Mtoto wa Malecela amshukia Mukama

Alipigwa chini kura za maoni vibaya sana. Nadhani mpaka sasa utakuwa umeshazijuwa sababu.

Vipi, Josephine anaendelea kurekebisha "software" iliyoleta mapato "0" bungeni? Nasikia kitengo cha fedha kakishika yeye pale makao makuu, anaeleta "kwi" hakai. Source - TUNTEMEKE
Siwezi kuhangaika kubishana na mtu mwenye fungus za nyuma na kaswende ya Ubongo.
 
Kwa mtazamo wangu, sidhani kama siasa ni za kulazimisha! Matokeo huwa ni kinyume kabisa! Haya, ngoja tulisongeshe tuone hiyo 2015! Tujaaliwe uzima tu!
 
Baba ni baba na mwana ni mwana mpeni labda ataweza!

Nyota njema huonekana Alfajiri. Hana uwezo wa siasa za kisasa, inataka mtu machachari kama January, huyu anaonesha ni kijana mvivu sana, ambae hata kutembea kwake ni kujisukuma sukuma, hana mazoezi hana purukushani, siasa ni zaidi ya kukaa na kuandika mitandaoni kama Zomba.
 
Nyota njema huonekana Alfajiri. Hana uwezo wa siasa za kisasa, inataka mtu machachari kama January, huyu anaonesha ni kijana mvivu sana, ambae hata kutembea kwake ni kujisukuma sukuma, hana mazoezi hana purukushani, siasa ni zaidi ya kukaa na kuandika mitandaoni kama Zomba.

Hahahaha mie hapa sitii neno!
 
Huyu anadhani vyeo katika tanganyika vitaendelea kupeana kama ilivyo katika chama chao, asubiri tanganyika itakapokombolewa hapo 2015 ataona mazuri
 
- ha! Ha! Ha! Ha! Ha! Le biig shoow jf stress sydrome, so the biig shoow is still on! Ha! Ha! Ha1

i am humbled sana you know!!


Le biig shoow!!

Willy, what's wrong with you boy?
With no benefit of doubt, your thinking capacity seem to be below average!
 
Hii ni dhahiri kwamba mambo si shwari ndani ya CCM nijuavyo mimi zaidi ya makundi ya 2005 kuna evolving factions za Napeism na Mukamaism, moja likijifanya kujenga taswira safi na mpya ya chama ili kurejesha imani kwa wananchi bila kujali gharama na madhara kwa wazee waliochafuka kwa kashfa. Kundi la pili ni lile la wazee ambao hawakubaliani na hoja za Napeism kwa kuhofia kupoteza nafasi na maslahi yao. Vita hii ya kimtazamo inaonekana wazi kutokana na hoja zinazotolewa wazi kama afanyavyo W.Malechela. Kwa mtazamo wangu makundi haya mawili ndiyo yanayokwenda kuimaliza CCM 2015. Kinachoonekana wazi ni kwamba Napeism faction wameanza kujipambanua kwa kiongozi wake Nape kufanya kazi za kiutendaji zaidi ya uenezi jambo ambalo linazidi kuwachanganya Mukamaism faction. Hatari iliyopo ni kwamba Napeism haina uungwaji mkono sana kwenye ngazi za juu za maamuzi za chama kwani waliojaa huko ni Mukamaism. Tusubiri tuone mwisho wa huu msuguano
 
- ha! Ha! Ha! Ha! Ha! Le biig shoow jf stress sydrome,...

Le biig shoow!!

Willy, umenukuliwa ati huna tabia ya kuzunguka mbuyu, siamini katu. Naona u mnafiki kama Wana-CCM wenzako, mmeacha kile kiapo: "nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko."
Mzee Makamba alipokuwa K/Mkuu, wenzako wakasema kama ulivyonukuliwa; "amepitwa na wakati." Leo nawe wasema Mkama kapitwa na wakati! Ungekuwa mkweli ungekiri; tatizo la CCM ni M/kiti wenu aliyewateua Mzee Makamba na Mkama
 
Labda kama tumekariri na kuchagua watu wa kuongea points hata tuzikubali.

Sioni tatizo lolote katika mahojiano aliyoyafanya William, he is technically and logically right. Ssa nimeanza kuuona ukweli katika majibu yake kuwa watu wana wivu na mafanikio yake. Kama kuna mtu anadhani akiongeacho si sahihi na aanishe makosa hayo badala ya kuanza kumu attack mtu kwa sababu tu humpendi.....sawa inawezekane kabise asipendwe, Je ni sahihi kuruhusu chuki ku cloud akili na mitazamo yetu?

Mimi nampa BIG UP sana kwa mahojiano aliyoyafanya na kwa namna alivyochangia, kwani ni ukweli usio pingika.
Mukama alikuwa katika kamati iliyokuwa katika kutafuta chanzo cha CCM kupoteza mvuto wake mbele ya wananchi, aliifanya kazi ile vizuri na kukabidhi report ambayo kwa hakika haikuwa na Shaka.

Technical mistake ilifanywa na Mwenyekiti wa CCM mwenyewe (Kama ilivyo kawaida yake, kwani makosa ndiyo mambo pekee anayoweza kuyafanya kwa umakini kabisa na kuyarudia kila nafasi itakapojitokeza) kwa kumteua Mukama kuwa katibu wa CCM.....hapo nilitambua fika kuwa anguko la CCM limeingia katika stage ya 'The Must', kwani siku zote mimi nimekuwa nikiamini kuwa akili na mbinu iliyotumika katika kulivumbua tatizo si sahihi kutumika katika kulikabili, ndiyo maana kuna research projects, ambapo hizo projects zimalizapo kazi yake hutoa report ambayo baadaye hutumika katika Program implemtation.

Nadhani kama mwandishi hakuyaweka maneno hayo katika kinywa cha William Malecela, basi ni aina ya mtu tunaye muhitaji sana kama taifa, no matter what...
 
Huyu mwana JF mwenzetu hana mshiko kabisa. Hivi anaijuwa siasa au anapayuka tu? aliwahi kuwa hata mjumbe wa nyumba kumi kule NY?

Kumbe kuna wakati unakuwa na akili Zomba.Huyu jamaa ana tamaa sana na anadhani anaweza kuwa kama Mbowe .Ana msongo wa mawazo mno na kesha tamaa na anakumbuka shuka very late baridi kubwa ikiwa inaanza kumuumiza mwilini .
 
- ha! Ha! Ha! Ha! Ha! Le biig shoow jf stress sydrome, so the biig shoow is still on! Ha! Ha! Ha1

i am humbled sana you know!!


Le biig shoow!!

Wee mdogo wangu punguza mashambulizi, hivi Mukama akija hapo nyumbani kumsalimu mzee utakimbilia wapi...:hat::hat:
 
W.J. Malecela,

Ankoo umeshusha nondo safi kabisa maana unakipenda chama chako na bahati nzuri sana chama chako kina watu kama wewe, Nape na vijana wengine wanaofikiria siasa za Leo ambazo ni tofauti kabisa na enzi za Mwinyi wala Mkapa..

Ni lazima tukubali kwamba ktk kipindi hiki cha JK Upinzani umekuwa mgumu zaidi ya wakati wote uliopita. Enzi za kina Mrema watu walisema sana lakini ukifikiria kwa undani wake, Mrema alikuwa mtu wa Usalama wa Taifa na kuna kiapo chake, hivyo upinzani wake unakuwa na mipaka na mashindani tu. Angevunja kiapo chake hukumu yake ni Kifo, kwa hiyo alitumia zaidi siasa za ushindani na sii Upinzani.

Rais wetu Kikwete ni dhaifu ktk Uongozi wa nchi lakini ni mwanasiasa mzuri sana pengine mzuri kuliko wote waliotangulia, kwa sababu nina hakika hakuna kiongozi wa umri wa kina Mkama, Malecela na Wassira wanaweza kukubaliana na upinzani wa leo bila kutumia nguvu ya Urais, bila kumwaga damu za watu ama kuwasweka ndani wapinzani kila mara..Lakini JK kama mwanasiasa ameweza kusimama na siasa za leo vizuri tu akikubali kukosolewa na kuacha Upinzani ukomae badala ya kuudumaza.

Kuna watu wengi sana ndani ya CCM wanamlaumu JK kwa kuwa dhaifu kisiasa maana walichokitaka ni kumwona JK akitumia Urais, mkuu wa majeshi kama silaha ya kukilinda chama maana ndivyo tulivolelewa. Sasa inapofikia mahala chama kinataka kujitangaza chenyewe kwa sera zake ambazo kwa bahati mbaya zilitungwa toka tupate Uhuru hapo ndipo utata wa kinadharia unapojitokeza.

Mkuu wangu Willy labda nikufahamishe jambo moja kubwa sana na muhimu kulielewa. Nyie vijana mloingia CCM naweza kusema mumeingia chumba kisicho, mumeingia mlango wa chooni kwa sababu kwanza itikadi zenu ni tofauti kabisa na zile zinazotangazwa na chama.

Ni nyie vijana humuamini ktk siasa ya UJAMAA na KUJITEGEMEA halafu unamtaka Mkama ajiuzuru ilihali yeye anatetea misingi na malengo ya ujenzi wa dhamira ya chama toka kiundwe!..Nani kati yenu kisiasa anatakiwa kujikata?..Bila shaka watu kama nyie ndio hamtakiwi CCM kwa sababu hamuungi mkono madhumuni ya chama isipokuwa mnataka kupandikiza yenu kulingana na wakati. Toka Ujio wa Lowassa ndani ya CCM kumekuwepo na misuguano ya chama ambayo wengi wenu mnafikiria yanatokana na uchaguzi wa mwaka 2005.

Lakini mnachoshindwa kufahamu ni kwamba misuguano hiyo imetokana na tofauti zenu Kiitikadi toka 1992 ujio wa Azimio la Zanzibar..Nusu yenu wanakubalianana na madhumuni 18 ya CCM na nusu yenu hasa matajiri hawakubaliani na baadhi ya madhumuni ya chama hivyo nguvu ya ushindani inaanza toka ndani.

Please kama unayo nafasi soma Katiba yenu au kwa kifupi soma Madhumuni ya CCM halafu nambie kama kweli wewe unakubaliana nayo kulingana na record yako hapa JF..Nitaweka madhumuni machache nayoyakumbuka hukubaliani nayo:-

1. Dhumuni la 3 linasema - Kuhimiza ujenzi wa Ujamaa na Kujitegemea kwa mujibu wa Azimio la Arusha.

2. Dumuni la 4 - Kusimamia utekelezaji wa Siasa ya CCM pamoja na kuendeleza fikra za viongozi waasisi wavyama vya TANU na ASP, kama zilivyofafanuliwa katika maandiko mbali mbali ya Vyama hivyo.

3. Dhumuni la 7 - Kusimamia haki na maendeleo ya Wakulima, Wafanyakazi na wananchi wengine wenye shughuli halali za kujitegemea; na hasa kuona kwamba kila mtu ana haki ya kupata malipoyanayostahili kutokana na kazi yake.

4. Dhumuni la 9 - Kuona kwamba Nchi yetu inatawaliwa kwa misingi ya kidemokrasia na ya kijamaa.

5. Dhumuni la 13 - Kuona kwamba Serikali na Vyombo vyote vya Umma vinasaidia kwa vitendo kuanzishwa na kuendeleza shughuli za Ushirika na za ujamaa, na shughuli nyinginezo halali za wananchi zakujitegemea.

6. Dhumuni la 17 - Kuendelea kupiga vita Ukoloni Mamboleo, Ubeberu na Ubaguzi wa aina yoyote.

7. Dhumuni la 18 - Kuimarisha uhusiano mwema na Vyama vyote vya Siasa vya Nchi nyingine vyenye itikadi kama ya CCM ambavyo kweli vinapinga Ukoloni, Ukoloni Mamboleo, Ubeberu na Ubaguzi waaina yoyote.

Haya yote 7...ni kati ya madhumuni yanayokitengeneza chama cha Mapinduzi na kwa bahati mbaya sana kuna watu wengi sana ndani ya CCM ambao hawakubaliani na madhumuni haya lakini wako radhi kujaribu kukibadilisha chama kiitikadi, waweke yao pinzani jambo ambalo sijawahi kuliona Duniani.

Kilichotakiwa kufanyika ni kwamba wale wote wasiokubaliana na misingi hii ndio walitakiwa kujiengua na kuwaacha wanao amini misnigi na madhumuni haya. Sasa kutokana na watu kama kina Lowassa, Mkapa na wahuni wengine waliokivamia chama hiki, ndio maana umeona sisi wengine tukakimbia mapemaaa.

Kiitikadi hayo yote yaliyoorodheshwa hapo juu mimi ninayakubali tofati kabisa na wewe, lakini siko CCM kwa sababu misingi ya ujenzi wa chama hicho imekwisha ingiliwa na wahuni na kuharibika. Hivyo siasa za CCM zinaendeshwa kiholela na sidhani kama makosa ya kina Mkama, vijana au wazee bali kuna watu wenye fikra mbili tofauti zinazopingana kiitikadi na zimekutana ndani ya chama kimoja - Only in Tanzania.
Think again, mkuu utakisafisha vipi chama kama hiki?
 
Kweli ukubwa wa pua si wingi wa makamasi,

Mosi there is no way utazungumzi kuhusu Katibu Mkuu wa Chama ukamwacha Mwenyekiti wa Chama husika na sababu kubwa ni kwamba yeye (Mwenyekiti) ndiye aliyemteua hivyo kama Katibu haendani na siasa za wakari huu Mwenyekiti vile vile yumo katika kundi hilo.

Lakini la pili sijui ni katika minajili ipi mtu anaweza kusimama na kusema eti Nape anafanya kazi nzuri na anaendana na Siasa za nyakati hizi; hivi ni kwa jinsi anavyo copy na kupaste fikra za watu?? Wenzio wamekaa kibunifu wewe unaogelea ndani ya huo ubunifu badala ya kutafuna namna na wewe uweze kuwa mbunifu, mathalan wenzio wanasema "vua gamba vaa gwanda" wewe unakuja kuchomekea ati "vua gamba vua gwanda vaa uzalendo" hiki ni kituko moja kwa moja.

Hakuna namna waweza mfananisha Nape na January labda katika matakwa ya urafiki na si vinginevyo.Zaidi ya Siasa kuna ubunifu yakinifu na kuzingatia mahitaji ya watu kwa wakati husika.

Hii Nchi bana kila mtu anajua kila kitu ila wakati mwingine mtu ujitahidi kusema kidogo kuhusu mambo mengi si unasema tuuuuu kwa sababu ya ubatizo......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom