Mtoto wa Mkulima: Si lazima uwe na wanachama wengi ili chama kipendwe

Lekachonka

Member
Dec 17, 2016
35
17
Kuna jambo kubwa sana la kujifunza kupitia kauli hiyo ya mzee Pinda. Alitoa mfano wa China,anasema alijiuliza kuwa China inao watu takribani 1.3 B ,akataka kujua Communist Party (CP) itakuwa na wanachama wangapi? Anasema alistaajabu sana pale alipokuta chama kina wanachama milioni 80 tu. Ambayo hii 6% ya wachina wote walio wanachama wa CP.

Hapa kwetu Tanzania,CCM inao takribani wanachama milioni 6,ambao ni kama 11.5% ya Watanzania wote walio wanaCCM. Akazidi kusema kuwa kinachofanya chama kipendwe si kuwa na wanachama wengi,ni chama kujikita zaidi katika kutatua matatizo ya Wananchi,chama kuwa na viongozi waadilifu. Akasisitiza kwa kusema....Mzee hawa wanaCCM ulionao wanatosha!! Hapa lazima tujiulize kidogo.

1. Kwanini mzee huyu kaamua kuzungumza hivo katika wakati huu ambapo tunaona wimbi kubwa la usajili wa wanachama wapya kutoka upinzani?

2. Kwanini anaona hamna umuhimu wa kuwa na wanachama wengi zaidi iwezekanavyo?

3. Mzee alikuwa anamwambia Rais kuwa upinzani kuwepo ndiyo uhai wa CCM na Taifa kwa ujumla?

Aliyeielewa kauli ile ya Mzee pinda,tusaidiane kuitafakari.
 
Atakuwa amekunywa maziwa ya ngo'mbe wake na kujawa na mkojo. Asiyejaribiwa ni genius sana,chemistry ya kuongoza imejaa pale! Viva Mr."Don't dare me"!
 
Kuna jambo kubwa sana la kujifunza kupitia kauli hiyo ya mzee Pinda. Alitoa mfano wa China,anasema alijiuliza kuwa China inao watu takribani 1.3 B ,akataka kujua Communist Party (CP) itakuwa na wanachama wangapi? Anasema alistaajabu sana pale alipokuta chama kina wanachama milioni 80 tu. Ambayo hii 6% ya wachina wote walio wanachama wa CP. Hapa kwetu Tanzania,CCM inao takribani wanachama milioni 6,ambao ni kama 11.5% ya Watanzania wote walio wanaCCM. Akazidi kusema kuwa kinachofanya chama kipendwe si kuwa na wanachama wengi,ni chama kujikita zaidi katika kutatua matatizo ya Wananchi,chama kuwa na viongozi waadilifu. Akasisitiza kwa kusema....Mzee hawa wanaCCM ulionao wanatosha!! Hapa lazima tujiulize kidogo....
1. Kwanini mzee huyu kaamua kuzungumza hivo katika wakati huu ambapo tunaona wimbi kubwa la usajili wa wanachama wapya kutoka upinzani?
2. Kwanini anaona hamna umuhimu wa kuwa na wanachama wengi zaidi iwezekanavyo?
3. Mzee alikuwa anamwambia Rais kuwa upinzani kuwepo ndiyo uhai wa CCM na Taifa kwa ujumla?
Aliyeielewa kauli ile ya Mzee pinda,tusaidiane kuitafakari.
Sasa watu kama Mtulia au Msendo wana nini cha ziada sana sana ni kuleta wingi tu na si ubora!
 
Jana ulikuwa ni mwendo wa Mafumbo tu

Nae Mzee Makamba alisema Mzee Mwinyi,Mzee Kikwete,Comrade Kinana na Dkt Shein ni Waungwana hawawezi kutamka neno Pumbavu, kazi hiyo wamemuachia Mzee Mkapa ukumbi ukalipuka kwa kushangilia Sijui Kama walimuelewa Mzee Makamba?
 
Kuna jambo kubwa sana la kujifunza kupitia kauli hiyo ya mzee Pinda. Alitoa mfano wa China,anasema alijiuliza kuwa China inao watu takribani 1.3 B ,akataka kujua Communist Party (CP) itakuwa na wanachama wangapi? Anasema alistaajabu sana pale alipokuta chama kina wanachama milioni 80 tu. Ambayo hii 6% ya wachina wote walio wanachama wa CP.

Hapa kwetu Tanzania,CCM inao takribani wanachama milioni 6,ambao ni kama 11.5% ya Watanzania wote walio wanaCCM. Akazidi kusema kuwa kinachofanya chama kipendwe si kuwa na wanachama wengi,ni chama kujikita zaidi katika kutatua matatizo ya Wananchi,chama kuwa na viongozi waadilifu. Akasisitiza kwa kusema....Mzee hawa wanaCCM ulionao wanatosha!! Hapa lazima tujiulize kidogo.

1. Kwanini mzee huyu kaamua kuzungumza hivo katika wakati huu ambapo tunaona wimbi kubwa la usajili wa wanachama wapya kutoka upinzani?

2. Kwanini anaona hamna umuhimu wa kuwa na wanachama wengi zaidi iwezekanavyo?

3. Mzee alikuwa anamwambia Rais kuwa upinzani kuwepo ndiyo uhai wa CCM na Taifa kwa ujumla?

Aliyeielewa kauli ile ya Mzee pinda,tusaidiane kuitafakari.
Kauli ya Pinda ilikuwa nzuri sana,ila itakuwa hivyo tu kwa wale watakaoitafsri vizuri kwa maslahi mapana ya taifa.Kwa mtazamo wangu comment yake haikuwa na uhusiano wowote na wimbi la wanasiasa wanaohama vyama vingine kuingia CCM.Rather comment yake illilenga zaidi kwenye aspect ya uadilifu na weledi.Kwamba haijalishi chama kina wanachama wangapi,waliopo wakiwa waadilifu katika kiwango cha juu na pia wakawa na weledi wa hali ya juu,output itakuwa kubwa.Hii itasukuma maendeleo ya taifa mbele na hivyo chama kupendwa.Hiki ndicho kinachotokea kwa serikali ya CCM kwa sasa,sio kwamba watu wananunuliwa kama inavyodaiwa.Ni kwamba output inaonekana.

Nakiri kwamba more needs to be done in terms of removing corrupt elements inside the party without mercy,kitu ambacho alisisitiza.Chama bado kina too many corrupt officials and this needs to be tackled from the bottom. Naomba nikiri pia kwamba swala la weledi bado halitiliwi mkazo,it's more of who will take care of my interests na hili litakimaliza chama.Chama kinahitaji wazalendo,watu wenye weledi na uaminifu usiotiliwa shaka.Kunyooshewa kidole itoshe kumuondoa mtu CCM.

Hata hivyo mimi huwa nashindwa kabisa kuwaelewa viongozi wetu.They pretend to see problems when they are out of power.This trend has been so consistent with all government and political leaders and now with Pinda.Very hipocritical.

However so far so good.
 
Ccm ni Chama mfu kinacholazmisha kuishi kwa kutumia rasilimali za taifa na jeshi la police. Manunuzi yanaendlea cjui km PPRA wanahusishwa
 
Wameshajijua wanaoiunga mkono sisiyemu ni wachache sana hivyo wameamua tu kujifariji
 
Jana ulikuwa ni mwendo wa Mafumbo tu

Nae Mzee Makamba alisema Mzee Mwinyi,Mzee Kikwete,Comrade Kinana na Dkt Shein ni Waungwana hawawezi kutamka neno Pumbavu, kazi hiyo wamemuachia Mzee Mkapa ukumbi ukalipuka kwa kushangilia Sijui Kama walimuelewa Mzee Makamba?

Sasa taifa limejaa wajinga kuanzia watawala mpaka watawaliwa unategemea nini
 
Jana ulikuwa ni mwendo wa Mafumbo tu

Nae Mzee Makamba alisema Mzee Mwinyi,Mzee Kikwete,Comrade Kinana na Dkt Shein ni Waungwana hawawezi kutamka neno Pumbavu, kazi hiyo wamemuachia Mzee Mkapa ukumbi ukalipuka kwa kushangilia Sijui Kama walimuelewa Mzee Makamba?
Mzee mkapa alikunja sura baada ya kauli hiyo na katika hali ya kawaida maana yake makamba alimtangaza mkapa kuwa si muungwana aisee na mafumbo mengi sana yaliongelewa nanhawa wakongwe jana lakin kila la kheri iwa mwenye kiti
 
Jana ulikuwa ni mwendo wa Mafumbo tu

Nae Mzee Makamba alisema Mzee Mwinyi,Mzee Kikwete,Comrade Kinana na Dkt Shein ni Waungwana hawawezi kutamka neno Pumbavu, kazi hiyo wamemuachia Mzee Mkapa ukumbi ukalipuka kwa kushangilia Sijui Kama walimuelewa Mzee Makamba?
Sijui kama na wewe ulimuelewa Makamba
 
Back
Top Bottom