Mtanganyika
JF-Expert Member
- Jul 18, 2007
- 1,601
- 945
Na Richard Bukos
Mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Elimu wa zamani Joseph Mungai aitwae Justina Mungai na wenzake saba ambao ni wafanya kazi wa benki Kuu ya Tanzania (BoT), Jana (Ijumaa) walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam baada ya kutiwa mbaroni wakidaiwa kuwa na vyeti feki....
Vijana hao waliotiwa mbaroni na kufikishwa mahakamani hapo ni mtoto huyo wa kigogo wa zamani na watoto wengine wa vigogo ambao ni Christina G. Ntemi, Siamini E. Kombakono, Janeth Mahenge, Betha C. Massawe, Jacqueline D. Juma, Philimina P. Mutagurwa na Amina M. Mwinchumu.
Akiwasomea mashtaka yao Mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo Abubakar Mbangi alidai watuhumiwa walitenda kosa la kufoji vyeti vya elimu ya sekondari kwa nyakati tofauti ambapo washitakiwa wote walikana mashtaka dhidi yao.
Baada ya kukana makosa hayo watoto saba wa vigogo hao walipelekwa rumande katika Gereza la Segerea hadi kesi hiyo itakapotajwa tena Octoba 6, mwaka huu isipokuwa Philimina Mwinchumu ambaye alitimiza masharti ya dhamana na kutolewa.
Source na Global Publisher
Mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Elimu wa zamani Joseph Mungai aitwae Justina Mungai na wenzake saba ambao ni wafanya kazi wa benki Kuu ya Tanzania (BoT), Jana (Ijumaa) walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam baada ya kutiwa mbaroni wakidaiwa kuwa na vyeti feki....
Vijana hao waliotiwa mbaroni na kufikishwa mahakamani hapo ni mtoto huyo wa kigogo wa zamani na watoto wengine wa vigogo ambao ni Christina G. Ntemi, Siamini E. Kombakono, Janeth Mahenge, Betha C. Massawe, Jacqueline D. Juma, Philimina P. Mutagurwa na Amina M. Mwinchumu.
Akiwasomea mashtaka yao Mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo Abubakar Mbangi alidai watuhumiwa walitenda kosa la kufoji vyeti vya elimu ya sekondari kwa nyakati tofauti ambapo washitakiwa wote walikana mashtaka dhidi yao.
Baada ya kukana makosa hayo watoto saba wa vigogo hao walipelekwa rumande katika Gereza la Segerea hadi kesi hiyo itakapotajwa tena Octoba 6, mwaka huu isipokuwa Philimina Mwinchumu ambaye alitimiza masharti ya dhamana na kutolewa.
Source na Global Publisher