Mtoto wa nje ya ndoa anaweza kurithi mali ya mama yake aliyefariki akiwa ndoani na baba mwingine ikiwa baba ndio aliwakuta mtoto na mama?

Deejay nasmile

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
5,759
5,289
Wakuu naomba kuuliza hili swali?

Mtoto wa nje ya ndoa anaweza kurithi mali ya mama yake aliyefariki akiwa ndoani na baba mwingine? Ikiwa baba ndio aliwakuta mtoto na mama wanajitegemea

Iko hivi wakuu

Ikiwa mama anaishi na mtoto wake baada ya baba mtoto kufariki, wakawa na maisha yao ya kawaida tu.

Baadae mama anaolewa (funga ndoa) na baba mwingine..maisha yanaendelea,familia inakua na mali wanachuma vizuri.

Ikatokea mama kafariki gafla bila kuacha wosia ..je yule mtoto wa kwanza anaweza kurithi sehem ya mali za mama yake zilizochumwa pamoja na baba wa pili?Sheria hapo inasemaje?

Kwa kifupi hiyo sheria haipo kwa hapa Tz. Kwa mujibu wa sheria ya mtoto ya Tz iliyofanyiwa mapitio mwaka 2019, kifungu cha 10 cha sheria hiyo chenye "marginal note" isemayo "right to parental property" kinasema...
"A person shall not deprive a child of reasonable enjoyment out of the estate of a parent."
Yaani kwa kiswahili ni kusema kuwa
"Mtu hatamzuia mtoto yeyote kufurahia(kunufaika) mali ya mzazi wake"
Hilo neno "mtoto" tafsiri yake kwenye sheria hiyo halijabagua mtoto wa ndani au nje ya ndoa. So hao watoto wana haki ya kurithi mali ya mama yao.
 
Nami napenda kujua...
Kwa kifupi hiyo sheria haipo kwa hapa Tz. Kwa mujibu wa sheria ya mtoto ya Tz iliyofanyiwa mapitio mwaka 2019, kifungu cha 10 cha sheria hiyo chenye "marginal note" isemayo "right to parental property" kinasema...

"A person shall not deprive a child of reasonable enjoyment out of the estate of a parent."

Yaani kwa kiswahili ni kusema kuwa

"Mtu hatamzuia mtoto yeyote kufurahia(kunufaika) mali ya mzazi wake"

Hilo neno "mtoto" tafsiri yake kwenye sheria hiyo halijabagua mtoto wa ndani au nje ya ndoa. So hao watoto wana haki ya kurithi mali ya mama yao.
 
Kwa kifupi hiyo sheria haipo kwa hapa Tz. Kwa mujibu wa sheria ya mtoto ya Tz iliyofanyiwa mapitio mwaka 2019, kifungu cha 10 cha sheria hiyo chenye "marginal note" isemayo "right to parental property" kinasema...

"A person shall not deprive a child of reasonable enjoyment out of the estate of a parent."

Yaani kwa kiswahili ni kusema kuwa

"Mtu hatamzuia mtoto yeyote kufurahia(kunufaika) mali ya mzazi wake"

Hilo neno "mtoto" tafsiri yake kwenye sheria hiyo halijabagua mtoto wa ndani au nje ya ndoa. So hao watoto wana haki ya kurithi mali ya mama yao.
Asante mkuu...kwahiyo watoto wakienda kudai mahakamani mali za mama yao wanashinda bila chenga
 
Kichwa cha habari tu nishadata..🤣
Yaani mwanaume kamkuta singo maza akiwa anaishi na watoto/mtoto wake..then akaanza nae mahusiano hapo hapo kwa singo maza, na baadae wakafunga ndoa na kuanza maisha ya ndoa wakapata mtoto..je mali watakazochuma na huyo singo maza, wale watoto/mtoto wa singo maza wataweza kupata sehem ya urithi ikiwa mama atafariki? Au zitamuhusu tu yule aliyezaliwa baada ya ndoa?
 
Yaani mwanaume kamkuta singo maza akiwa anaishi na watoto/mtoto wake..then akaanza nae mahusiano hapo hapo kwa singo maza, na baadae wakafunga ndoa na kuanza maisha ya ndoa wakapata mtoto..je mali watakazochuma na huyo singo maza, wale watoto/mtoto wa singo maza wataweza kupata sehem ya urithi ikiwa mama atafariki? Au zitamuhusu tu yule aliyezaliwa baada ya ndoa?
Ngoja waje wataalum.
 
Asante mkuu...kwahiyo watoto wakienda kudai mahakamani mali za mama yao wanashinda bila chenga
Naam mkuu...mtoto ana haki ya kurithi mali ya mzazi wake...ktk story yako hao watoto wa huyo mama ambao alikuwa nao kabla hajaanza mahusiano na mume wa sasa...wana haki kisheria ya kurithi mali za mama yao.

Hili suala liliwahi kuamuliwa na Mahakama kuu kanda ya Mwanza ktk kesi ya ELIZABETH MOHAMED VS ADOLF JOHN MAGESA na Jaji Mruma kuwa kwa sasa hapa Tanzania hakuna sheria yoyote inayomkataza mtoto asirithi mali za mzazi wake.

Hivyo ktk hii scenario hao watoto wana haki ya kurithi mali yoyote ambayo ni ya mama yao...haijalishi amazipata mali hizo kabla au baada ya kukutana na huyu baba wa sasa aliyezaa naye tena mtoto/watoto.

So watoto wote ambao huyo single mother alikuwa nao kabla hajaolewa na aliowapata baada ya kuolewa...wote wana haki ya kurithi mali za mama yao.
 
Naam mkuu...mtoto ana haki ya kurithi mali ya mzazi wake...ktk story yako hao watoto wa huyo mama ambao alikuwa nao kabla hajaanza mahusiano na mume wa sasa...wana haki kisheria ya kurithi mali za mama yao.

Hili suala liliwahi kuamuliwa na Mahakama kuu kanda ya Mwanza ktk kesi ya ELIZABETH MOHAMED VS ADOLF JOHN MAGESA na Jaji Mruma kuwa kwa sasa hapa Tanzania hakuna sheria yoyote inayomkataza mtoto asirithi mali za mzazi wake.

Hivyo ktk hii scenario hao watoto wana haki ya kurithi mali yoyote ambayo ni ya mama yao...haijalishi amazipata mali hizo kabla au baada ya kukutana na huyu baba wa sasa aliyezaa naye tena mtoto/watoto.

So watoto wote ambao huyo single mother alikuwa nao kabla hajaolewa na aliowapata baada ya kuolewa...wote wana haki ya kurithi mali za mama yao.
Asante sana mkuu...jua umesaidia wengi sana kwa jibu lako
 
Asante sana mkuu...jua umesaidia wengi sana kwa jibu lako
Kesi ya Elizabeth Mohamed dhidi ya Adolf John Magesa iliyohusu endapo kama mtoto wa nje ya ndoa ana haki ya kurithi mali ya mzazi wake hii hapa.

Jaji Mruma anajadili hilo kuanzia ukurasa wa 20 na kuendelea.
 

Attachments

  • 4_5906933260230854565.pdf
    403.3 KB · Views: 29
Back
Top Bottom