all them jobs to put food on the table
Phil's my father, daddy and thats the scoop
Can I go to the gym with you and shoot some hoops
Come on he put me under his wing
Was the ball boy for his little Arthur team
Sometimes he even made me mad
But it didn't matter cause I still wanted to be like dad
but a little bit better
Encouraged me to stay in school and to get then good letters
I wasn't a brainiac but I tried hard
Got to watch the Knicks play if I had a good report card
All types, all sorts
Disobeyed my dad and I couldn't play sports
I learned to dribble from right to left
I couldn't do a damn thang with all them F's
Age 15 father and son confrontation that's nothin
but father and son trials and tribulation
Back then I could under stand but I'm glad you did it
cause now I'm a man
He took me from a boy to a man so Phil is my father
cause my biological didn't bother

(chorus)

[Verse 3]
Look at me now successful for sure
Phil raised me well, to be an entrepeneur
and if your making big dope be materialistic
cause you'll end up another statistic
everything's going well following my dreams
I dunked on Patrick Ewing
I won the ring like hakeem
Uh oh what do you know
Biological ones on the Ricky Lake show
What does he want, does he want money
What people do for money!!!
It's kinda funny to me
He aint gettin no check from me (check it)
He can go on all the talk shows he want
Phil is my dad so dont even front
He took me from a boy to a man so Phil is my father
cause my biological didn't bother

(Chorus)
 
Pole bibie,

Ninafurahi unajijua mkosaji ila ushauri mmoja ninao ni hivi:

"Only the TRUTH can set you FREE"
mara nyingi wanaume na wanawake husaliti ndoa zao na kujifanya jeuri huku wakitaka ndoa zao zidumu au hata kulazimisha kuwa ndoa zao zidumu kwa vitisho na vipigo. Na mara nyingi njia hizi hazisaidii hata siku moja. Na wengi husahau kuwa katika kuwa mkweli na muwazi, msamaha wa kweli hutokea na pendo kuchipukia upya.

"Every person is humbled by the Truth"

Siwezi semea mumeo maana simfahamu kitabia wala mwenendo na wala siwezi kukusemea wewe maana kitabia sikujui. Ila jifunze kuwa mkweli. Ukweli hulipa siku zote hata kama atachukia sana ataheshimu kuwa ulimwambia ukweli na wala hukumdanganya. Umweleze kuanzia mwanzo ilivyokuwa na wala usifiche jambo lolote.

ukianza kuwa slective katika yale utakayomweleza basi ujue hata msamaha wa kweli hautapatikana.

Pole ila na hili liwe fundisho kwa wanawake wengine na wanaume wengine.
 
Kama ni mimi ungeweza kuniambia .... Isingekuwa ni big deal.

I am different charater on this palnet.

Ungekuwa na maswali machache tu ya kunijibu ili kutegeneza hii issue.

Ni uwuzi, tena uwazi kabisa kabisa..ungekuokoa...But dont do this to ua husband...maana mimi naye inawezekana tunatofautiana sana.

Lakini kwanza ..tell me all this very HONESTLY...hata kama ukisikia kufa...Just tell it as it was....Jibu kama mimi ni mume wako!

Was you forced into the act?

What really drove you to that ..Chap?

Ulikuwa fully aware when you went with him?

Unafikiri mimi ningetakiwa nifanye nini ... ili usiende naye ..hapa nina maana there was ..weakness in my part ndio maana..ukapata hiyo nafasi.

Na

Kabala sijaendelea..?

Ilikuwaje Baba wa mtoto akajua kuwa una mtoto naye?

Did you tell him?

Why?

Ulivyomuabia ..didi you fill Highhh..yaani ulikuwa unajisikai vizuri..yaani kama umemkomesha mumeo .....kitu kama hicho..just be very frankly...

Let me get all this answers before you get my advice...!

I am sure all will be very fine..if this is true..story..!
 
Mimi ningemwambia ukweli, even if it means inaweza kufanya tukaachana.

Ni mume wako na kama unampenda, sidhani kama ni kitu kizuri kuishi/kuendelea na hiyo siri, mimi ingeni-tear apart slowly. Baada ya mazungumzo hayo mambo yatakuwa magumu, ila ni mwanzo tu, maana hata ingekuwa mimi, ni ngumu sana ku-deal and accept fact that mtoto ni wa mtu mwingine, kuna feeling ya betrayal ambayo ni ngumu kwa most of us to deal with. Lakini, with time, yataisha! Good luck mama, maana you need it.

Kama Bi mkubwa alisema hapo juu, truth will set you free, even if it means you are going to end up alone. It's a price you have to pay, si lazima tuwe responsible for our actions? but in the end, it will be good for everyone involved.
 
Ndugu na rafiki zangu wa Jamii Forums,

Naomba msaada katika jambo hili.

Dada Maindainda, pole sana ila huu ni mwiba wa kujidunga! maoni yangu ni nyamaza hivyo hivyo,, kama miaka na miaka imepita ya nini kusema sasa. u need to think abt the repurcussions becoz this is the highest form of betrayal, sijui kama mumeo atakusamehe na hata akikusamehe huyo mtoto atakuwa a constant reminder of your infidelity

Na huyo biological father anakutishia tu, ana uhakika gani, mmefanya DNA testing? yeye yuko tayari kuweka ndoa yake on the line?? kwa sababu akiharibu yako na ya kwakeje?

the other thing is kwa sababu you are really sorry and remorseful about what you did, letting it out will give you some piece of mind. but u need to be careful how u do it.

My advice tread carefully.. na kila la kheri!

dont worry unaona signature hapa that It happens, to good pple most of the time..........
 
Azimio,

Kukujibu tu maswali yako. Kwanza silichukulii kama ni jambo rahisi kama wewe unavyotaka kufanya lionekane. Jasho lingekutoka. Pili, nataka kukuhakikishia kuwa hii ni true story, my true story.

Was you forced into the act? - NO

What really drove you to that ..Chap? - NOTHING, IT IS JUST THOSE CRAZY FEELINGS WHEN A MAN AND A WOMAN ARE TOGETHER KATIKA MAZINGIRA FULANI.

Ulikuwa fully aware when you went with him? - SIJAKUELEWA, ILA SIKUBAKWA

Unafikiri mimi ningetakiwa nifanye nini ... ili usiende naye ..hapa nina maana there was ..weakness in my part ndio maana..ukapata hiyo nafasi. - KAMA WEWE NI MUME WANGU, YOU ARE GOOD. HE IS NOT EVEN A HALF OF WHAT YOU ARE. HII NI KWELI KABISA.

Na

Kabala sijaendelea..?

Ilikuwaje Baba wa mtoto akajua kuwa una mtoto naye? - ALIULIZA NILIPOKUWA NA MIMBA. HE IS CRAZY AND VERY STUPID, ALIJUA KUWA NAWEZA KUBEBA MIMBA ILA SI NYIE NDIO MNASHIKA MPINI BWANA...... HALAFU MAJUA MAMBO HAYA UNAKUMBUKA KUWA UTAPATA MIMBA BAADAE UMESHAFIKA MBALI LABDA HATA UKISEMA MWENZIO HAKUSIKII!

Did you tell him?

Why?

Ulivyomuabia ..didi you fill Highhh..yaani ulikuwa unajisikai vizuri..yaani kama umemkomesha mumeo .....kitu kama hicho..just be very frankly... - SIJAWAHI KUTAKA KUMKOMOA MUME WANGU KATIKA HILI, NEVER

Let me get all this answers before you get my advice...!

I am sure all will be very fine..if this is true..story..![/QUOTE]
 
Kwa wale wajuao sheria - Kisheria, huyu mtoto ni wa nani?

Kama ni wa Biological father, naweza kufanyaje awe wa kwangu?

Kama alivyoshauri Pundit, hata kama hayupo katika birth certificate, anaweza kushinda kwa kuangalia Vinasaba-DNA, kama ni mtu anaependa fujo au kuna watu hawajali ndoa zao au zimewashinda na wanaweza kutumia chochote ili mke/mume apate EXIT way. Najaribu kuwa mwangalifu hapa.
 
Dada Maindainda,
Pole kwa yaliyokusibu.
Mueleze mumeo na muombe msamaha na sikiliza au pokea matokeo bila kinyongo.
Mahali ulipo sidhani kuna lingine la kusema, kwani kwa kweli umeathiri watu wengi au utaathiri watu wengi kweli kwa ubinafsi wako. Mfikirie mumeo. Tena unavyoelezea jinsi anavyokupenda kwa kweli namuonea huruma. Wafikirie wanao katika ndoa. Mfikirie huyo mtoto na mazingira aliyokulia halafu leo itokee vinginevyo. Fikiria ni jinsi gani utaathiri ile ndoa nyingine. Fikiria familia yako ya mumeo. Fikiria standing yako kwenye jamii.

Kwa kweli nakuonea huruma, I wish ningekuwa namfahamu mmoja wa hao wanaume niongee naye, na hasa huyo alleged baba mtoto. Kwani anapaswa pia kufikiria haya yote niliyokuambia wewe, but above it all, psychologiacally huyo mtoto atakuwa affected kiasi gani.

Jamani tuwe waangalifu. This is just a tip of an iceberg.

Good Luck, dada na pole.
 
Maindainda, pole sana!

Ni ngumu, lkn jitutumue ufanye vile unavyoona ni sahihi katika mazingira yako, haswa baada ya kufanya upembuzi yakinifu, ambao utakusaidia kuishi kutokana na matokeo yake.
Kama wengi walivyokubali kuwa 'UKWELI HUKUWEKA HURU',lkn je hao wahusika wengine nao watakuwa huru??!!??!?

Binafsi niligundua kuwa mimi ni mtoto wa nje ya ndoa nikiwa ninafanya kazi, nilihisi kama nimeonewa! Kwa ufupi nilikosa imani na mama!! Nikawa nimechanganyikiwa haswa ukizingatia sikuweza kumuuliza mama anipe ukweli kutokana na mazingira aliyoyaweka baina yangu na ya baba aliyetoa mbegu!!!

Baba mlezi ananipenda kupindukia, kuliko hata watoto wao halisi, baba alioetoa mbegu naye ananipenda na kwakweli alijaribu kuwa karibu ingawa mimi sikuwa naelewa kutokana na mazingira aliyoyaweka mama!
Nikifika hapo sasa nazidi kuchanganyikiwa!

Sasa Maindainda, hebu jitahidi kufanya upembuzi wa yale unayoyataka kufanya, yasilete majeraha na vidonda ktk mioyo na hisia za hao wahusika na kikubwa zaidi kwako pia!

Every little action has a rection!!
 
Palloma,

Nimekuelewa, pole sana. Watoto wengi wa nje ya ndoa hukosa raha wanapojua. Hii ndio faida ya JF, wengi wanajifunza, najua wapo wengine kama mimi katika forum hii, wake kwa waume.

Ni katika mazingira gani ulijua wewe una baba mwingine, yaani alikuambia au?

Kuna uhusiano gani kati ya mama yako na baba yako biological kwa sasa?

Kama baba mlezi anakupenda sana kwa nini unajisikia bado wataka kuhusiana na huyo mwingine?

Asante kwa kutokumtukana mama yako kwa kitendo alichokifanya.
 
  • Thanks
Reactions: SG8
............................Naomba mnishauri hasa wanaume- ingekuwa wewe ungefanyaje? Nimwambie au niache?
Hili ni tukio la kweli, naomba ushauri usiwe katika yafuatayo:
1. Kusema kwamba mimi msaliti na mke mbaya-hilo nalijua na wengi wenu mnayajua haya na haitanisaidia sana.
2. Kusema nimefanya ngono zembe nikapime ukimwi - nimepima na sina

Naomba msaada.

Ushauri wa PUNDIT nauunga mkono na ikishindikana njoo tena uombe ushauri hapa,
Next time usirudie upuuzi huo, unajue sie wengin tumeoa na unapoleta hizi story unasababisha tuwaangalie mawifi zako kwa jicho kali kidogo. Inafika mahala mtu unataka uhakikishe kuwa hata mate yanafanana na mtoto ili kujiridhisha.....
 
Dah pole sana dada....mm naona hapo kwa jinsi wanaume walivyo ni bora ubaki na siri moyoni usimwambie itakuathiri wewe pamoja na mwanao....sio wewe tu walio wabambikia watoto wanaume zao.

Kwa hiyo wewe vumilia tu weka siri moyoni mpaka mtoto atakapo kuwa na kuanza kujitegemea ndipo utamwonyesha baba yake na sio sasa hivi.Ukisema ukweli utakuja kuumia tena sana...utatengwa na ndugu pamoja na jamii inayo kuzunguka.

Naongea hivi kuna binamu yangu imemtokea kama wewe akamwambia mwanaume ikawa balaa akaambulia kuachika na sasa hivi anatanga tanga tu na ndugu wamemtenga kabisa vile vile jamii inayo mzunguka inamwona mtu wa ajabu wanaona kama ni kosa kubwa sana.

Lakini angeweka siri moyoni yote haya yasingetokea na angeishi na jamaa kwa raha mstarehe....si mnajua ukweli unauma kwa hiyo pindi usemapo ukweli uwe tayari kubeba lawama,kudharaulika na mengine mengi.Ni bora uacha tu na uweke siri moyoni watu wasijue kabisa.

Hakuna kitu kinacho uma kama kujua.....sasa usitake hii ikutokeee wewe weka siri jamaa aendelee kuhudumia na mtoto aendelee kumwita baba ingawa ni wa kambo.Ukimwambia tu jamaa itamuuma sana na itaweza kukuathiri wewe na mwanao hapo nyumbani wewe chuna tu imradi maisha yanasonga mbele.
Pole sana endelea kuweka siri moyoni.
 
Pole Maindainda,

Well, your story is very serious!
You just be silent until the kid is mature enough to handle the matter. It will be unpleasing if the kid discovers that the man you live with is not his dad. The kid will recall all the hardship she/he suffered on the hand of the current said father and conclude that it was deliberately and that will provoke more crisis to the kid.

Kwa hivyo, once mtoto atakapokuwa mkubwa na ukiona ni muda muafaka, rudi kwenu kisha waeleze wazazi/wakubwa zako kuhusu jambo hilo na uwaombe wakamweleze mumeo na kukuombea msamaha. Mume akikubali usuluhishi atarudi kukuchukua nyumbani, akikataa then it will be over.

Kwa upande mwingine, mumeo ndio atakuwa na wajibu wa kumweleza mtoto kuhusu hilo kwani kimsingi yeye ndio psychological father. Lakini naimani akiwa ni mtu mwenye busara
hataweza kumwambia mtoto chochote na wewe unabidi ukae kimya ili usimvuruge mtoto.

Kikubwa ni kwamba duniani, sote tunakosea kwa namna moja au nyingine. Mungu anatusamehe lakini adhabu ya itakuwepo.

Kama we ni msomaji wa Biblia kidogo kama sikosei kuna nabii mmoja mwanaume alitakiwa na Mungu aone Kahaba na huyo kahaba amzalie watoto watatu wa zinaa ili aone uchungu ni jinsi gani unavyoweza kuteseka ikiwa mkeo akiamua kufanya ufisadi. Lakini Mungu alimtaka nabii yule avumilie kama vile Mungu alivyowavumilia Wayahudi na mambo yao ya kufanya yasiyofaa.

Kwa hivyo, kwa mumeo kama anauwezo wa kuvumilia mambo hiyo ni baraka kwa Mungu.

Ok i think you got me right
 
Kwa wale wajuao sheria - Kisheria, huyu mtoto ni wa nani?

Kama ni wa Biological father, naweza kufanyaje awe wa kwangu?

Kama alivyoshauri Pundit, hata kama hayupo katika birth certificate, anaweza kushinda kwa kuangalia Vinasaba-DNA, kama ni mtu anaependa fujo au kuna watu hawajali ndoa zao au zimewashinda na wanaweza kutumia chochote ili mke/mume apate EXIT way. Najaribu kuwa mwangalifu hapa.
Da Mainda kumbuka kitanda hakizai haramu! Mtoto kisheria baba yake ni mumeo wa ndoa, piga ua hata mkipima DNA huyo mwizi hawezi kupewa mtoto!
 
Azimio,

Kukujibu tu maswali yako. Kwanza silichukulii kama ni jambo rahisi kama wewe unavyotaka kufanya lionekane. Jasho lingekutoka. Pili, nataka kukuhakikishia kuwa hii ni true story, my true story.


Was you forced into the act? - NO

What really drove you to that ..Chap? - NOTHING, IT IS JUST THOSE CRAZY FEELINGS WHEN A MAN AND A WOMAN ARE TOGETHER KATIKA MAZINGIRA FULANI.

Ulikuwa fully aware when you went with him? - SIJAKUELEWA, ILA SIKUBAKWA

Unafikiri mimi ningetakiwa nifanye nini ... ili usiende naye ..hapa nina maana there was ..weakness in my part ndio maana..ukapata hiyo nafasi. - KAMA WEWE NI MUME WANGU, YOU ARE GOOD. HE IS NOT EVEN A HALF OF WHAT YOU ARE. HII NI KWELI KABISA.

Na

Kabala sijaendelea..?

Ilikuwaje Baba wa mtoto akajua kuwa una mtoto naye? - ALIULIZA NILIPOKUWA NA MIMBA. HE IS CRAZY AND VERY STUPID, ALIJUA KUWA NAWEZA KUBEBA MIMBA ILA SI NYIE NDIO MNASHIKA MPINI BWANA...... HALAFU MAJUA MAMBO HAYA UNAKUMBUKA KUWA UTAPATA MIMBA BAADAE UMESHAFIKA MBALI LABDA HATA UKISEMA MWENZIO HAKUSIKII!

Did you tell him?

Why?

Ulivyomuabia ..didi you fill Highhh..yaani ulikuwa unajisikai vizuri..yaani kama umemkomesha mumeo .....kitu kama hicho..just be very frankly... - SIJAWAHI KUTAKA KUMKOMOA MUME WANGU KATIKA HILI, NEVER

Let me get all this answers before you get my advice...!

I am sure all will be very fine..if this is true..story..!
[/QUOTE]

GET THIS VERY CLEAR AND TAKE IT VERY SERIOUSLY:


1. Mimi ningekuwa huyo mtoto unayemuogelea hapa... Nisingependa kumjua BABA zadi ya yule niliyemuona pale nyumbani. Yule aliyenipeleka shule. Yule aliyenipa feelings and emotional of care and all the attention. Singejali what my DNA constitutes etc. Leo hii Mama yangu akija na kuniambia kuwa The father I have been staying with, mpaka ni kawa mtu mzima sio Baba yangu kwa sababu tu ya DNA..nitamuona 'Mama is stupid'. Who cares about the DNA? Baba sio chemicals..which make the DNA ni UTU alionipa na kuutumia kunijali, kunipa mapenzi na kunilea..

2. Kutokana na Maelezo yako. Honestly speaking MOYO wako haukumsaliti Mumeo. Ila It was only feelings, emotions and your beautiful body... Sioni mahali ulipokuwa na kisasi cha NGUVU kwa Mumeo (ambayo hiyo ndio mbaya)... Kwa wanawake wengine They feel very very good wanapo_MSANIFU mume akiitwa Baba na Mtoto asiye wake..They Feel..”MSHENZI NIMEMUWEZA” etc..and you know that is evil...Wewe sikuoni hapo....DEEP IN YOU BADO MNA NDOA NA MUMEO...watch that...!!. Wanaume wa Kweli wanachohitaji kwa Mwanamke .."SIO MWILI KWANZA" ila “MOYO....” Kila mwanamke anaweza kunipa mwili wake but vigumu sana kuupata MOYO wake. Kama Mke wangu kabakwa...hakutoa moyo wake...kwa hao washenzi..Nasimama naye . Namtetea kabisa..... Lakini kama kwa akili timamu...kaamua kujitoa that is different story. Kama alipanga kabisa hiyo Game na kuwa fascinated nayo..hapo hatutelewana. Si unaona case yako? you was simply arroused on the ovulation day......So jua kuwa Bado una clear BOND na mumeo. Huhitaji kumvuruga. dont tell him. Haina maana yeyote...And don’t do it again….Yaani Kosa hilo...dont repeat. How?

3. You know why it happened? Maelezo yako yanatosha kabisa kujieleza. I tell you ni kitu kilikuwa kimjificha ndaniyako."Uncosciouse"

Go into your Past. Utaona kuwa kilichotokea na huyo bwana uliyezaa naye nje ya ndoa ni MARUDIO. Ni replay!!!

Yaani...tukio karibu kabisa na hilo limewahi kutokea huko nyuma. Kivipi?

Umeshawahi kurelate na mtu kama huyo..au karibu kumfanania huyo. Au hiyo enviroment uliyojikuta unakuwa helpless na ku_yield...Imejirudia..yaani inafanina au karibu kabisa ...na hiyo uliyojikuta.

AU:

Umekuwa na chuki kubwa sana na huyo bwana au mtu kama huyo..yaani una mchukia mtu mpaka ..unajikuta sexualy attracted..It happens many times..na dunia inashangaa hata wewe..tena huyo!!

Posibility zote hizo...KIUKWELI SIO KOSA LAKO HASA...ILA..NI VERY PSYCHOLOGICAL....Na zinaweza kukubeba....hakuna mtu atakuelewa...lakini be carefull na condition hizo nilizotitaja...maana ukijikuta hapo you can repeat the MISTAKE…the ACT..bila ridhaa yako.

4. Don’t bother to tell this to you husband. Chukulia kuwa it was just a bad dream. Ungemueleza kama ni Mimi...Narudia sio kuwa ni na oversimplyfiy..but because I understand the mechenics… I deely understand. Pole na endelea na masiha.
 
you know your husband better than all of us .. mwengine ukimwambia ukweli atakuchukia maisha it can kill him as well ... eeh its very painful

one mistake you did ni kumwambia that thieeeef kwamba you have his baby ... why did you do that for christs sake ... unakimbelembele kweli

Mi I suggest ... study the situation carefully reverse the order umwambie yule bazazi the child is not his and then kwa mume wako .... just swallow ... because you will distabilise and dismantle him kabisa.

Kila mtu ana madhambi ..... so go wisely on this
 
you know your husband better than all of us .. mwengine ukimwambia ukweli atakuchukia maisha it can kill him as well ... eeh its very painful

one mistake you did ni kumwambia that thieeeef kwamba you have his baby ... why did you do that for christs sake ... unakimbelembele kweli

Mi I suggest ... study the situation carefully reverse the order umwambie yule bazazi the child is not his and then kwa mume wako .... just swallow ... because you will distabilise and dismantle him kabisa.

Kila mtu ana madhambi ..... so go wisely on this

Nimeipenda sana hiyo comment hapo kati....

1. Ila kisheria, kama mama atamweleza mumewe na mumewe akaridhia basi huyo mtoto atakuwa ktk custody na kutambulika kama mtoto wa kwenye ndoa kisheria (sheria za nchi yetu pia zinapromoti hiyo) ikiwa ni pamoja na mirathi, na hii inaweza hata kufanyika mbele ya court of law na kesi inaisha bila hata ya rungu ya hakimu kugonga meza. Na baba au mama mlezi (ndoa) anaweza pia kumdai fidia ya kiwango chochote jamaa ambaye ame tresspass kwa mkewe au mumewe.

2. Ila endapo mume halali au hata mke halali (wa ndoa) akamreject mtoto ambaye si mwuunganiko wao kibaologia, basi huyo mtoto ataenda kuwa chini ya custody ya tresspasser na hakutakuwa na fidia wala adhabu hapo. Na most of all anayelose ni mwenye ndoa maana sheria inaweza kumpa ruhusa ya kumlea au akaondolewa chini ya uangalizi wa wenye ndoa na akapelekwa upande wa pili (trespasser) ambapo kisheria baba na mama kibaologia wanaruhusiwa kuaccess huyo mtoto phyisical. Mnajua matokeo yake??? anaweza kupatikana wa pili hapo...

Huyo bazazi anayesema kuwa atakuja kumchukua mtoto, ijulikane anachoweza kuwaza haraka haraka ni kutumia mahakama. hivyo ushauri wangu namba moja ukitumia na baba mlezi akamkubali mtoto baaas huyo trespasse kaisha...

Hivyo namshauri Maindainda aende kumwangukia mumewe kwa kila hali amkubali mtoto au la anaweza kukosa kote. yaani akakosa mume na akakosa buzi (mwizi) ikiwa haya mambo yatafika ktk sheria....

Natumaini wakija akina Augustoos hapa wanaweza kunyoosha sentensi vizuri...
 
Last edited:
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom