Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
KUKOSEKANA kwa mafuta ya petroli jana kulizua tafrani kubwa kwa wakazi wa Jiji la Dar es alaam baada ya vituo vingi vinavyouza nishati hiyo kugoma kutoa huduma hiyo. Misururu mingi ya magari hasa madogo ilionekana kila kona ya jiji, huku ikituhumiwa kuwa wamiliki wa vituo vya mafuta walikuwa wakitii agizo la mtoto wa kigogo mmoja wa serikali ambaye anadaiwa kuwashawishi baadhi ya wafanyabiashara kusitisha uuuzaji wa nishati hiyo, kama njia ya kupinga bei mpya ya kikomo iliyotangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).
Inadaiwa kwamba mtoto huyo wa kigogo ana uhusiano mkubwa na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wa mafuta, na inadaiwa pia kuwa ana hisa katika baadhi ya makampuni. Vituo vingi juzi na jana vilikuwa vikiuza dizeli na mafuta ya taa tu, huku vikidai kutokuwa na mafuta ya petroli kwa madai ya kuishiwa.
Hata hivyo, EWURA imetishia kuvichukulia hatua kali vituo vya mafuta vitakavyobainika kugoma kuuza nishati hiyo, na kudai kuwa ndio pekee wanaoweza kutamka kukosekana kwa mafuta, hivyo basi hakuna haja kwa umma kupata hofu na kuanza kujazana kwenye vituo vya mafuta kujaza mafuta zaidi, kwani kwa kufanya hivyo, kunaharibu mfumo mzima wa usambazaji wa mafuta.
Tanzania Daima 20/12/2011
Maoni yanguInadaiwa kwamba mtoto huyo wa kigogo ana uhusiano mkubwa na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wa mafuta, na inadaiwa pia kuwa ana hisa katika baadhi ya makampuni. Vituo vingi juzi na jana vilikuwa vikiuza dizeli na mafuta ya taa tu, huku vikidai kutokuwa na mafuta ya petroli kwa madai ya kuishiwa.
Hata hivyo, EWURA imetishia kuvichukulia hatua kali vituo vya mafuta vitakavyobainika kugoma kuuza nishati hiyo, na kudai kuwa ndio pekee wanaoweza kutamka kukosekana kwa mafuta, hivyo basi hakuna haja kwa umma kupata hofu na kuanza kujazana kwenye vituo vya mafuta kujaza mafuta zaidi, kwani kwa kufanya hivyo, kunaharibu mfumo mzima wa usambazaji wa mafuta.
Tanzania Daima 20/12/2011
Hatukatazi mtoto/ndugu/jamaa wa kigogo yeyote serikalini kufanya biashara, hasa biashara halali, ila utata unajitokeza pale tu ambapo mtoto/ndugu/jamaa ya kiongozi yeyote awaye nchini anayetumia influence/wadhifa wa mzazi/ndugu yake kutusumbua /kutunyonya/kutuibia. Ikifikia point hiyo ya mtu kutumia wadhifa wa mzazi wake kuinyonya nchi, ndipo wanawanchi huanza kuchoka na hata kuanziasha chuki dhidi ya watu hawa. Wahenga walisema ukila na kipofu usimshike mkono, ila kwa staili hii naona wameamua kukamata kabisa mkono wa kipofu usiingizwe tena kwenye bakuli. Ole wenu mnaotufanyia mchezo huu, naimani ipo siku tutaamua kuharibu hizo biashara zinazowapa jeuri hii ya kifisadi. Kwanza mitaji ya biashara hizo most likely mmetuibia, pili biashara hizo mnaendesha kwa magumashi so hatutasita kuziharibu mana zinatokana na fedha za kifisadi mnazotuibia kila kukicha. Hivyo ni vyema mkajua kuwa tunafahamu A to Z kuhusu mnayoyafanya na hivyo ni vyema muoperate in low profile.