JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,458
Mtoto mwenye umri wa miaka minne amenusurika kuumia baada ya kupata ajali ya gari alilokuwa akiendesha mtaani bila ruhusa kutoka kwa wazazi wake Nchini Uholanzi.
Polisi wa Kituo cha Utrecht wamesema mtoto huyo akikwangua gari hilo katika maeneo mawili ya kuegesha magari baada ya hapo akaondoka akilitelekeza huku akiwa peku.
Polisi wamesema, mtoto huyo alichukua funguo ya gari la mama, akaondoka nalo bila wazazi wake kujua. Polisi walipomkamata wakaenda naye kituoni, akajieleza, wakampa chokoleti kisha kumrudisha kwa mama yake ambaye hakuwa anajua mwanaye alipoelekea.
Alipoulizwa aliwezaje kuendesha gari akawaonesha alivyofanya kuanzia mwanzo ambapo alisema alikuwa akiona wazazi wake wanavyofanya. Wazazi wa mtoto huyo wameshauriwa kutoweka funguo za gari sehemu ya wazi.
Source: BBC