Mtoto wa mkulima ananyimwa mkopo wa fisadi anasoma katika chuo bora US!

TanzActive

JF-Expert Member
Nov 14, 2007
367
73
Jamani nimeona katika media jana picha hii

f1.jpg


kwamba mmoja wa mabinti hao ni mtoto wa fisadi fulani ,nikasononeka sana yaani watoto wa wakulima hapa wananyimwa mikopo na wale wa wezi wa pesa za wakulima wanatumia pesa hizo za wizi kusomesha watoto wao katika vyuo ghali kabisa duniani!!! Je haya ndo maisha bora kwa kila mtanzania?
 
Hakuna cha kustajabisha hapo kwani wanaowapigia kura ni hao wazee wa watoto wa kikulima kwa hilo inaonesha wameridhika nao na miendesho yao au kwa mana nyingine wamejikubalisha maisha yao yawe hivyo kuwatumikia wengine.
 
Ni kweli inabidi tufike sehemu tusiwaonee huruma kwani wao watawapigia kura ena 2010 bila kujali kinachoendelea nchini sasa, lazima watoto wao wakose vyuo kwanza kwa asira wataamua kuwawajibisha viongozi kwa kutumia sanduku la kura
 
Hakuna cha kustajabisha hapo kwani wanaowapigia kura ni hao wazee wa watoto wa kikulima kwa hilo inaonesha wameridhika nao na miendesho yao au kwa mana nyingine wamejikubalisha maisha yao yawe hivyo kuwatumikia wengine.


Jamani tusiwalaumu hao wazee wetu, historia mkuu, CCM imetumia ujanja huu wa uelewamdogo wa wananchi kutufikisha hapa tulipo. Cha msingi ni kuwa saidia hao wazee wetu kuwaelemisha ili nao waamke waweze kufanya jambo ili tutoke tulipo!

Hata hivo napenda niwatie moyo kwamba hapa tulipo si mbaya.. tunako enda ni kuzuri zaidi!. yanayotokea busanda hakuna aliye yategemea. Tutafika tu!
 
Wewe mtu ulieanzisha hii huna akili ata kidogo.. kwanza kabisa huyo mtoto wa karamagi unaesema its the wrong one. Na yule binti alie stanford anaakili vibaya sana. She did extremely well in her IGCSEs (A zote) akapata scholarship akaenda IST akasoma bure na kule pia anasoma bure.. Kamasio sheria za JF ningekuita Punda kwasababu inaonekana unaupungufu wa fikra.. acha kupayuka vitu usivyo vijua.
 
Wewe mtu ulieanzisha hii huna akili ata kidogo.. kwanza kabisa huyo mtoto wa karamagi unaesema its the wrong one. Na yule binti alie stanford anaakili vibaya sana. She did extremely well in her IGCSEs (A zote) akapata scholarship akaenda IST akasoma bure na kule pia anasoma bure.. Kamasio sheria za JF ningekuita Punda kwasababu inaonekana unaupungufu wa fikra.. acha kupayuka vitu usivyo vijua.


Kinyambis bana.................sasa umeshamwita umwite mara ngapi!!!
 
Wewe mtu ulieanzisha hii huna akili ata kidogo.. kwanza kabisa huyo mtoto wa karamagi unaesema its the wrong one. Na yule binti alie stanford anaakili vibaya sana. She did extremely well in her IGCSEs (A zote) akapata scholarship akaenda IST akasoma bure na kule pia anasoma bure.. Kamasio sheria za JF ningekuita Punda kwasababu inaonekana unaupungufu wa fikra.. acha kupayuka vitu usivyo vijua.

Umeguswa?????????Mbona ka' vile umepakawa pilipili au umekalia sindano!lol
 
Mkuu kwa namna moja ama nyingine tunasema unapo kipigia kura chama cha mapinduzi ina maana umeridhika na utawala huu wa hiki chama na umeridhika watoto wao wanao enda kula mabata mzinga UK na kwingineko huku wewe ada ya 20000/= shule ya kata aka yebo yebo inakutoa jasho. Wakulamiwa ni wewe mpiga kura unaye kubali haya na wewe ukiendelea kuteseka na kuwapa wao unacho chuma kwa jasho lako mwenyewe.
 
Its the wrong Karamagi, hako katoto kanako ongelewa nakafahamu dada yake alikuwa classmate wangu mda mrefu. SIo mtoto wa Nazir Karamagi. huyu kaona jina akaassume ndio ndio mwenyeew. Kilichoniudhi mimi nikwamba hakufanya any effort to confirm ameshutumu mtu ambae amefika alipofika kwa efforts zake na akili alizopewa na Mungu. Sasa kama tuna jazba kiasi cha kuto kukemea watu wanao operate kwa utaratibu huo basi tutakuwa taifa lisilo na tofauti na genge la wahuni. Mtu kapata A zote, sio mchezo sasa anasomea udaktari labda atakuja kutusadia wakati huo tuwazee.. Sio mtoto wa karamagi, simple as.. unless kama kuna karamagi mmoja duniani.lol
 
Wewe mtu ulieanzisha hii huna akili ata kidogo.. kwanza kabisa huyo mtoto wa karamagi unaesema its the wrong one. Na yule binti alie stanford anaakili vibaya sana. She did extremely well in her IGCSEs (A zote) akapata scholarship akaenda IST akasoma bure na kule pia anasoma bure.. Kamasio sheria za JF ningekuita Punda kwasababu inaonekana unaupungufu wa fikra.. acha kupayuka vitu usivyo vijua.

Wewe ndiye Karamagi?
 
Wewe ndiye Karamagi?

ukweli huu chini huyo dada mnamwonea


Return home after studies, Gvt tells Tanzanians abroad​
SUNDAY NEWS Reporter
Daily News; Saturday,August 16, 2008 @20:06

MINISTER of Education and Vocational Training, Prof Jumanne Maghembe, has called on Tanzanians studying abroad to return home after graduating, so they could serve the nation.

He made the comment when handing over 700m/- sponsorship to four students who were going to study at Stanford and Trinity universities.

Prof Maghembe said that there were several opportunities at home that would benefit them, their families and the nation as a whole if properly utilized.

“You should not be driven by the thought that when you work outside you will become rich faster. If you remain in the US you may work as a clerk for so long, something which may be different at home,” the minister said.

Prof Maghembe was speaking at a function to hand over air tickets to the four students. The function was held at Golden Tulip Hotel in Dar es Salaam recently. He counselled the students to maintain the spirit of performance they had previously shown.

The students who secured the 600,000 US dollars sponsorship were Wende Aman and Nellin Njovu from St. Francis Secondary School, Christine Karamagi from Academy International and Dushyant Pattni from Aga Khan Mzizima Secondary School.

The Stanford and Trinity universities have sponsored the students to pursue studies from 2008 to 2012. Ms Aman and Ms Karamagi would join Stanford University, while Ms Njovu and Mr Pattni would join Trinity University.

Prof Maghembe presented the air tickets worth 11,000 US dollars issued to students by IST Alumni Association, which carried out the interviews of the students with the participation of IST Management.

The association was formed several years ago with the valuable support from the International School of Tanganyika. It was aimed at, among other things, participating in charitable and community based projects in education, fund raising and advice.
 
mbona hii article is very clear... scholarship zimetolwea na shule hizo za US. Wapi hela za wakulima?
 
Jamani acheni majungu. Huyo binti namfahamu. Na nilimhoji kwa undani. Hana undugu wowote na Karamagi. Ni majina tu yamefanana. Alafu ni kweli huyu binti ni kichwa sana. Alafu anajituma sana. Niliwahi kukutana naye usiku wa manane katika harakati zake za kusoma wakati anajiandaa na huo mtihani wa mwisho. Na alifaulu sana na kupata skolashipu. Hivyo yuko huko Stanifodi Univesiti kwa skolashipu na sio kwa hela zenu walipa kodi wa Tanzania. Tuwe wakweli wakuu.
 
Ndio matatizo ya kukurupuka hayo halafu hawezi kuwa na ujasiri wa kuomba radhi.

Wenyewe wanaita kumkoma nyani giladi.....
 
Ndio matatizo ya kukurupuka hayo halafu hawezi kuwa na ujasiri wa kuomba radhi.

Wenyewe wanaita kumkoma nyani giladi.....

teh teh teh..huku sio kumkoma nyani giladi bali ni kudandia treni ya India kwa mbele..Sijui tatizo ni kuelewa kingereza au nini..
 
Hakuna cha kustajabisha hapo kwani wanaowapigia kura ni hao wazee wa watoto wa kikulima kwa hilo inaonesha wameridhika nao na miendesho yao au kwa mana nyingine wamejikubalisha maisha yao yawe hivyo kuwatumikia wengine.

Nimeipenda sana hii. ngoja nikatengeneze kikombe cha kahawa
 
lol! Watanzania wana hasira hadi wanaota ufisadi kila sehemu!
 
ujinga tuu na jazba zisizo na maana. Mwengine kaja na rabis yake hapa ananiita karamagi..hehehe.. Mwisho wasiku jazba hazitupeleki popote mtabaki kuongea vapour tuu.. Tuongelee jinsi ya kujenga Taifa imara sio kuwasimanga watoto wa watu especially ones with the brains that we need now and in the future. Christine is a smart young lady na baadae kama atakuwatayari kuwasaidia watanzania itakuwa jambo la kheri sana. Sijui mchukia fisadi na yule ambae nimekataa kumuita punda mtatusaidiaje zaidi ya kuongea MVUKE! hahahaha..aah aisee. Too funny.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom